Revised Common Lectionary (Semicontinuous)
Babeli Inaangamizwa
18 Kisha nikaona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni. Malaika huyu alikuwa na nguvu kuu. Utukufu wa malaika ukaing'arisha dunia. 2 Malaika akapaza sauti akasema:
“Ameteketezwa!
Mji mkuu Babeli umeteketezwa!
Umekuwa nyumba ya mapepo.
Mji ule umekuwa najisi.
Mji uliojaa kila aina ya ndege najisi.
Ni mahali ambapo kila mnyama najisi
na anayechukiwa anaishi.
3 Watu wote wa dunia wamekunywa mvinyo
wa uzinzi wake na ghadhabu ya Mungu.
Watawala wa dunia walizini pamoja naye,
na wafanya biashara wa ulimwengu walitajirika
kutokana na utajiri wa anasa zake.”
4 Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema:
“Enyi watu wangu, tokeni katika mji huo,
ili msishiriki katika dhambi zake.
Ili msiteseke kwa adhabu yoyote kuu atakayoipata.
5 Dhambi za mji huo zimerundikana na kufika mbinguni.
Mungu hajasahau makosa aliyotenda.
6 Upeni mji huo sawasawa na ulivyowapa wengine.
Mlipeni mara mbili kadiri ya alivyotenda.
Mwandalieni mvinyo ulio na nguvu mara mbili
ya mvinyo aliowaandalia wengine.
7 Alijipa utukufu mwingi na kuishi kitajiri.
Mpeni mateso mengi na huzuni nyingi.
Kama vile utukufu na starehe aliyoifurahia.
Hujisemea mwenyewe, ‘Mimi ni malkia nikaaye kwenye kiti changu cha enzi.
Mimi si mjane;
Sitakuwa na huzuni.’
8 Hivyo katika siku moja atateseka
kwa njaa kuu, maombolezo na kifo.
Atateketezwa kwa moto,
kwa sababu Bwana Mungu anayemhukumu ni mwenye nguvu.”
9 Watawala wa dunia waliozini pamoja naye na kushiriki utajiri wake watakapoona moshi wa kuungua kwake, watalia na kuhuzunika kwa sababu ya kifo chake. 10 Wataogopa mateso yake na kukaa mbali sana. Watasema:
“Inatisha! Inatisha sana, Ee mji mkuu,
ee Babeli, mji wenye nguvu!
Adhabu yako imekuja katika saa moja!”
19 Walirusha mavumbi juu ya vichwa vyao na kulia kwa sauti kuu kuonesha huzuni kuu waliyokuwa nayo. Walisema:
“Inatisha! Inatisha sana kwa mji mkuu!
Wote waliokuwa na meli baharini walitajirika kwa sababu ya utajiri wake!
Lakini umeteketezwa katika saa moja!
20 Ufurahi kwa sababu ya hili, Ee mbingu!
Furahini, watakatifu wa Mungu, mitume na manabii!
Mungu amemhukumu kwa sababu ya kile alichowatendea ninyi.”
© 2017 Bible League International