Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Revised Common Lectionary (Semicontinuous)

Daily Bible readings that follow the church liturgical year, with sequential stories told across multiple weeks.
Duration: 1245 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Exod for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Wafilipi 1:3-14

Maombi ya Paulo

Ninamshukuru Mungu kila wakati ninapowakumbuka. Kila wakati ninapowaombea ninyi nyote, daima ninawaombea kwa furaha. Ninamshukuru Mungu kwa namna mlivyonisaidia nilipokuwa ninawahubiri watu Habari Njema. Mlinisaidia tangu siku ya kwanza mlipoamini mpaka sasa. Nina uhakika kwamba Mungu, aliyeianzisha kazi njema ndani yenu, ataiendeleza mpaka itakapomalizika siku ile ambayo Kristo Yesu atakuja tena.

Ninajua niko sahihi kwa namna ile ninayowawazia ninyi nyote kwa sababu mko karibu sana na moyo wangu. Mmechangia sehemu muhimu sana katika neema ya Mungu kwa ajili yangu wakati huu nikiwa gerezani, na wakati wowote ninapoutetea na kuuthibitisha ukweli wa Habari njema. Mungu anajua kwamba ninataka sana kuwaona. Ninawapenda nyote kwa upendo wa Kristo Yesu.

Hili ndiyo ombi langu kwa ajili yenu:

Ya kwamba mkue zaidi na zaidi katika hekima na ufahamu kamili pamoja na upendo; 10 ya kwamba mjue tofauti kati ya kitu kilicho muhimu na kisicho muhimu ili muwe safi msio na lawama, mkiwa tayari kwa siku atakayokuja Kristo; 11 Maisha yenu yajaye matendo mengi mema yanayozalishwa na Kristo Yesu ili kumletea Mungu utukufu na sifa.

Matatizo Ya Paulo Yesaidia Kazi ya Bwana

12 Ndugu zangu, ninataka mjue kwamba yote yaliyonipata yamesaidia katika kusambaza Habari Njema, ingawa ninyi mnaweza kuwa mlitarajia kinyume chake. 13 Walinzi wote wa Kirumi na wengine wote hapa wanafahamu kuwa nimefungwa kwa sababu ninamtumikia Kristo. 14 Kufungwa kwangu gerezani kumesababisha waamini walio wengi hapa kuweka tumaini lao kwa Bwana, na kuhubiri ujumbe wa Mungu kwa ujasiri mwingi pasipo woga.

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International