Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Old/New Testament

Each day includes a passage from both the Old Testament and New Testament.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: 2Sam for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Luka 17:1-19

17 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Majaribu yanayowafanya watu watende dhambi hayana budi kuwepo. Lakini ole wake mtu yule anayeyasababisha. Ingekuwa nafuu kama mtu huyo angefungiwa jiwe zito shingoni na kuzamishwa baharini kuliko kumfanya mmoja wa hawa wadogo atende dhambi. Kwa hiyo, jihadharini. Ndugu yako akikukosea mwonye; akiomba msamaha, msamehe. Hata kama akikuko sea mara saba kwa siku na kila mara aje kwako akisema, ‘Nisa mehe

Wanafunzi wakamwambia Bwana, “Tuzidishie imani.” Aka waambia, “Kama mngekuwa na imani kiasi cha punje ndogo sana ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu, ‘Ng’oka na mizizi yote ukaote baharini,’ nao ungewatii!”

Wajibu Wa Mtumishi

“Tuseme mmoja wenu ana mtumishi aliyekwenda shambani kulima au kuchunga kondoo. Je, mtumishi huyo akirudi utamwambia, ‘Karibu keti ule chakula’? Hata kidogo. Badala yake utamwambia, ‘Nitayarishie chakula na ujiandae kunihudumia ninapokula na kunywa, na baada ya hapo unaweza kula chakula chako.’ Wala hutamshukuru mtumishi huyo kwa kutimiza wajibu wake. 10 Hali kadhalika nanyi, baada ya kufanya mliyoagizwa, semeni, ‘Sisi ni watumishi tusiostahili, tumetimiza wajibu wetu tu.”’

Yesu Atakasa Wakoma Kumi

11 Yesu alipokuwa akienda Yerusalemu alipitia kati ya Samaria na Galilaya. 12 Alipokuwa akikaribia kijiji kimoja, watu kumi waliokuwa na ukoma walikutana naye. 13 Wakasimama mbali wakaita kwa nguvu, “Yesu! Bwana! tuonee huruma!” 14 Alipowaona akawaambia, “Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani.” Na walipokuwa wakienda, wakapona ukoma wao. 15 Mmoja wao alipoona kwamba ame pona, akarudi kwa Yesu akimsifu Mungu kwa sauti kuu. 16 Kwa heshima kubwa akajitupa miguuni kwa Yesu akamshukuru. Yeye ali kuwa ni Msamaria .

17 Yesu akauliza, “Hawakuponywa wote kumi? Wako wapi wale tisa wengine? 18 Hakuna hata mmoja aliyekumbuka kurudi kumsifu Mungu isipokuwa huyu mgeni?” 19 Akamwambia, “Inuka, uende; imani yako imekuponya.” Ufalme Wa Mungu Utakavyokuja

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica