Revised Common Lectionary (Semicontinuous)
Maisha Yanayompendeza Mungu
4 Kaka na dada zangu sasa nina mambo mengine ya kuwaambia. Tuliwafundisha namna ya kuishi maisha yanayompendeza Mungu. Nanyi mnaishi hivyo. Na sasa tunawaomba na kuwatia moyo katika Bwana Yesu kuishi zaidi na zaidi katika njia hiyo. 2 Mnafahamu yote tuliyowaamuru kufanya kwa mamlaka ya Bwana Yesu Kristo. 3 Mungu anawataka muwe watakatifu. Anawataka mkae mbali na dhambi za zinaa. 4 Mungu anawataka kila mmoja wenu ajifunze kuuthibiti mwili wake mwenyewe. Tumieni miili yenu kwa namna iliyo takatifu na yenye heshima.[a] 5 Msiruhusu tamaa za mwili kuwatawala kama watu wasiomjua Mungu. 6 Msimtendee vibaya ndugu aliye mwamini wala kuwadanganya katika hili. Bwana atawahukumu watendao hivyo. Tumekwisha kuwaambia juu ya hili na kuwaonya. 7 Mungu alituita kuwa watakatifu na safi. 8 Hivyo kila anayekataa kuyatii mafundisho haya anakataa kumtii Mungu, siyo wanadamu. Na Mungu ndiye anayewapa ninyi Roho Mtakatifu.
© 2017 Bible League International