Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Old/New Testament

Each day includes a passage from both the Old Testament and New Testament.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: Deut for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Marko 13:21-37

21 “Na wakati huo mtu akiwaambia, ‘Tazama, Kristo huyu hapa’ au , ‘Tazama, yule pale,’ msiamini. 22 Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo nao watafanya ishara na miujiza ili kuwadanganya hata wale waliochaguliwa na Mungu, kama ikiwezekana. 23 Kwa hiyo jihadharini kwa maana nimewaambia mambo haya kabla hayajatokea.”

Kuja Kwa Mwana Wa Adamu

24 “Siku hizo, baada ya hiyo dhiki, jua litatiwa giza na mwezi hautatoa mwanga wake. 25 Nyota zitaanguka kutoka mbinguni na nguvu za anga zitatikisika. 26 Ndipo watu wote wataniona mimi Mwana wa Adamu nikija katika mawingu kwa nguvu nyingi na utu kufu. 27 Nami nitawatuma malaika wawakusanye watu wangu kutoka pande zote nne za dunia, kutoka mwisho wa nchi hadi mwisho wa mbi ngu.

28 “Sasa jifunzeni jambo hili kutoka kwa mtini: mwonapo matawi ya mtini yakianza kulainika na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia. 29 Hali kadhalika mtaka poyaona mambo haya yanatokea, tambueni kwamba mimi Mwana wa Adamu, ni karibu kuja. 30 Ninawaambieni hakika, kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo haya kutokea. 31 Mbingu na nchi zita toweka, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”

Hakuna Ajuaye Siku Wala Saa

32 “Hakuna ajuaye siku hiyo itakuwa lini au saa ngapi; hata malaika mbinguni hawajui wala mimi Mwana sijui, isipokuwa Mungu Baba peke yake. 33 “Jiandaeni, muwe macho. Kwa maana hamjui wakati mambo haya yatakapotokea. 34 Ni kama mtu anayesafiri na kuwaachia wat umishi wake madaraka, kila mtu na wajibu wake; kisha akamwambia mlinzi wa mlango awe macho. 35 Kesheni basi, kwa sababu hamjui ni lini bwana mwenye nyumba atarudi. Anaweza akaja jioni, au usiku wa manane au alfajiri au mapambazuko. 36 Kama akija gha fla, pasipo ninyi kumtazamia, asije awakute mmelala. 37 Na haya ninayowaambia ninyi nawaambia watu wote: Kesheni!”

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica