Marko 1
Neno: Bibilia Takatifu
Mahubiri Ya Yohana Mbatizaji
1 Huu ni mwanzo wa Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu. 2 Kama alivyoandika nabii Isaya, Mungu alisema: “Namtuma mjumbe wangu akutangulie, ambaye ataandaa njia yako.” 3 “Mtu aitaye kwa sauti kuu jangwani. ‘Mtengenezeeni Bwana njia; nyoosheni sehemu zote atakazopitia.’ ”
4 Yohana alitokea nyikani, akawabatiza watu huko na kuwahubi ria kwamba watubu, wabatizwe, ili wasamehewe dhambi zao. 5 Watu kutoka eneo lote la Yudea na sehemu zote za Yerusalemu walikwenda kumsikiliza. Wakatubu dhambi zao, akawabatiza katika mto wa Yor dani. 6 Yohana alivaa mavazi ya manyoya ya ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa ni nzige na asali ya mwituni. 7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo kunizidi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake. 8 Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawaba tiza kwa Roho Mtakatifu.”
Yesu Abatizwa
9 Baadaye Yesu akaja kutoka Nazareti katika sehemu ya Gali laya, akabatizwa na Yohana katika mto wa Yordani. 10 Yesu alipo toka kwenye maji aliona mbingu zikifunuka na Roho wa Mungu anam shukia kama njiwa. 11 Na sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni mwanangu mpendwa; nimependezwa nawe.”
Yesu Ajaribiwa Nyikani
12 Mara tu baada ya haya, Roho akamwongoza Yesu mpaka nyikani. 13 Akakaa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini aki jaribiwa na shetani. Alikaa na wanyama wa porini na malaika wal imhudumia.
Yesu Aanza Kuhubiri
14 Yohana mbatizaji alipokamatwa na kutiwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya akaanza kutangaza Habari Njema za Mungu, 15 akisema, “Wakati umefika: Ufalme wa Mungu umewasili. Tubuni, muamini Habari Njema.”
Yesu Awaita Wanafunzi Wanne
16 Yesu alipokuwa akitembea kando kando ya Ziwa la Galilaya alimwona Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa kutumia nyavu; ndugu hawa wawili walikuwa wavuvi. 17 Yesu akawaambia, “Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.” 18 Wakaacha nyavu zao mara moja wakamfuata Yesu.
19 Alipokwenda mbele kidogo, akawaona Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo. Wao walikuwa katika mashua wakitengeneza nyavu zao. 20 Mara tu alipowaona akawaita, nao wakamwacha baba yao na wavuvi wa kuajiriwa, wakamfuata Yesu.
Yesu Afukuza Pepo Mchafu
21 Wakaenda mpaka Kapernaumu. Ilipofika siku ya sabato, Yesu akaenda katika sinagogi akaanza kufundisha. 22 Watu waliom sikiliza, walishangazwa sana na mafundisho yake. Yeye hakufund isha kama walimu wao wa sheria. Alifundisha kama mtu mwenye mam laka.
23 Wakati huo huo, mtu mmoja aliyekuwa na pepo 24 akapiga kelele humo katika sinagogi akasema, “Mbona unatuingilia, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninafahamu wewe ni nani! Wewe ni Mtakatifu wa Mungu.” 25 Lakini Yesu akamkemea akamwambia, “Kaa kimya! Mtoke!” 26 Yule pepo mchafu akamtikisa yule mtu kwa nguvu kisha akamtoka akipiga kelele.
27 Watu wakashangaa, wakaanza kuulizana, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya? Huyu mtu anatoa amri kwa mamlaka na hata pepo wanamtii!”
28 Sifa zake zikaenea upesi kila mahali katika mkoa wote wa
Yesu Amponya Mama Mkwe Wa Simoni
29 Yesu na wanafunzi wake walipoondoka katika sinagogi, walikwenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea. Wanafunzi wengine waliokuwepo ni Yakobo na Yohana. 30 Mama mkwe wake Simoni alikuwa kitandani, ana homa. Na mara Yesu alipofika wakamweleza. 31 Yesu akaenda karibu na kitanda, akamshika yule mama mkono, akamwinua; homa ikamtoka, akawahudumia.
