Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Old/New Testament

Each day includes a passage from both the Old Testament and New Testament.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: Lam for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Waebrania 10:19-39

Haja Ya Kuwa Imara

19 Kwa hiyo ndugu zangu, kwa kuwa tunao ujasiri wa kuingia Patakatifu pa Patakatifu kwa damu ya Yesu, 20 kwa njia mpya iliyo hai tuliyofunguliwa kupitia lile pazia, yaani kwa njia ya mwili wake, 21 na kwa kuwa tunaye kuhani mkuu anayemiliki nyumba ya Mungu; 22 basi tumkaribie Mungu kwa moyo wa kweli na imani timilifu, mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa na kuwa safi kutokana na dhamiri mbaya na miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi. 23 Tushikilie kwa makini tumaini tunalokiri kwa maana yeye ali yeahidi ni mwaminifu. 24 Na tujishughulishe kutafuta jinsi ya kuhimizana katika kuonyeshana upendo na kutenda mema. 25 Tusiache kukutana pamoja, kama wengine wanavyofanya, bali tutiane moyo, hasa zaidi tunapoona siku ile ikikaribia.

Hatari Ya Kukufuru

26 Kama tukiendelea kutenda dhambi makusudi baada ya kupokea na kufahamu ile kweli, hakuna tena dhabihu iliyobaki inayoweza kutolewa kwa ajili ya dhambi. 27 Kinachobakia ni kungojea kwa hofu hukumu ya Mungu na moto mkali utakaowaangamiza maadui zake. 28 Mtu aliyevunja sheria ya Mose aliuawa pasipo huruma kwa usha hidi wa watu wawili au watatu. 29 Je, mnadhani ni adhabu kali kiasi gani zaidi anastahili kupewa mtu ambaye anamdharau na kum kataa Mwana wa Mungu, na ambaye anaona kuwa damu ya agano iliyom takasa si kitu, na ambaye amemtukana Roho wa neema? 30 Kwa maana tunamjua yeye aliyesema, “Kulipiza kisasi ni juu yangu, mimi nitalipiza.” Pia alisema, “Bwana atawahukumu watu wake.” 31 Kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai ni jambo la kutisha.

32 Kumbuka siku zile za mwanzo baada ya kupokea mwanga, jinsi mlivyovumilia mapambano makali na mateso. 33 Wakati mwin gine mlitukanwa na kuteswa hadharani; wakati mwingine mlikuwa radhi kuungana na wale walioteswa hivyo. 34 Mliwaonea huruma waliokuwa kifungoni, na mkakubali kwa furaha kunyang’anywa mali zenu kwa maana mlifahamu kwamba mlikuwa na mali bora zaidi inay odumu.

35 Kwa hiyo msitupe tumaini lenu, ambalo litapewa tuzo kubwa. 36 Mnahitaji kuvumilia ili mkisha kufanya mapenzi ya Mungu mpate kile alichoahidi. 37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo tu yeye anayekuja atakuja , wala hatakawia; 38 lakini mtu wangu mwenye haki ataishi kwa imani, na akirudi nyuma sitapendezwa naye.”

39 Lakini sisi hatumo miongoni mwa hao wanaorudi nyuma wakaangamizwa, bali sisi ni miongoni mwa wanaoamini wakaokolewa.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica