Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Old/New Testament

Each day includes a passage from both the Old Testament and New Testament.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: Neh for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Matendo Ya Mitume 4:23-37

23 Mara Petro na Yohana walipoachiliwa, walirudi kwa waamini wenzao wakawaeleza waliyoambiwa na makuhani wakuu na wazee. 24 Waamini wote waliposikia maneno yao walimwomba Mungu kwa pamoja wakasema, “Wewe Bwana Mtukufu, uliyeumba mbingu na nchi na bahari na kila kiumbe kilichopo, 25 wewe ulitamka kwa njia ya Roho wako mtakatifu kupitia kwa baba yetu Daudi mtumishi wako, aliposema, ‘Mbona mataifa wanaghadhabika, na watu wanawaza mambo yasiyo na maana? 26 Wafalme wa dunia wamejiandaa na watawala wamekusanyika wampinge Bwana na Masihi wake.’ 27 Ndiyo sababu katika mji huu Herode na Pontio Pilato walikutana na Waisraeli wote na watu wa mataifa juu ya mtumishi wako mtakatifu Yesu, 28 wakaamua kumfanyia yale yote ambayo wewe ulikuwa umekusudia tangu awali na kupanga kwa uweza wako yatendeke.

29 “Sasa Bwana, sikia vitisho vyao na utuwezeshe sisi wat umishi wako kuhubiri neno lako kwa ujasiri mkuu; 30 na unyooshe mkono wako ili tuweze kuponya wagonjwa na kutenda ishara na miu jiza kwa jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu.” 31 Walipokwisha kusali, nyumba waliyokuwa wamekutania ikatikisika na wote wakaja zwa na Roho Mtakatifu, wakahubiri neno la Mungu kwa ujasiri. 32 Waamini wote walikuwa na nia moja na moyo mmoja, wala hakuna aliyeona mali aliyokuwa nayo kuwa yake, bali walishirikiana vitu vyote kwa pamoja. 33 Na kwa uwezo mkubwa mitume wakashuhudia kwa ujasiri habari za kufufuka kwa Bwana Yesu. Mungu akawapa wote neema kuu. 34 Wala hakuwepo mtu ye yote miongoni mwa waamini aliyepungukiwa na kitu kwa sababu wale waliokuwa na mashamba na nyumba waliuza vyote wakaleta fedha waliyopata 35 kwa wale mitume; kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.

36 Ndivyo ilivyokuwa kwamba Yusufu ambaye mitume walimwita Barnaba, maana yake Mwana wa Faraja, wa ukoo wa Lawi kutoka kisiwa cha Kipro 37 aliuza shamba alilokuwa nalo akaleta fedha alizopata kwa wale mitume.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica