Revised Common Lectionary (Semicontinuous)
Bakuli Zilizojazwa Ghadhabu ya Mungu
16 Kisha nikasikia sauti kuu kutoka hekaluni. Ikiwaambia malaika saba, “Nendeni mkazimimine bakuli saba zenye ghadhabu ya Mungu juu ya dunia.”
2 Malaika wa kwanza akaondoka. Akaimimina bakuli yake duniani. Ndipo wale wote waliokuwa na alama ya mnyama na walioiabudu sanamu yake wakapata majipu mabaya yenye maumivu makali.
3 Malaika wa pili akaimimina bakuli yake baharini. Bahari ikawa kama damu ya mtu aliyekufa. Kila kitu kinachoishi baharini kikafa.
4 Malaika wa tatu akaimimina bakuli yake juu ya mito na chemichemi za maji. Mito na chemichemi za maji zikawa damu. 5 Ndipo nikasikia malaika wa maji akimwambia Mungu:
“Wewe ni yule uliyepo na uliyekuwepo daima.
Wewe ni Mtakatifu.
Uko sahihi kwa hukumu hizi ulizofanya.
6 Watu walimwaga damu za
watakatifu na manabii wako.
Sasa umewapa watu hao damu ili wanywe.
Hiki ndicho wanachostahili.”
7 Pia nikasikia madhabahu ikisema:
“Ndiyo, Bwana Mungu Mwenye Nguvu,
hukumu zako ni za kweli na za haki.”
© 2017 Bible League International