Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Revised Common Lectionary (Semicontinuous)

Daily Bible readings that follow the church liturgical year, with sequential stories told across multiple weeks.
Duration: 1245 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Error: Book name not found: Lam for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Lam for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
2 Timotheo 1:1-14

Salamu kutoka kwa Paulo, mtume wa Kristo Yesu.[a] Ni mtume kwa sababu ndivyo Mungu alivyotaka. Yeye alinituma kwa sababu Mungu alipenda niwaeleze watu juu ya ahadi ya uzima ulio katika Kristo Yesu.

Kwa Timotheo, mwanangu mpendwa:

Neema, rehema na amani iwe kwako kutoka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu.

Shukrani na Kutia Moyo

Daima namshukuru Mungu katika maombi yangu ninapokukumbuka usiku na mchana kwa ajili yako. Ni Mungu wa mababu zangu na daima nimemtumikia kwa dhamiri safi. Nikiyakumbuka machozi yako kwa ajili yangu, ninatamani kukuona, ili niweze kujazwa na furaha. Nimekumbuka imani yako ya kweli ambayo mwanzoni ilikuwa kwa bibi yako Loisi na kwa mama yako Eunike. Nami nashawishika hiyo iko kwako. Kwa sababu hii ninakukumbusha karama ya Mungu ambayo uliipokea wakati nilipokuwekea mikono. Sasa nataka uitumie karama hiyo na ikue zaidi na zaidi kama mwali wa moto mdogo uwakavyo ndani ya moto. Kwani Roho ambaye Mungu alitupa sisi ni chanzo cha ujasiri wetu, ni nguvu, upendo na fikra safi.

Hivyo usione aibu kushuhudia juu ya Bwana wetu Yesu au kunionea aibu mimi, niliye mfungwa kwa ajili yake. Bali aliteseka pamoja nami kwa ajili ya Habari Njema na Mungu hutupa nguvu.

Alituokoa na kutuita katika maisha ya utakatifu, sio kwa sababu ya kitu cho chote tulichokifanya wenyewe, bali kwa kusudi lake mwenyewe na neema, ambayo ametupa sisi kwa Kristo Yesu kabla ya mwanzo wa wakati, 10 na ambayo sasa imeonyeshwa kwetu kwa kuja kwake Kristo Yesu, Mwokozi wetu. Yeye Kristo aliiharibu mauti na kuleta uzima na kutokufa kwenye nuru kwa njia ya Habari Njema.

11 Niliteuliwa na Mungu kutangaza Habari Njema kama mtume na mwalimu. 12 Na ni kwa kazi hii ninateseka lakini sioni haya kwa sababu namjua yeye niliyemwekea imani yangu, na nina uhakika kuwa anaweza kukilinda kile nilichokikabidhi kwake hadi Siku ile.

13 Yale uliyoyasikia nikiyafundisha yawe mfano kwako wa mafundisho utakayofundisha wewe. Uyafuate na yawe kielelezo cha mafundisho ya kweli na uzima kwa uaminifu na upendo ule ule ambao Kristo Yesu ametuonesha. 14 Kwa msaada wa Roho Mtakatifu anayeishi ndani yako, uyalinde mafundisho haya ya mazuri na yenye thamani mliyopewa dhamana kwayo.

Luka 17:5-10

Imani Yako Ni Kubwa Kiasi Gani?

Kisha mitume wakamwambia Bwana, “Tuongezee imani.”

Bwana akasema, “Imani yenu ingekuwa kubwa kama mbegu ya haradali, mngeuambia mforosadi huu, ‘Ng'oka, ukajipandikize baharini,’ nao ungewatii.

Iweni Watumishi Wema

Chukulia mmoja wenu ana mtumishi ambaye amekuwa shambani akilima au akichunga kondoo shambani. Akirudi kutoka shambani au machungani, utamwambia nini? Je, utamwambia, ‘Njoo ndani, keti, ule chakula’? Hapana! Utamwambia mtumishi wako, ‘Nitayarishie chakula nile. Jitayarishe na unihudumie. Nitakapomaliza kula na kunywa, ndipo utakula.’ Mtumishi asipewe shukrani maalumu kwa kufanya kazi yake. Anafanya kile alichoagizwa na mkuu wake. 10 Vivyo hivyo nanyi. Mkimaliza kufanya yote mliyoamriwa kufanya, mseme, ‘Sisi ni watumwa, hatustahili shukrani yoyote maalumu. Tumefanya kazi tunayotakiwa kufanya.’”

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International