Old/New Testament
28 Kwa hiyo Yesu akawaambia, “Mtakaponiinua juu, mimi Mwana wa Adamu, ndipo mtakapofahamu ya kuwa, ‘Mimi Ndiye
29 Baba yangu ambaye amenituma yupo pamoja nami, hajaniacha; kwa kuwa siku zote nafanya mapenzi yake.” 30 Wengi waliomsikia Yesu akisema maneno haya walimwamini.
Watu Huru Na Watumwa
31 Kwa hiyo Yesu akawaambia wale waliomwamini, “Kama mkiendelea kutii maneno yangu mtakuwa wanafunzi wangu halisi. 32 Mtaelewa yaliyo kweli kumhusu Mungu na ukweli huu utawafanya muwe watu huru. 33 Wao wakamjibu, “Una maana gani kusema tuta kuwa huru? Sisi ni wa uzao wa Ibrahimu. Hatujawahi kuwa watumwa wa mtu ye yote.” 34 Yesu akawaambia, “Ukweli ni kwamba, mtu ye yote anayetenda dhambi ni mtumwa wa dhambi. 35 Mtumwa hana haki ya kuishi siku zote katika nyumba anapotumika, lakini mwana ana haki zote katika nyumba ya baba yake. 36 Kwa hiyo, kama Mwana akiwafanya muwe huru, mtakuwa huru kweli. 37 Ninajua ya kuwa ninyi ni wa uzao wa Ibrahimu; lakini mnatafuta njia ya kuniua kwa sababu hamkubaliani na mafundisho yangu. 38 Ninasema yale niliy oyaona kwa Baba yangu na ninyi mnafanya yale mliyosikia kutoka kwa baba yenu.” 39 Wakasema, “Baba yetu ni Ibrahimu.” Yesu akawajibu, “Kama mngekuwa wa uzao wa Ibrahimu mngekuwa na tabia kama yake. 40 Lakini mnataka kuniua kwa sababu nimewaambia maneno ya kweli niliyosikia kutoka kwa Mungu. Ibrahimu hakufanya jambo la namna hii! 41 Ninyi mnafanya kama baba yenu afanyavyo. Wakamjibu, “Sisi si watoto wa haramu; tunaye Baba mmoja ambaye ni Mungu.” 42 Ndipo Yesu akawaambia, “Kama Mungu angekuwa ni Baba yenu, mngenipenda, kwa maana nilitoka kwa Mungu na sasa nipo hapa. Sikuja kwa mapenzi yangu mwenyewe ila kwa kuwa Mungu alini tuma. 43 Kwa nini hamwelewi ninayowaambia? Ni kwa sababu mnaka taa kusikiliza ujumbe wangu. 44 Ninyi ni watoto wa baba yenu shetani; kwa hiyo mnapenda kufanya maovu kama yeye. Tangu mwanzo yeye alikuwa muuaji na hana uhusiano wo wote na mambo ya kweli; kwa maana hana asili ya kusema lililo kweli. Shetani anapodanga nya anadhihirisha asili yake kwa kuwa yeye ni mwongo na ni baba wa uongo. 45 Lakini mimi nawaambia yaliyo kweli ndio sababu ham uamini maneno yangu! 46 Ni nani kati yenu anayeweza kuonyesha kuwa mimi nina dhambi? Kama nawaambia yaliyo kweli, mbona basi hamnisadiki? 47 Mtu wa Mungu hupokea maneno ya Mungu. Ninyi ham pokei maneno ya Mungu kwa sababu ninyi si wa Mungu.”
Yesu Amekuwepo Kabla Ya Ibrahimu
48 Wakamjibu, “Tulitamka sawa tuliposema kuwa wewe ni Msa maria na tena umepagawa na pepo.” 49 Yesu akawajibu, “Sina pepo. Mimi namheshimu Baba yangu bali ninyi mnanivunjia heshima yangu. 50 Hata hivyo mimi sitafuti utukufu wangu binafsi; yuko anayetaka niheshimiwe na ndiye atakayekuwa mwamuzi. 51 Ninawaam bia wazi kwamba, mtu ye yote anayetii mafundisho yangu hatakufa kamwe.” 52 Wakasema, “Sasa umetuhakikishia kabisa kwamba una wazimu! Ikiwa Ibrahimu alikufa na Manabii nao walikufa, utase maje, ‘mtu akitii mafundisho yangu hatakufa?’ 53 Je, wewe ni mkuu zaidi ya baba yetu Ibrahimu ambaye alikufa? Na Manabii ambao nao walikufa? Hivi unajifanya wewe kuwa nani?” 54 Yesu akawa jibu, “Kama nikijisifu mwenyewe sifa hiyo itakuwa haina maana. Anayenipa heshima ni Baba yangu, huyo ambaye ninyi mnamwita Mungu wenu. 55 Lakini ninyi hamumfahamu. Mimi namfahamu. Nikisema sim fahamu nitakuwa mwongo kama ninyi. Mimi namfahamu na ninatii maneno yake. 56 Baba yenu Ibrahimu alishangilia alipojua kuwa atashuhudia siku ya kuja kwangu. Aliiona siku hiyo na akafurahi sana.” 57 Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza hata miaka hamsini, itawezekanaje uwe umemwona Ibrahimu?” 58 Yesu akawa jibu, “Nawaambia wazi, kabla Ibrahimu hajazaliwa, ‘Mimi nipo.’ ” 59 Ndipo wakainua mawe wamwue; lakini Yesu akajificha wasim wone; akatoka Hekaluni.
Copyright © 1989 by Biblica