Add parallel Print Page Options

Mafundisho ya Yesu Mlimani

(Lk 6:20-23)

Yesu alipoyaona makundi ya watu, alipanda kwenye kilima na kukaa chini. Wanafunzi wake walimjia Yesu. Kisha Yesu akaanza kuwafundisha watu kwa akasema:

“Heri[a] kwa walio maskini na wenye kujua kwamba wanamhitaji Mungu.[b]
    Kwa kuwa ufalme wa Mungu ni wao.
Heri kwa wenye huzuni sasa.
    Kwa kuwa watafarijiwa na Mungu.
Heri kwa walio wapole.
    Kwa kuwa watairithi nchi.[c]
Heri kwa wenye kiu na njaa ya kutenda haki.[d]
    Kwa kuwa Mungu ataikidhi kiu na njaa yao.
Heri kwa wanaowahurumia wengine.
    Kwa kuwa watahurumiwa pia.
Heri kwa wenye moyo safi,[e]
    Kwa kuwa watamwona Mungu.
Heri kwa wanaotafuta amani.[f]
    Kwa kuwa wataitwa watoto wa Mungu.
10 Heri kwa wanaoteswa kwa sababu ya kutenda haki.
    Kwa kuwa ufalme wa Mungu ni wao.

11 Heri kwenu ninyi pale watu watakapowatukana na kuwatesa. Watakapodanganya na akasema kila neno baya juu yenu kwa kuwa mnanifuata mimi. 12 Furahini na kushangilia kwa sababu thawabu kuu inawasubiri mbinguni. Furahini kwa kuwa ninyi ni kama manabii walioishi zamani. Watu waliwatendea wao mambo mabaya kama haya pia.

Ninyi ni Kama Chumvi na Nuru

(Mk 9:50; 4:21; Lk 14:34-35; 8:16)

13 Mnahitajika kama chumvi inavyohitajiwa na wale waliopo duniani. Lakini chumvi ikipoteza ladha yake, haiwezi kufanywa chumvi tena. Haina manufaa yo yote isipokuwa hutupwa nje na kukanyagwa na watu.

14 Ninyi ni nuru inayong'aa ili ulimwengu uweze kuiona. Ni kama mji uliojengwa juu ya kilima unavyoonekana wazi. 15 Watu hawawashi taa na kuificha kwenye chungu. Bali huiweka kwenye kinara cha taa ili nuru iangaze kwa kila mtu. 16 Kwa namna hiyo hiyo mnapaswa kuwa nuru kwa ajili ya watu wengine. Hivyo ishini katika namna ambayo watakapoyaona matendo yenu mema, watamtukuza Baba yenu wa mbinguni.

Yesu Afundisha Kuhusu Sheria ya Musa

17 Msifikiri kwamba nimekuja kuiharibu Sheria ya Musa au mafundisho ya manabii. Sikuja kuyaharibu mafundisho yao bali kuyakamilisha. 18 Ninawahakikishia kuwa hakuna jambo litakaloondolewa katika sheria mpaka mbingu na nchi zitakapopita. Hakuna hata herufi ndogo ama nukta katika Sheria ya Musa itakayotoweka mpaka hapo itakapotimizwa.

19 Kila mtu anapaswa kutii kila amri iliyo katika sheria, hata ile isiyoonekana kuwa ya muhimu. Kila atakayevunja mojawapo ya amri hizi ndogo na kuwafundisha wengine kuzivunja atahesabiwa kuwa ni mdogo sana katika ufalme wa Mungu. Lakini kila anayeitii na kuwafundisha wengine kuitii sheria atakuwa mkuu katika ufalme wa Mungu. 20 Ninawambia, ni lazima muitii sheria ya Mungu kwa kiwango bora kuliko kile cha walimu wa sheria na Mafarisayo. La sivyo, hamtaweza kuingia katika ufalme wa Mungu.

Yesu Afundisha Kuhusu Hasira

21 Mmesikia kuwa hapo kale baba zetu waliambiwa, ‘Usimwue yeyote. Na yeyote atakayeua atahukumiwa.’(A) 22 Lakini ninawaambia, msimkasirikie mtu yeyote kwa sababu mkifanya hivyo mtahukumiwa. Na mkimtukana mtu yeyote, vivyo hivyo mtahukumiwa na baraza kuu. Na ukimwita mtu kuwa ni mjinga, utakuwa katika hatari ya kutupwa kwenye moto wa Jehanamu.

23 Unapokwenda kutoa sadaka yako madhabahuni na ukakumbuka kuwa kuna mtu ana jambo dhidi yako. 24 Unapaswa kuiacha sadaka yako kwenye madhabahu na uende kupatana na mtu huyo. Ukiisha patana naye ndipo urudi na kuitoa sadaka hiyo.

25 Akiwepo mtu anayetaka kukushtaki, patana naye haraka. Jitahidi kufanya hivyo kabla ya kufika mahakamani, hata kama bado mpo njiani. Usipofanya hivyo anaweza kukupeleka kwa hakimu. Na hakimu atakupeleka kwa walinzi watakaokufunga gerezani. 26 Ninakuhakikishia kuwa hautatoka huko mpaka umelipa kila kitu unachodaiwa.

Yesu Afundisha Kuhusu Uzinzi

27 Mmesikia ilisemwa kuwa, ‘Usizini’.(B) 28 Lakini ninawaambia kuwa mwanaume akimwangalia mwanamke na akamtamani, amekwisha kuzini naye katika akili yake. 29 Jicho la kuume likikufanya utende dhambi, liondoe na ulitupe. Ni bora kupoteza sehemu moja ya mwili wako kuliko mwili wako wote ukatupwa Jehanamu. 30 Na mkono wako wa kuume ukikufanya utende dhambi, uukate na kuutupa. Ni bora kupoteza sehemu moja ya mwili wako kuliko mwili wako wote kutupwa Jehanamu.

Yesu Afundisha Kuhusu Talaka

(Mt 19:9; Mk 10:11-12; Lk 16:18)

31 Ilisemwa pia kuwa, ‘Kila anayemtaliki mkewe ni lazima ampe hati ya talaka.’(C) 32 Lakini ninawaambia kuwa, kila atakayemtaliki mkewe kutokana na sababu isiyohusiana na uzinzi, anamfanya mke wake kuwa mzinzi. Na kila atakayemwoa mwanamke aliyetalikiwa, atakuwa anazini.

Yesu Afundisha Kuhusu Kiapo

33 Pia, mmesikia hapo kale baba zetu waliambiwa, ‘Unaweka kiapo, usishindwe kutimiza kile ulichoapa kufanya. Timiza kiapo ulichoweka mbele za Bwana.’ 34 Lakini ninawaambia mnapoweka ahadi, msiape kwa jina la mbingu, kwa sababu mbingu ni kiti cha enzi cha Mungu. 35 Na usiape kwa jina la dunia kwa sababu, dunia ni mahali pa kuweka miguu yake. Wala msiape kwa jina la mji wa Yerusalemu, kwa sababu nao ni mali yake Mungu, aliye Mfalme Mkuu. 36 Pia usiape kwa jina la kichwa chako kana kwamba ni uthibitisho kuwa utatimiza kiapo, kwa sababu huwezi kuufanya hata unywele mmoja wa kichwa chako kuwa mweusi au mweupe. 37 Sema ‘ndiyo’ tu kama una maana ya ndiyo na ‘hapana’ tu kama una maana ya hapana. Ukisema zaidi ya hivyo, utakuwa unatoa kwa Yule Mwovu.

Yesu Afundisha Kuhusu Kisasi

(Lk 6:29-30)

38 Mmesikia ilisemwa, ‘Jicho kwa jicho na jino kwa jino.’(D) 39 Lakini ninawaambia msishindane na yeyote anayetaka kuwadhuru. Mtu akikupiga shavu la kulia mgeuzie na la kushoto pia. 40 Mtu akitaka kukushitaki ili akunyang'anye shati, mpe na koti pia. 41 Askari akikulazimisha kwenda naye maili moja,[g] nenda maili mbili pamoja naye. 42 Mpe kila anayekuomba, usimkatalie anayetaka kuazima kitu kwako.

Wapende Adui Zako

(Lk 6:27-28,32-36)

43 Mmesikia ilisemwa kuwa, ‘Wapende rafiki zako(E) na wachukie adui zako.’ 44 Lakini ninawaambia wapendeni adui zenu na waombeeni wale wanaowatendea vibaya. 45 Mkifanya hivi mtakuwa watoto halisi walio kama Baba yenu wa mbinguni. Yeye huwaangazia jua watu wote, bila kujali ikiwa ni wema au wabaya. Huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki. 46 Ikiwa mnawapenda wale wanaowapenda ninyi, kwa nini mpate thawabu toka kwa Mungu? Hata watoza ushuru hufanya hivyo. 47 Na ikiwa mnakuwa wema kwa rafiki zenu tu, ninyi si bora kuliko wengine. Hata watu wasiomjua Mungu ni wakarimu kwa rafiki zao pia. 48 Ninalosema ni kuwa, mkue hata kufikia upendo kamili[h] alionao baba yenu wa Mbinguni kwa watu wote.

Footnotes

  1. 5:3 Heri Maana yake ni baraka kuu.
  2. 5:3 maskini … wanamhitaji Mungu Kwa maana ya kawaida, “maskini wa roho”, ama wenye uhitaji wa kiroho.
  3. 5:5 watairithi nchi Wataurithi ulimwengu ujao yaani ufalme wa Mungu unaokuja.
  4. 5:6 wenye kiu na njaa ya kutenda haki Kwa maana ya kawaida, “wenye njaa na kiu ya kutenda haki zaidi ya kitu kingine chochote”.
  5. 5:8 wenye moyo safi Au wenye mawazo safi ama wenye kukusudia mema moyoni, ama wenye nia njema moyoni.
  6. 5:9 wanaotafuta amani Au “wapatanishi wa watu waliofarakana”.
  7. 5:41 maili moja Kama kilomita moja na nusu.
  8. 5:48 kamili Neno “kamilifu”, hapa lina maana “imeendelezwa kwa ukamilifu”, na inaelezea aina ya upendo ambao watoto wanaweza kujifunza kutoka kwa baba.

Yerusalemu, Yudea na kutoka ng’ambo ya mto Yordani.

Yesu alipoona umati wa watu, alipanda mlimani akaketi chini. Wanafunzi wake wakamjia, naye akaanza kuwafundisha akisema:

“Wamebarikiwa walio maskini wa roho; maana Ufalme wa mbin guni ni wao. Wamebarikiwa wanaoomboleza; maana watafarijiwa. Wamebarikiwa walio wapole; maana watairithi nchi. Wamebari kiwa wenye hamu ya kutenda haki; maana wataridhishwa. Wamebari kiwa walio na huruma; maana nao watahurumiwa. Wamebarikiwa walio na moyo safi; maana watamwona Mungu. Wamebarikiwa walio wapatanishi; maana wataitwa wana wa Mungu. 10 Wamebarikiwa wanaoteswa kwa kutenda haki; maana Ufalme wa mbinguni ni wao.

11 Mmebarikiwa ninyi wakati watu watakapowatukana na kuwatesa na kuwasingizia maovu kwa ajili yangu. 12 Shangilieni na kufurahi, kwa maana zawadi yenu huko mbinguni ni kubwa; kwa kuwa ndivyo walivyowatesa manabii waliowatangulia ninyi.

13 “Ninyi ni chumvi ya ulimwengu. Lakini chumvi ikipoteza ladha yake, haiwezekani kuwa chumvi tena. Haifai kwa kitu cho chote, ila kutupwa nje ikanyagwe na watu.

14 “Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji uliojengwa kwenye mlima haufichiki. 15 Wala hakuna mtu anayewasha taa kisha akaifunika. Badala yake, huiweka mahali pa juu ili itoe mwanga kwa kila mtu aliyemo ndani ya nyumba. 16 Hali kadhalika, nuru yenu iwaangazie watu ili waone matendo yenu mema wamtukuze Baba yenu aliye mbin guni.’