Yesu Aponya Wengi
32 Jioni ile, baada ya jua kutua, watu wakawaleta wagonjwa wote na wengine waliopagawa na pepo kwa Yesu. 33 Watu wote wa mji huo wakakusanyika mbele ya nyumba hiyo. 34 Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya kila aina. Akawatoa pepo wengi; lakini hakuwaruhusu pepo hao wazungumze, kwa sababu wal ifahamu yeye ni nani.
Yesu Aondoka Kapernaumu Na Kwenda Galilaya
35 Kesho yake alfajiri, kabla hapajapambazuka, Yesu akaamka akaenda mahali pa faragha, akaomba. 36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta. 37 Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu ana kutafuta!”
38 Yesu akawajibu, “Twendeni kwenye vijiji vingine vya jirani nikahubiri huko pia; kwa sababu hicho ndicho kilicho nileta.” 39 Kwa hiyo akazunguka Galilaya nzima akihubiri katika masinagogi na kuponya watu waliopagawa na pepo.
Yesu Amponya Mtu Mwenye Ukoma
40 Akaja mtu mwenye ukoma, akapiga magoti mbele ya Yesu akamsihi, “Ukitaka, unaweza kunitakasa.” 41 Yesu akamwonea huruma, akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka upone, takasika.” 42 Mara ukoma wote ukaisha akapona kabisa. 43 Yesu akamruhusu aende lakini 44 akamwonya, “Usimwambie mtu ye yote habari hizi; bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na utoe sadaka ya utakaso kama alivyoamuru Musa, iwe ushuhuda kwa watu.”
45 Lakini yule mtu alikwenda akatangaza habari za kuponywa kwake kila mahali. Kwa hiyo Yesu hakuweza tena kuingia katika vijiji na miji waziwazi isipokuwa alikaa sehemu zisizo na watu, nao wakamfuata huko kutoka pande zote.
Mark 1
New International Version
John the Baptist Prepares the Way(A)
1 The beginning of the good news about Jesus the Messiah,[a] the Son of God,[b](B) 2 as it is written in Isaiah the prophet:
“I will send my messenger ahead of you,
who will prepare your way”[c](C)—
3 “a voice of one calling in the wilderness,
‘Prepare the way for the Lord,
make straight paths for him.’”[d](D)
4 And so John the Baptist(E) appeared in the wilderness, preaching a baptism of repentance(F) for the forgiveness of sins.(G) 5 The whole Judean countryside and all the people of Jerusalem went out to him. Confessing their sins, they were baptized by him in the Jordan River. 6 John wore clothing made of camel’s hair, with a leather belt around his waist,(H) and he ate locusts(I) and wild honey. 7 And this was his message: “After me comes the one more powerful than I, the straps of whose sandals I am not worthy to stoop down and untie.(J) 8 I baptize you with[e] water, but he will baptize you with[f] the Holy Spirit.”(K)
The Baptism and Testing of Jesus(L)(M)
9 At that time Jesus came from Nazareth(N) in Galilee and was baptized by John(O) in the Jordan. 10 Just as Jesus was coming up out of the water, he saw heaven being torn open and the Spirit descending on him like a dove.(P) 11 And a voice came from heaven: “You are my Son,(Q) whom I love; with you I am well pleased.”(R)
12 At once the Spirit sent him out into the wilderness, 13 and he was in the wilderness forty days,(S) being tempted[g] by Satan.(T) He was with the wild animals, and angels attended him.
Jesus Announces the Good News(U)
14 After John(V) was put in prison, Jesus went into Galilee,(W) proclaiming the good news of God.(X) 15 “The time has come,”(Y) he said. “The kingdom of God has come near. Repent and believe(Z) the good news!”(AA)
Jesus Calls His First Disciples
16 As Jesus walked beside the Sea of Galilee, he saw Simon and his brother Andrew casting a net into the lake, for they were fishermen. 17 “Come, follow me,” Jesus said, “and I will send you out to fish for people.” 18 At once they left their nets and followed him.(AB)
19 When he had gone a little farther, he saw James son of Zebedee and his brother John in a boat, preparing their nets. 20 Without delay he called them, and they left their father Zebedee in the boat with the hired men and followed him.
Jesus Drives Out an Impure Spirit(AC)
21 They went to Capernaum, and when the Sabbath came, Jesus went into the synagogue and began to teach.(AD) 22 The people were amazed at his teaching, because he taught them as one who had authority, not as the teachers of the law.(AE) 23 Just then a man in their synagogue who was possessed by an impure spirit cried out, 24 “What do you want with us,(AF) Jesus of Nazareth?(AG) Have you come to destroy us? I know who you are—the Holy One of God!”(AH)
25 “Be quiet!” said Jesus sternly. “Come out of him!”(AI) 26 The impure spirit shook the man violently and came out of him with a shriek.(AJ)
27 The people were all so amazed(AK) that they asked each other, “What is this? A new teaching—and with authority! He even gives orders to impure spirits and they obey him.” 28 News about him spread quickly over the whole region(AL) of Galilee.
Jesus Heals Many(AM)(AN)
29 As soon as they left the synagogue,(AO) they went with James and John to the home of Simon and Andrew. 30 Simon’s mother-in-law was in bed with a fever, and they immediately told Jesus about her. 31 So he went to her, took her hand and helped her up.(AP) The fever left her and she began to wait on them.
32 That evening after sunset the people brought to Jesus all the sick and demon-possessed.(AQ) 33 The whole town gathered at the door, 34 and Jesus healed many who had various diseases.(AR) He also drove out many demons, but he would not let the demons speak because they knew who he was.(AS)
Jesus Prays in a Solitary Place(AT)
35 Very early in the morning, while it was still dark, Jesus got up, left the house and went off to a solitary place, where he prayed.(AU) 36 Simon and his companions went to look for him, 37 and when they found him, they exclaimed: “Everyone is looking for you!”
38 Jesus replied, “Let us go somewhere else—to the nearby villages—so I can preach there also. That is why I have come.”(AV) 39 So he traveled throughout Galilee, preaching in their synagogues(AW) and driving out demons.(AX)
Jesus Heals a Man With Leprosy(AY)
40 A man with leprosy[h] came to him and begged him on his knees,(AZ) “If you are willing, you can make me clean.”
41 Jesus was indignant.[i] He reached out his hand and touched the man. “I am willing,” he said. “Be clean!” 42 Immediately the leprosy left him and he was cleansed.
43 Jesus sent him away at once with a strong warning: 44 “See that you don’t tell this to anyone.(BA) But go, show yourself to the priest(BB) and offer the sacrifices that Moses commanded for your cleansing,(BC) as a testimony to them.” 45 Instead he went out and began to talk freely, spreading the news. As a result, Jesus could no longer enter a town openly but stayed outside in lonely places.(BD) Yet the people still came to him from everywhere.(BE)
Footnotes
- Mark 1:1 Or Jesus Christ. Messiah (Hebrew) and Christ (Greek) both mean Anointed One.
- Mark 1:1 Some manuscripts do not have the Son of God.
- Mark 1:2 Mal. 3:1
- Mark 1:3 Isaiah 40:3
- Mark 1:8 Or in
- Mark 1:8 Or in
- Mark 1:13 The Greek for tempted can also mean tested.
- Mark 1:40 The Greek word traditionally translated leprosy was used for various diseases affecting the skin.
- Mark 1:41 Many manuscripts Jesus was filled with compassion
Copyright © 1989 by Biblica
Holy Bible, New International Version®, NIV® Copyright ©1973, 1978, 1984, 2011 by Biblica, Inc.® Used by permission. All rights reserved worldwide.
NIV Reverse Interlinear Bible: English to Hebrew and English to Greek. Copyright © 2019 by Zondervan.