Revised Common Lectionary (Semicontinuous)
Watu Wengi Wataacha Kumpenda Mungu
3 Kumbuka hili: Katika siku za mwisho nyakati ngumu zitakuja. 2 Watu watajipenda wenyewe na kupenda fedha. Watakuwa na majivuno na wenye jeuri. Watawatukana wengine kwa matusi. Hawatawatii wazazi wao. Watakuwa wasio na shukrani. Watapinga kila kinachompendeza Mungu. 3 Hawatakuwa na upendo kwa wengine na hawatakubali kuwasamehe wengine. Watawasingizia wengine na hawataweza kujizuia. Watakuwa wakatili na watayachukia yaliyo mema. 4 Watu watawasaliti rafiki zao. Watafanya mambo ya kipuuzi bila kufikiri na watajisifu wenyewe. Badala ya kumpenda Mungu watapenda starehe. 5 Watajifanya kuwa wanamheshimu Mungu, lakini watazikana nguvu za uzima ambazo ndizo zinazotuwezesha kwa hakika kumpa utukufu na kumpendeza. Ukae mbali na watu wa jinsi hiyo.
6 Nasema hivi kwa sababu baadhi yao wanaziendea nyumba na kuwateka wanawake dhaifu, waliolemewa na dhambi na kuvutwa na kila aina ya tamaa. 7 Wanawake hawa nyakati zote wanataka kujifunza, lakini hawawezi kamwe kuufikia ufahamu wote wa kweli. 8 Kama ambavyo Yane na Yambre[a] walivyompinga Musa, ndivyo hata watu hawa wanavyoipinga kweli. Ni watu ambao akili zao zimeharibika, nao wameshindwa kuifuata imani. 9 Lakini hawataendelea mbele zaidi, kwa sababu upumbavu wao utadhihirika wazi wazi kwa watu wote, kama ujinga wa Yane na Yambre ulivyojulikana.
© 2017 Bible League International