Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Old/New Testament

Each day includes a passage from both the Old Testament and New Testament.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: Exod for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Matayo 14:22-36

Yesu Atembea Juu Ya Maji

22 Baadaye Yesu akawaambia wanafunzi wake watangulie kwe nye mashua waende ng’ambo ya pili ya ziwa, wakati yeye anawaaga wale watu. 23 Baada ya kuwaaga, akaenda mlimani peke yake kuomba. Jioni ilipofika, Yesu alikuwa hapo peke yake. 24 Wakati huo ile mashua ilikwisha fika mbali, ikisukwa sukwa na mawimbi kwa sababu upepo ulikuwa mkali.

25 Ilipokaribia alfajiri, Yesu akawaendea wanafunzi wake akiwa anatembea juu ya maji. 26 Lakini wanafunzi wake walipom wona akitembea juu ya maji, waliingiwa na hofu kuu. Wakasema, “Ni mzimu.” Wakapiga mayowe kwa hofu. 27 Lakini mara moja Yesu akasema nao, akawaambia, “Jipeni moyo. Ni mimi; msiogope.”

28 Petro akamjibu, “Bwana, kama ni wewe, niambie nije kwako nikitembea juu ya maji.” 29 Yesu akamwambia, “Njoo.” Basi Petro akatoka katika mashua, akatembea juu ya maji akimfuata Yesu. 30 Lakini alipoona upepo mkali aliingiwa na hofu, akaanza kuzama, huku akipiga kelele, “Bwana, niokoe!”

31 Mara Yesu akanyoosha mkono wake, akamshika, akamwambia, “Wewe mwenye imani haba, kwa nini ulikuwa na shaka?” 32 Na walipoingia katika mashua, upepo ukakoma. 33 Wote waliokuwamo katika mashua wakamwabudu wakisema, “Hakika, wewe ni Mwana wa

Yesu Awaponya Wagonjwa Genesareti

34 Walipokwisha kuvuka, wakafika Genesareti. 35 Watu wa eneo lile walipomtambua Yesu, walipeleka habari sehemu zote za jirani na watu wakawaleta wagonjwa wote kwake 36 wakamsihi awaru husu wagonjwa waguse tu pindo la vazi lake. Na wote waliomgusa, waliponywa.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica