Revised Common Lectionary (Semicontinuous)
Paulo Amalizia Barua Yake
13 Iweni waangalifu. Simameni imara katika imani yenu. Mwe jasiri na wenye nguvu. 14 Fanyeni kila kitu katika upendo.
15 Mnajua kuwa Stefana na familia yake walikuwa waamini wa kwanza katika Akaya. Wamejitia katika kazi ya kuwahudumia watu wa Mungu. Ndugu zangu, ninawaomba, 16 mjiweke chini ya uongozi wa watu kama hawa na wengine wanaofanya kazi kwa bidii na kutumika pamoja nao.
17 Ninafurahi kwa sababu Stefana, Fortunato na Akaiko wamekuja. Hamko hapa pamoja nami lakini wamejaza nafasi yenu. 18 Wamekuwa faraja kuu kwangu na kwenu pia. Basi, mnapaswa kuitambua thamani ya watu kama hawa.
19 Makanisa ya Asia yanawasalimu. Akila na Priska wanawasalimu katika Bwana. Na kanisa linalokutana nyumbani mwao linawasalimu pia. 20 Ndugu wote walioko hapa wanawasalimu. Salimianeni kila mmoja wenu kwa salamu maalum ya watu wa Mungu.[a]
21 Hii ni salamu yangu kwa mkono wangu mwenyewe: Paulo.
22 Ikiwa mtu yeyote hampendi Bwana, mwacheni mtu huyo abaki chini ya laana ya Mungu.
Njoo, Ewe Bwana![b]
23 Neema ya Bwana Yesu iwe pamoja nanyi.
24 Upendo wangu uwe nanyi nyote katika Kristo Yesu.
© 2017 Bible League International