Revised Common Lectionary (Complementary)
Barua ya Yesu kwa Kanisa la Sardi
3 Andika hivi kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi:
Huu ni ujumbe kutoka kwake Yeye mwenye roho saba na nyota saba.
Ninayajua matendo yako. Watu husema kuwa u hai, lakini hakika umekufa. 2 Amka! Jitie nguvu kabla ya nguvu kidogo uliyonayo haijakuishia kabisa. Unachofanya hakistahili kwa Mungu wangu. 3 Hivyo usisahau kile ulichopokea na kusikia. Ukitii. Geuza moyo na maisha yako! Amka, la sivyo nitakuja kwako na kukushtukiza kama mwizi. Hautajua wakati nitakapokuja.
4 Lakini una watu wachache katika kundi lako hapo Sardi waliojiweka safi. Watatembea pamoja nami. Watavaa nguo nyeupe, kwa kuwa wanastahili. 5 Kila atakayeshinda atavikwa nguo nyeupe kama wao. Sitayafuta majina yao katika kitabu cha uzima. Nitawakiri mbele za Baba yangu na malaika zake ya kuwa wao ni wangu. 6 Kila anayesikia hili azingatie kile ambacho Roho anayaambia makanisa.
© 2017 Bible League International