Mafundisho Kuhusu Sheria

17 “Msidhani kwamba nimekuja kufuta sheria ya Musa na mafundisho ya manabii. kwamba mpaka mbingu na dunia zitaka potoweka, hakuna hata herufi moja ya sheria itakayopotea mpaka shabaha yake ikamilike. 19 Kwa hiyo ye yote atakayelegeza hata mojawapo ya amri ndogo kuliko amri zote na akawafundisha wengine kufanya hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika Ufalme wa mbinguni. Sikuja kuzifuta bali kuzitimiza. 18 Kwa maana ninawaambia hakika Lakini atakayetii amri hizi na kuwafundisha wengine kuzitii a taitwa mkuu katika Ufalme wa mbinguni. 20 Kwa maana nawaambieni, ikiwa haki yenu haitazidi haki ya waandishi wa sheria na Mafari sayo, hamtaingia katika Ufalme wa mbinguni kamwe.”

Mafundisho Kuhusu Hasira

21 “Mmesikia walivyowafundisha watu wa zamani kwamba, ‘Usiue; na ye yote atakayeua atastahili hukumu.’ 22 Lakini mimi nawaambia kwamba, ye yote atakayemkasirikia ndugu yake atasta hili hukumu; na ye yote atakayemtukana ndugu yake, atashtakiwa katika baraza; na ye yote atakayemwambia ndugu yake, ‘Wewe mjinga,’ atastahili hukumu ya moto wa Jehena.

23 “Basi, kama ulikuwa tayari kutoa sadaka yako madhaba huni, ukakumbuka kuwa ndugu yako amekukasirikia, 24 acha sadaka yako hapo hapo, uende kwanza ukapatane naye, kisha urudi kumtolea Mungu sadaka yako. 25 “Mtu akikushtaki, patana naye kabla hamjafika mahaka mani; ili mshtaki wako asije akakukabidhi kwa hakimu, na hakimu akamwamuru askari akufunge gerezani; 26 nami nawaambia hakika, hutatoka huko mpaka deni lako lote litakapolipwa.”

Mafundisho Kuhusu Uzinzi

27 “Mmesikia walivyowafundisha watu wa zamani kwamba, ‘Usi zini’. 28 Lakini mimi nawaambia: ye yote atakayemwangalia mwa namke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake. 29 Jicho lako la kulia likikufanya utende dhambi, ling’oe ulitu pilie mbali. Ni afadhali upoteze sehemu ya mwili wako kuliko mwili mzima utupwe Jehena. 30 Na kama mkono wako wa kuume ukiku fanya utende dhambi, ukate uutupilie mbali. Ni afadhali upoteze sehemu ya mwili wako kuliko mwili mzima utupwe Jehena.

31 “Pia mliambiwa kwamba, ‘Mtu ye yote anayemwacha mkewe ampe talaka.’ 32 Lakini mimi nawaambia, ye yote atakayempa mkewe talaka isipokuwa kwa kosa la uasherati, anamfanya mkewe mzinzi. Na ye yote atakayemwoa mwanamke aliyepewa talaka anazini.”

Mafundisho Kuhusu Kuapa

33 “Tena mmesikia watu wa kale waliambiwa kwamba, ‘Usi vunje kiapo chako bali umtimizie Mungu kama ulivyoapa kutenda.’ 34 Lakini mimi nawaambia, msiape kabisa, ama kwa mbingu, kwa sababu ni kiti cha enzi cha Mungu, 35 au kwa ardhi, kwa sababu ndipo mahali pake pa kuwekea miguu, au kwa Yerusalemu kwa sababu ndio mji wa Mfalme mkuu. 36 Na msiape kwa vichwa vyenu kwa sababu hamwezi kugeuza hata unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi. 37 Ukisema ‘Ndio’ basi iwe ‘Ndio’; na ukisema ‘Hapana’ basi iwe ‘ Hapana.’ Lo lote zaidi ya haya hutoka kwa yule mwovu.”

Mafundisho Kuhusu Kulipiza Kisasi

38 “Mmesikia kuwa watu zamani walikuwa wakisema, ‘Jicho kwa jicho na jino kwa jino.’ 39 Lakini mimi nawaambia, msishindane na mtu mwovu. Lakini mtu akikupiga kwenye shavu la kulia, mgeuzie na shavu la kushoto pia; 40 na kama mtu akitaka kukushtaki achukue shati lako, mwachie achukue na koti pia. 41 Na kama mtu akikulazimisha uende kilometa moja naye, fanya zaidi, nenda naye kilometa mbili. 42 Mtu akikuomba kitu mpe, na usikatae kumsaidia mtu anayetaka kukukopa.”

Wapendeni Maadui Zenu

43 “Mmesikia kuwa watu zamani walikuwa wakisema, ‘Umpende jirani yako na umchukie adui yako.’ 44 Lakini mimi ninawaambia, wapendeni maadui zenu na waombeeni wanaowatesa, 45 ili mpate kuwa watoto wa Baba yenu aliye mbinguni. Kwa maana yeye huwaanga zia jua lake watu waovu na watu wema; na pia huleta mvua kwa wenye haki na wasio haki. 46 Kama mkiwapenda wanaowapenda tu, mtapata thawabu gani? Hata wenye dhambi hufanyiana hivyo. 47 Na kama mkiwasalimu ndugu zenu tu, mnafanya nini zaidi ya wengine? Hata watu wa mataifa wasiomjua Mungu, hufanya hivyo. 48 Kwa hiyo inawapasa ninyi muwe wakamilifu kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.”

The Beatitudes(A)

And seeing the multitudes, (B)He went up on a mountain, and when He was seated His disciples came to Him. Then He opened His mouth and (C)taught them, saying:

“Blessed(D) are the poor in spirit,
For theirs is the kingdom of heaven.
(E)Blessed are those who mourn,
For they shall be comforted.
(F)Blessed are the meek,
For (G)they shall inherit the [a]earth.
Blessed are those who (H)hunger and thirst for righteousness,
(I)For they shall be filled.
Blessed are the merciful,
(J)For they shall obtain mercy.
(K)Blessed are the pure in heart,
For (L)they shall see God.
Blessed are the peacemakers,
For they shall be called sons of God.
10 (M)Blessed are those who are persecuted for righteousness’ sake,
For theirs is the kingdom of heaven.

11 (N)Blessed are you when they revile and persecute you, and say all kinds of (O)evil against you falsely for My sake. 12 (P)Rejoice and be exceedingly glad, for great is your reward in heaven, for (Q)so they persecuted the prophets who were before you.

Believers Are Salt and Light(R)

13 “You are the salt of the earth; (S)but if the salt loses its flavor, how shall it be seasoned? It is then good for nothing but to be thrown out and trampled underfoot by men.

14 (T)“You are the light of the world. A city that is set on a hill cannot be hidden. 15 Nor do they (U)light a lamp and put it under a basket, but on a lampstand, and it gives light to all who are in the house. 16 Let your light so shine before men, (V)that they may see your good works and (W)glorify your Father in heaven.

Christ Fulfills the Law

17 (X)“Do not think that I came to destroy the Law or the Prophets. I did not come to destroy but to fulfill. 18 For assuredly, I say to you, (Y)till heaven and earth pass away, one [b]jot or one [c]tittle will by no means pass from the law till all is fulfilled. 19 (Z)Whoever therefore breaks one of the least of these commandments, and teaches men so, shall be called least in the kingdom of heaven; but whoever does and teaches them, he shall be called great in the kingdom of heaven. 20 For I say to you, that unless your righteousness exceeds (AA)the righteousness of the scribes and Pharisees, you will by no means enter the kingdom of heaven.

Murder Begins in the Heart(AB)

21 “You have heard that it was said to those [d]of old, (AC)‘You shall not murder, and whoever murders will be in danger of the judgment.’ 22 But I say to you that (AD)whoever is angry with his brother [e]without a cause shall be in danger of the judgment. And whoever says to his brother, (AE)‘Raca!’[f] shall be in danger of the council. But whoever says, [g]‘You fool!’ shall be in danger of [h]hell fire. 23 Therefore (AF)if you bring your gift to the altar, and there remember that your brother has something against you, 24 (AG)leave your gift there before the altar, and go your way. First be reconciled to your brother, and then come and offer your gift. 25 (AH)Agree with your adversary quickly, (AI)while you are on the way with him, lest your adversary deliver you to the judge, the judge hand you over to the officer, and you be thrown into prison. 26 Assuredly, I say to you, you will by no means get out of there till you have paid the last penny.

Adultery in the Heart

27 “You have heard that it was said [i]to those of old, (AJ)‘You shall not commit adultery.’ 28 But I say to you that whoever (AK)looks at a woman to lust for her has already committed adultery with her in his heart. 29 (AL)If your right eye causes you to [j]sin, (AM)pluck it out and cast it from you; for it is more profitable for you that one of your members perish, than for your whole body to be cast into hell. 30 And if your right hand causes you to [k]sin, cut it off and cast it from you; for it is more profitable for you that one of your members perish, than for your whole body to be cast into hell.

Marriage Is Sacred and Binding(AN)

31 “Furthermore it has been said, (AO)‘Whoever divorces his wife, let him give her a certificate of divorce.’ 32 But I say to you that (AP)whoever divorces his wife for any reason except [l]sexual immorality causes her to commit adultery; and whoever marries a woman who is divorced commits adultery.

Jesus Forbids Oaths

33 “Again you have heard that (AQ)it was said to those of [m]old, (AR)‘You shall not swear falsely, but (AS)shall perform your oaths to the Lord.’ 34 But I say to you, (AT)do not swear at all: neither by heaven, for it is (AU)God’s throne; 35 nor by the earth, for it is His footstool; nor by Jerusalem, for it is the city of (AV)the great King. 36 Nor shall you swear by your head, because you cannot make one hair white or black. 37 (AW)But let [n]your ‘Yes’ be ‘Yes,’ and your ‘No,’ ‘No.’ For whatever is more than these is from the evil one.

Go the Second Mile(AX)

38 “You have heard that it was said, (AY)‘An eye for an eye and a tooth for a tooth.’ 39 (AZ)But I tell you not to resist an evil person. (BA)But whoever slaps you on your right cheek, turn the other to him also. 40 If anyone wants to sue you and take away your tunic, let him have your cloak also. 41 And whoever (BB)compels you to go one mile, go with him two. 42 Give to him who asks you, and (BC)from him who wants to borrow from you do not turn away.

Love Your Enemies(BD)

43 “You have heard that it was said, (BE)‘You shall love your neighbor (BF)and hate your enemy.’ 44 [o]But I say to you, (BG)love your enemies, bless those who curse you, (BH)do good to those who hate you, and pray (BI)for those who spitefully use you and persecute you, 45 that you may be sons of your Father in heaven; for (BJ)He makes His sun rise on the evil and on the good, and sends rain on the just and on the unjust. 46 (BK)For if you love those who love you, what reward have you? Do not even the tax collectors do the same? 47 And if you greet your [p]brethren only, what do you do more than others? Do not even the [q]tax collectors do so? 48 (BL)Therefore you shall be perfect, just (BM)as your Father in heaven is perfect.

Footnotes

  1. Matthew 5:5 Or land
  2. Matthew 5:18 Gr. iota, Heb. yod, the smallest letter
  3. Matthew 5:18 The smallest stroke in a Heb. letter
  4. Matthew 5:21 in ancient times
  5. Matthew 5:22 NU omits without a cause
  6. Matthew 5:22 Lit., in Aram., Empty head
  7. Matthew 5:22 Gr. More
  8. Matthew 5:22 Gr. Gehenna
  9. Matthew 5:27 NU, M omit to those of old
  10. Matthew 5:29 Lit. stumble or offend
  11. Matthew 5:30 Lit. stumble or offend
  12. Matthew 5:32 Or fornication
  13. Matthew 5:33 ancient times
  14. Matthew 5:37 Lit. your word be yes yes
  15. Matthew 5:44 NU But I say to you, love your enemies and pray for those who persecute you
  16. Matthew 5:47 M friends
  17. Matthew 5:47 NU Gentiles