Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Revised Common Lectionary (Semicontinuous)

Daily Bible readings that follow the church liturgical year, with sequential stories told across multiple weeks.
Duration: 1245 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Error: Book name not found: Isa for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Waebrania 1:1-4

Mungu Amesema Kupitia Mwanaye

Zamani Mungu alisema na baba zetu kwa kuwatumia manabii. Alisema nao mara nyingi na kwa njia nyingi tofauti. Lakini sasa katika siku hizi za mwisho Mungu amesema nasi tena kupitia Mwana wake. Mungu aliuumba ulimwengu wote kupitia Mwana wake. Na alimchagua Mwana kumiliki mambo yote. Huyo Mwana huuonesha utukufu wa Mungu. Yeye ni nakala halisi ya asili yake Mungu, na huviunganisha vitu vyote pamoja kwa amri yake yenye nguvu. Mwana aliwasafisha watu kutoka katika dhambi zao. Kisha akaketi upande wa kuume[a] wa Mungu, aliye Mkuu huko Mbinguni. Mwana akawa mkuu zaidi kuliko malaika, na Mungu akampa jina lililo kuu zaidi kuliko lolote katika majina yao.

Waebrania 1:5-12

Mungu kamwe hajamwambia malaika yeyote maneno haya:

“Wewe ni Mwanangu.
    Mimi leo hii nimekuwa Baba yako.”(A)

Mungu pia kamwe hajasema juu ya malaika,

“Nitakuwa Baba yake,
    naye atakuwa mwanangu.”(B)

Na kisha, pale Mungu anapomtambulisha Mwanaye mzaliwa wa kwanza ulimwenguni,[a] anasema,

“Basi malaika wote wa Mungu wamwabudu yeye.”[b]

Hivi ndivyo Mungu alivyosema kuhusu malaika:

“Yeye huwabadilisha malaika zake kuwa upepo[c]
    na watumishi wake kuwa miali ya moto.”(C)

Lakini hivi ndivyo alivyosema kuhusu Mwana wake:

“Mungu, ufalme wako utadumu milele na milele.
    Unatumia mamlaka yako kwa haki.
Unapenda kilicho sahihi na kuchukia kilicho na makosa.
    Hivyo Mungu, Mungu wako, amekuchagua wewe,
    na amekupa heshima na furaha zaidi kupita yeyote aliye kama wewe.”(D)

10 Pia Mungu alisema,

“Ee Bwana, mwanzo uliiumba dunia,
    na mikono yako ikaliumba anga.
11 Vitu hivi vitatoweka, lakini wewe utaendelea kuwepo.
    Vyote vitachakaa kama mavazi makuu kuu.
12 Utavikunja hivyo kama koti,
    navyo vitabadilishwa kama mavazi.
Lakini wewe hubadiliki,
    na uhai wako hautafikia mwisho.”(E)

Yohana 1:1-14

Yesu ni Neno la Mungu la Milele

Mwanzoni Kabla ulimwengu haujaumbwa
    alikuwepo Neno.[a]
Huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu,
    na Neno alikuwa Mungu.
Alikuwepo pamoja na Mungu
    toka mwanzo.
Kila kitu kilifanyika kupitia kwake.
    Hakuna chochote katika uumbaji wa Mungu
    kilichofanyika bila yeye.
Ndani yake Neno kulikuwemo na uzima,
    na uzima huo ulikuwa nuru
    kwa ajili ya watu wa ulimwenguni.
Nuru[b] hiyo yamulika gizani,
    na giza halikuishinda.[c]

Alikuwepo mtu aliyeitwa Yohana, aliyetumwa na Mungu. Alikuja kuwaambia watu kuhusu nuru. Ili kupitia kwake watu wote waweze kusikia kuhusu yule aliye nuru na wamwamini. Yohana mwenyewe hakuwa nuru. Lakini alikuja kuwaambia watu kuhusu nuru.

Nuru ya kweli,
    anayeleta mwangaza kwa watu wote,
    alikuwa tayari kuonekana kwa ulimwengu.
10 Huyo Neno alikuwapo tayari ulimwenguni.
    Ulimwengu uliumbwa kupitia yeye,
    lakini ulimwengu haukumkubali.
11 Alikuja kwa ulimwengu ulio wake,
    na watu wake mwenyewe hawakumkubali.
12 Lakini baadhi ya watu walimkubali wakamwamini
    na akawapa haki ya kuwa watoto wa Mungu.
13 Ndiyo, walikuwa watoto wa Mungu,
    lakini si kwa kuzaliwa kimwili.
Haikuhusisha matamanio
    ya kibinadamu.
Mungu mwenyewe aliwafanya
    kuwa watoto wake.
14 Neno akafanyika kuwa mwanadamu
    na akaishi pamoja nasi.
Tuliouna ukuu wa uungu wake;
    utukufu alionao Mwana pekee wa Baba.

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International