Old/New Testament
Yesu Ni Bwana Wa Sabato
12 Wakati huo Yesu alipitia kwenye mashamba ya ngano siku ya sabato. Wanafunzi wake walikuwa na njaa, wakaanza kuvunja masuke ya ngano na kula. 2 Lakini Mafarisayo walipoona jambo hili wakam wambia, “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo lisilo halali kufanya siku ya sabato.”
3 Yesu akawajibu, “Hamjasoma walichofanya Daudi na wafuasi wake walipokuwa na njaa? 4 Waliingia katika nyumba ya Mungu wakala mkate uliowekwa wakfu, jambo ambalo halikuwa halali kwao kufanya isipokuwa makuhani peke yao. 5 Au hamjasoma katika sheria kwamba siku ya sabato makuhani huvunja sheria ya sabato Hekaluni lakini hawahesabiwi kuwa na hatia? 6 Nawaambieni wazi kwamba, aliye mkuu kuliko Hekalu yupo hapa. 7 Na kama mngalifahamu maana ya maneno haya, ‘Ninataka rehema wala si sadaka ya kuteketezwa;’ msingeliwalaumu watu wasio na hatia, 8 kwa maana Mwana wa Adamu ni Bwana wa sabato.”
Yesu Anamponya Mtu Aliyepooza Mkono
9 Yesu alipoondoka hapo, aliingia katika sinagogi lao. Huko alikuwepo mtu aliyepooza mkono . 10 Wakitafuta sababu ya kumsh taki, wakamwuliza, “Je, ni halali kuponya siku ya sabato?” 11 Yesu akawajibu, “Ni nani kati yenu ambaye kondoo wake aki tumbukia shimoni siku ya sabato hatamtoa? 12 Mtu ana thamani kubwa sana kuliko kondoo. Kwa hiyo ni halali kutenda mema siku ya sabato.”
13 Ndipo akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako.” Akau nyoosha, nao ukapona ukawa mzima kama ule mwingine. 14 Lakini Mafarisayo wakatoka nje wakashauriana jinsi ya kumwangamiza
Mtumishi Aliyechaguliwa Na Mungu
15 Lakini Yesu akiyafahamu mawazo yao, aliondoka mahali hapo. Na watu wengi walimfuata naye akawaponya wote. 16 Akawa kataza wasimtangaze. 17 Hii ilikuwa ili yatimie maneno aliyosema nabii Isaya: 18 “Mtazameni mtumishi wangu niliyemchagua, mpendwa wangu ambaye moyo wangu unapendezwa naye. Nitaweka Roho yangu juu yake , naye atatangaza haki kwa watu wa mataifa. 19 Hatabishana wala hatapiga kelele, sauti yake haitasikika mitaani. 20 Hataponda unyasi uliochubuliwa wala hatazima mshumaa unaokaribia kuzima, mpaka atakapoifanya haki ipate ushindi; 21 na watu wa mataifa wataweka tumaini lao katika jina lake.”
Yesu Na Beelzebuli
22 Kisha wakamletea kipofu mmoja ambaye pia alikuwa bubu na amepagawa na pepo. Yesu akamponya akaweza kusema na kuona. 23 Watu wote wakashangaa wakaulizana, “Je, yawezekana huyu ndiye Mwana wa Daudi?”
Copyright © 1989 by Biblica