Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Old/New Testament

Each day includes a passage from both the Old Testament and New Testament.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: 2Kgs for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Yohana 4:31-54

31 Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wakimsihi, “Rabi, kula angalau cho chote.”

32 Lakini yeye akawajibu, “Mimi ninacho chakula ambacho ninyi hamkifahamu.”

33 Basi wanafunzi wakaanza kuulizana, “Kuna mtu ambaye amemletea chakula?” 34 Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma, na kuikamilisha kazi yake. 35 Si mnao msemo kwamba, ‘Bado miezi minne tutavuna’? Hebu yaangalieni mashamba, jinsi mazao yalivyoiva tayari kuvunwa! 36 Mvunaji hupokea ujira wake, naye hukusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele. Kwa hiyo aliyepanda mbegu na anayevuna, wata furahi pamoja. 37 Ule msemo wa zamani kwamba , ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa. 38 Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi hiyo; ninyi mmefaidika kutokana na jasho lao!”

39 Wasamaria wengi walimwamini kutokana na ushuhuda wa yule mama alipowaambia kwamba, “Ameniambia mambo yote niliyowahi kutenda.” 40 Kwa hiyo wale Wasamaria walipokuja, walimsihi akae kwao, naye akakaa kwa siku mbili. 41 Watu wengi zaidi wakamwa mini kutokana na ujumbe wake. 42 Wakamwambia yule mama, sasa hatuamini tu kwa sababu ya yale uliyotuambia bali kwa kuwa tumem sikia sisi wenyewe, na tunajua hakika kwamba yeye ni Mwokozi wa ulimwengu.”

Yesu Amponya Mtoto Wa Afisa

43 Zile siku mbili zilipokwisha, Yesu aliondoka kwenda Gali laya. 44 Yesu mwenyewe alikwisha sema kwamba nabii haheshimiki nchini kwake. 45 Lakini alipofika, Wagalilaya walimpokea vizuri baada ya kuona mambo aliyofanya huko Yerusalemu wakati wa siku kuu, maana na wao walihudhuria.

46 Alikwenda tena mjini Kana katika Galilaya, kule alipo geuza maji kuwa divai. Na huko Kapernaumu alikuwapo afisa mmoja ambaye mtoto wake alikuwa mgonjwa. 47 Huyo afisa alipopata habari kuwa Yesu alikuwa amefika Galilaya kutoka Yudea, alikwenda akamwomba aje kumponya mwanae ambaye alikuwa mgonjwa karibu ya kufa.

48 Yesu akamwambia, “Ninyi watu hamwezi kuamini pasipo kuona ishara na miujiza?”

49 Yule afisa akajibu, “Bwana, tafadhali njoo kabla mwa nangu hajafa.” 50 Yesu akamwambia, “Nenda nyumbani, mwanao ataishi.” Yule afisa akaamini maneno ya Yesu, akaondoka kurudi nyumbani. 51 Alipokuwa bado yuko njiani, alikutana na watumishi wake wakamwambia kwamba mwanae alikuwa mzima. 52 Akawauliza saa ambayo alianza kupata nafuu. Wakamwambia, “Jana yapata saa saba, homa ilimwacha.” 53 Yule baba akakumbuka kuwa huo ndio wakati ambapo Yesu alikuwa amemwambia, “Mwanao ataishi.” Kwa hiyo yeye, pamoja na jamaa yake yote wakamwamini Yesu.

54 Hii ilikuwa ishara ya pili ambayo Yesu alifanya aliporudi Galilaya kutoka Yudea.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica