Matendo 4
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Mitume Mbele ya Baraza Kuu la Wayahudi
4 Petro na Yohana walipokuwa wanazungumza na watu, ghafla baadhi ya viongozi wa Kiyahudi waliwaendea. Walikuwepo baadhi ya makuhani, mkuu wa askari wanaolinda Hekalu na baadhi ya Masadukayo. 2 Walikasirika kwa sababu ya mafundisho ambayo Petro na Yohana walikuwa wanawafundisha na kuwaambia watu kuhusu Yesu. Mitume walikuwa wanafundisha pia kwamba watu watafufuka kutoka kwa wafu. 3 Waliwakamata Petro na Yohana. Kwa kuwa ilikuwa jioni tayari, waliwaweka gerezani usiku ule mpaka siku iliyofuata. 4 Lakini watu wengi waliowasikia mitume waliamini walichosema. Na siku hiyo idadi ya watu katika kundi la waamini ikafikia watu 5,000.
5 Siku iliyofuata, watawala wa Kiyahudi, wazee na walimu wa sheria walikutana Yerusalemu. 6 Kuhani mkuu Anasi alikuwepo. Kayafa, Yohana, Iskanda na jamaa wengine wa kuhani mkuu walikuwepo pia. 7 Waliwasimamisha Petro na Yohana mbele ya watu wote. Wakawauliza maswali mengi, “Mliwezaje kumponya mlemavu wa miguu huyu? Mlitumia nguvu gani? Mmefanya hili kwa mamlaka ya nani?”
8 Ndipo Petro, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akawaambia, “Enyi watawala nanyi wazee wa watu, 9 mnatuuliza leo ni nini tulifanya kumsaidia huyu mlemavu wa miguu? Mnatuuliza nini kilimponya? 10 Tunataka ninyi nyote na watu wote wa Israeli mtambue kuwa mtu huyu aliponywa na nguvu ya Yesu Kristo kutoka Nazareti. Mlimpigilia Yesu msalabani, lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu. Mtu huyu alikuwa mlemavu wa miguu, lakini sasa ni mzima. Anaweza kusimama hapa mbele zenu kwa sababu ya nguvu ya Yesu! 11 Yesu ndiye
12 Yesu peke yake ndiye anayeweza kuokoa watu. Jina lake ndiyo nguvu pekee iliyotolewa kumwokoa mtu yeyote ulimwenguni. Ni lazima tuokoke kupitia yeye!”
13 Viongozi wa Kiyahudi walijua kuwa Petro na Yohana walikuwa watu wa kawaida wasio na elimu yo yote. Lakini walikuwa wanazungumza kwa ujasiri bila woga; viongozi walishangaa. Walitambua pia kuwa Petro na Yohana walikuwa pamoja na Yesu. 14 Walimwona aliyeponywa akiwa amesimama kwa miguu yake mwenyewe pembeni mwa mitume. Na hivyo walishindwa kuzungumza chochote kilicho kinyume na mitume.
15 Viongozi wa Kiyahudi wakawaambia mitume watoke nje ya chumba cha mkutano wa baraza. Kisha viongozi wakajadiliana wao wenyewe juu ya nini wanachopaswa kufanya. 16 Wakaulizana, “Tuwafanye nini watu hawa? Kila mtu katika Yerusalemu anajua kuhusu muujiza walioufanya kama ishara kutoka kwa Mungu. Ni dhahiri, hatuwezi kusema muujiza huo haukufanyika. 17 Lakini ni lazima tuwatishe ili wasiendelee kuwaambia watu kutumia jina lile.[b] Ili tatizo hili lisisambae miongoni mwa watu.”
18 Hivyo viongozi wa Kiyahudi wakawaita Petro na Yohana ndani tena. Wakawaambia wasiseme wala kufundisha kitu chochote kwa kutumia jina la Yesu. 19 Lakini Petro na Yohana wakawajibu, “Mnadhani kipi ni sahihi? Mungu angetaka nini? Je, tunapaswa kuwatii ninyi au tumtii Mungu? 20 Hatuwezi kukaa kimya. Ni lazima tuwaambie watu kuhusu yale tuliyoona na kusikia.”
21-22 Viongozi wa Kiyahudi hawakupata sababu za kuwaadhibu mitume, kwa sababu watu wote walikuwa wanamsifu Mungu kwa kile kilichotendeka. Muujiza huu ulikuwa ishara kutoka kwa Mungu. Mtu aliyeponywa alikuwa na miaka zaidi ya arobaini. Hivyo viongozi wa Kiyahudi wakawaonya mitume tena na kuwaacha waende wakiwa huru.
Petro na Yohana Warudi kwa Waamini
23 Petro na Yohana waliondoka kwenye mkutano wa viongozi wa Kiyahudi na kurudi kwa waamini wenzao. Wakalieleza kundi la waamini kila kitu walichoambiwa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu. 24 Waamini waliposikia hili, wote kwa pamoja wakamwomba Mungu wakiwa na nia moja. Wakasema, “Bwana wa wote, wewe ndiye uliyeumba mbingu, dunia, bahari na kila kitu ulimwenguni. 25 Baba yetu Daudi alikuwa mtumishi wako. Kwa msaada wa Roho Mtakatifu aliandika maneno haya:
‘Kwa nini mataifa yanatenda kwa kiburi?
Kwa nini watu wanapanga mipango isiyofaa kama hii?
26 Wafalme wa dunia hujiandaa kwa mapigano,
na watawala hukusanyika pamoja kinyume na Bwana
na kinyume na Masihi wake.’(B)
27 Ndicho hasa kilichotokea wakati Herode, Pontio Pilato, mataifa mengine na watu wa Israeli walipokusanyika pamoja hapa Yerusalemu wakawa kinyume na Yesu; Masihi, Mtumishi wako mtakatifu. 28 Watu hawa waliokusanyika pamoja kinyume na Yesu waliwezesha mpango wako kukamilika. Ilifanyika kwa sababu ya nguvu zako na matakwa yako. 29 Na sasa, Bwana, sikiliza wanayosema. Wanajaribu kututisha. Sisi ni watumishi wako. Tusaidie ili tuseme yale unayotaka tuseme bila kuogopa. 30 Tusaidie, ili tuwe jasiri kwa kutuonesha nguvu zako. Ponya Wagonjwa. Fanya ishara na maajabu kutokea kwa mamlaka[c] ya Yesu mtumishi wako mtakatifu.”
31 Baada ya waamini kuomba, mahali walipokuwa palitikisika. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, na wakaendelea kuhubiri Habari Njema bila woga.
Ushirika wa Waamini
32 Kundi lote la waamini waliungana katika kuwaza na katika mahitaji yao. Hakuna aliyesema vitu alivyokuwa navyo ni vyake peke yake. Badala yake walishirikiana kila kitu. 33 Kwa nguvu kuu mitume walifanya ijulikane kwa kila mmoja kwamba Bwana Yesu alifufuliwa kutoka kwa wafu. Na Mungu aliwabariki sana waamini wote. 34 Hakuna aliyepungukiwa kitu. Kila aliyemiliki shamba au nyumba aliuza na kuleta pesa alizopata, 35 na kuzikabidhi kwa mitume. Kisha kila mtu akapewa kiasi alichohitaji.
36 Mmoja wa waamini aliitwa Yusufu. Mitume walimwita Barnaba, jina linalomaanisha “Mtu anayewatia moyo wengine.” Alikuwa Mlawi mzaliwa wa Kipro. 37 Yusufu aliuza shamba alilomiliki. Akaleta pesa na kuwapa mitume.
Acts 4
English Standard Version
Peter and John Before the Council
4 And as they were speaking to the people, the priests and (A)the captain of the temple and (B)the Sadducees came upon them, 2 greatly annoyed because they were teaching the people and proclaiming (C)in Jesus the resurrection from the dead. 3 And they arrested them and (D)put them in custody until the next day, for it was already evening. 4 But many of those who had heard the word believed, and (E)the number of the men came to about five thousand.
5 On the next day their rulers and elders and scribes gathered together in Jerusalem, 6 with (F)Annas the high priest and (G)Caiaphas and John and Alexander, and all who were of the high-priestly family. 7 And when they had set them in the midst, they inquired, (H)“By what power or (I)by what name did you do this?” 8 Then Peter, (J)filled with the Holy Spirit, said to them, “Rulers of the people and elders, 9 if we are being examined today (K)concerning a good deed done to a crippled man, by what means this man has been healed, 10 let it be known to all of you and to all the people of Israel that (L)by the name of Jesus Christ of Nazareth, whom you crucified, (M)whom God raised from the dead—by him this man is standing before you well. 11 (N)This Jesus[a] is the stone that was (O)rejected by you, the builders, which has become the cornerstone.[b] 12 And there is (P)salvation (Q)in no one else, for (R)there is no other (S)name under heaven given among men[c] by which we must be saved.”
13 (T)Now when they saw the boldness of Peter and John, and perceived that they were uneducated, common men, they were astonished. And they recognized that they had been with Jesus. 14 But seeing the man who was healed (U)standing beside them, (V)they had nothing to say in opposition. 15 But when they had commanded them to leave the council, they conferred with one another, 16 saying, (W)“What shall we do with these men? For that (X)a notable sign has been performed through them is evident to all the inhabitants of Jerusalem, and we cannot deny it. 17 But in order that it may spread no further among the people, let us warn them (Y)to speak no more to anyone in this name.” 18 So they called them and charged them not to speak or teach at all in the name of Jesus. 19 But Peter and John answered them, (Z)“Whether it is right in the sight of God to listen to you rather than to God, you must judge, 20 for (AA)we cannot but speak of what (AB)we have seen and heard.” 21 And when they had further threatened them, they let them go, finding no way to punish them, (AC)because of the people, for all were praising God (AD)for what had happened. 22 For the man on whom this sign of healing was performed was more than forty years old.
The Believers Pray for Boldness
23 When they were released, they went to their friends and reported what the chief priests and the elders had said to them. 24 And when they heard it, they lifted their voices (AE)together to God and said, “Sovereign Lord, (AF)who made the heaven and the earth and the sea and everything in them, 25 who through the mouth of our father David, your servant,[d] said by the Holy Spirit,
(AG)“‘Why did the Gentiles rage,
and the peoples plot in vain?
26 The kings of the earth set themselves,
and (AH)the rulers were gathered together,
against the Lord and against his (AI)Anointed’[e]—
27 for truly in this city there were gathered together against your (AJ)holy servant Jesus, (AK)whom you anointed, both (AL)Herod and (AM)Pontius Pilate, along (AN)with the Gentiles and (AO)the peoples of Israel, 28 (AP)to do whatever your hand and (AQ)your plan had predestined to take place. 29 And now, Lord, (AR)look upon their threats and grant to your servants to continue to speak your word with all (AS)boldness, 30 while (AT)you stretch out your hand to heal, and signs and wonders are performed (AU)through the name of your (AV)holy servant Jesus.” 31 And when they had prayed, (AW)the place in which they were gathered together was shaken, and (AX)they were all filled with the Holy Spirit and (AY)continued to speak the word of God with boldness.
They Had Everything in Common
32 Now the full number of those who believed were of (AZ)one heart and (BA)soul, and no one said that any of the things that belonged to him was his own, but (BB)they had everything in common. 33 And with great (BC)power the apostles were giving their testimony to the resurrection of the Lord Jesus, and (BD)great grace was upon them all. 34 (BE)There was not a needy person among them, for (BF)as many as were owners of lands or houses sold them and brought the proceeds of what was sold 35 and (BG)laid it at the apostles' feet, and (BH)it was distributed to each as any had need. 36 Thus Joseph, who was also called by the apostles Barnabas (which means (BI)son of encouragement), a Levite, a native of Cyprus, 37 sold a field that belonged to him and brought the money and (BJ)laid it at the apostles' feet.
© 2017 Bible League International
The ESV® Bible (The Holy Bible, English Standard Version®), © 2001 by Crossway, a publishing ministry of Good News Publishers. ESV Text Edition: 2025.
