Revised Common Lectionary (Semicontinuous)
15 Na mtu atawezaje kwenda na kuwaambia habari hizo ikiwa hajatumwa? Haya, hii ndiyo sababu Maandiko yanasema, “Ni jambo la kufurahisha kumwona mtu anayepeleka Habari Njema!”(A)
16 Lakini si watu wote walizipokea Habari Njema hizo. Na hii ndiyo sababu Isaya alisema, “Bwana, nani aliyeamini yale tuliyowaeleza?”(B) 17 Kwa hiyo imani hupatikana kutokana na kusikia Habari Njema. Na watu husikia Habari Njema wakati mtu anapowaeleza kuhusu Kristo.
18 Lakini nauliza, “Je, watu hao walizisikia Habari Njema?” Ndio Kwa kweli walizisikia kama Maandiko yanavyosema,
“Sauti zao zilitoka na kuenea duniani kote.
Maneno yao yakaenda kila mahali ulimwenguni.”(C)
19 Lakini tena nauliza, “Je, watu wa Israeli hawakuelewa?” Ndiyo, walielewa. Musa alikuwa wa kwanza kujibu swali hili. Na anasema haya kwa ajili ya Mungu:
“Nitawatumia wale ambao siyo Taifa halisi ili liwafanye muone wivu.
Nitalitumia taifa ambalo halielewi ili mkasirike.”(D)
20 Kisha Isaya ana ujasiri wa kutosha kusema haya kwa ajili ya Mungu:
“Watu walionipata mimi hawakuwa wakinitafuta.
Nilijitambulisha kwa watu ambao hawakuwa wakinitafuta.”(E)
21 Lakini kuhusu watu wa Israeli Mungu anasema,
“Kutwa nzima nilisimama nikiwa tayari kuwakubali watu hawa,
lakini ni wakaidi na wamekataa kunitii.”(F)
© 2017 Bible League International