Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Old/New Testament

Each day includes a passage from both the Old Testament and New Testament.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: Judg for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Luka 5:1-16

Siku moja Yesu alipokuwa amesimama akihubiri karibu na ziwa la Genesareti, watu wengi walimsonga ili wapate kusikia neno la Mungu. Akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa, lakini wenye mashua walikuwa wakiosha nyavu zao. Akaingia katika mashua moja, akamwomba mwenye mashua, ambaye jina lake lilikuwa Simoni, aisogeze zaidi katika maji. Kisha akakaa kwenye mashua, akaanza kuwafundisha.

Alipokwisha zungumza na watu akamwambia Simoni, “Sasa ipe leke mashua hadi mahali penye kina kirefu, kisha mshushe nyavu zenu nanyi mtapata samaki.”

Simoni akamjibu, “Bwana, tumekesha usiku kucha tukivua na hatukuambulia kitu cho chote. Lakini, kwa kuwa wewe umesema, tutazishusha nyavu.” Nao walipofanya kama Yesu alivyowaagiza, nyavu zao zikajaa samaki, zikaanza kuchanika! Wakawaashiria wavuvi wa ile mashua nyingine waje kuwasaidia. Mashua zote mbili zikajaa samaki hata karibu kuzama.

Simoni Petro alipoona yaliyotokea alipiga magoti mbele ya Yesu akamwambia, “Bwana,tafadhali uniache kwa maana mimi ni mwe nye dhambi.” Kwa kuwa yeye na wavuvi wenzake walikuwa wamesh angazwa sana na wingi wa samaki waliopata. 10 Hali kadhalika wavuvi wa ile mashua nyingine, Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo walishangazwa pia. Ndipo Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope; tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu.”

11 Nao walipokwisha fikisha mashua yao nchi kavu, wakaacha vyote, wakamfuata Yesu. Yesu Amponya Mwenye Ukoma

12 Siku moja Yesu alipokuwa katika mji fulani alitokea mtu mwenye ukoma mwili mzima. Alipomwona Yesu alijitupa chini kwa kunyenyekea akamsihi akisema, “Bwana, ukitaka unaweza kunita kasa!” 13 Yesu akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Ndio, nataka upone; takasika!” Wakati huo huo, ukoma wote ukamtoka . 14 Yesu akamwambia, “Usimweleze mtu ye yote jinsi ulivyopata kupona bali nenda moja kwa moja hadi kwa kuhani ili aone kuwa kweli umepona. Kisha utoe sadaka ya shukrani, kama she ria ya Musa inavyoagiza, ili kuthibitisha kuwa umetakasika.”

15 Lakini sifa za Yesu zikazidi sana kuenea. Watu wakamimi nika kwa wingi kutoka kila upande kuja kumsikiliza na kuponywa maradhi yao. 16 Ila mara kwa mara alitoka peke yake akaenda pasipo na watu akaomba.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica