Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Revised Common Lectionary (Semicontinuous)

Daily Bible readings that follow the church liturgical year, with sequential stories told across multiple weeks.
Duration: 1245 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Luka 1:46-55

Mariamu Amsifu Mungu

46 Mariamu akasema,

“Moyo wangu unamwadhimisha Bwana,
47     kwa maana, Yeye, Mungu na Mwokozi
    wangu amenipa furaha kuu!
48 Kwa maana ameonesha kunijali,
    mimi mtumishi wake, nisiye kitu.
Na kuanzia sasa watu wote
    wataniita mbarikiwa.
49 Kwa kuwa Mwenye Nguvu amenitendea mambo makuu.
    Jina lake ni takatifu.
50 Na huwapa rehema zake wale wamchao,
    kutoka kizazi hadi kizazi.
51 Ameonesha nguvu ya mkono wake;
    Amewatawanya wanaojikweza.
52 Amewaangusha watawala kutoka katika viti vyao vya enzi,
    na kuwakweza wanyenyekevu.
53 Amewashibisha wenye njaa kwa mambo mema,
    na amewatawanya matajiri bila ya kuwapa kitu.
54 Amemsaidia Israeli, watu aliowachagua ili wamtumikie.
    Amekumbuka kuonesha rehema;
55 Maana ndivyo alivyowaahidi baba zetu,
    Ibrahimu na wazaliwa wake.”

Error: Book name not found: Mic for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Waebrania 10:5-10

Hivyo baada ya Kristo kuja ulimwenguni alisema:

“Huhitaji sadaka na sadaka,
    lakini umeandaa mwili kwa ajili yangu.
Hukuridhishwa na sadaka za kuteketezwa
    na sadaka kuondoa dhambi.
Kisha nikasema, ‘Nipo hapa, Mungu.
    Imeandikwa juu yangu katika kitabu cha sheria.
    Nimekuja kufanya yale unayopenda.’”(A)

Kwanza Kristo alisema, “Wewe hufurahishwi na sadaka na sadaka. Hukuridhishwa na sadaka za kuteketezwa na sadaka ili kuondoa dhambi.” (Hizi ndizo sadaka zote ambavyo sheria inaagiza.) Kisha akasema, “Niko hapa, Mungu. Nimekuja kufanya yale unayopenda.” Hivyo Mungu akafikisha mwisho wa mfumo wa zamani wa utoaji sadaka na akaanzisha njia mpya. 10 Yesu Kristo alifanya mambo ambayo Mungu alimtaka ayafanye. Na kwa sababu ya hilo, tunatakaswa kwa njia ya sadaka ya mwili wa Kristo. Kristo aliitoa sadaka hiyo mara moja, inayotosha kwa nyakati zote.

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International