Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Read the New Testament in 24 Weeks

A reading plan that walks through the entire New Testament in 24 weeks of daily readings.
Duration: 168 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Waebrania 1-2

Mungu Amesema Kupitia Mwanaye

Zamani Mungu alisema na baba zetu kwa kuwatumia manabii. Alisema nao mara nyingi na kwa njia nyingi tofauti. Lakini sasa katika siku hizi za mwisho Mungu amesema nasi tena kupitia Mwana wake. Mungu aliuumba ulimwengu wote kupitia Mwana wake. Na alimchagua Mwana kumiliki mambo yote. Huyo Mwana huuonesha utukufu wa Mungu. Yeye ni nakala halisi ya asili yake Mungu, na huviunganisha vitu vyote pamoja kwa amri yake yenye nguvu. Mwana aliwasafisha watu kutoka katika dhambi zao. Kisha akaketi upande wa kuume[a] wa Mungu, aliye Mkuu huko Mbinguni. Mwana akawa mkuu zaidi kuliko malaika, na Mungu akampa jina lililo kuu zaidi kuliko lolote katika majina yao.

Mungu kamwe hajamwambia malaika yeyote maneno haya:

“Wewe ni Mwanangu.
    Mimi leo hii nimekuwa Baba yako.”(A)

Mungu pia kamwe hajasema juu ya malaika,

“Nitakuwa Baba yake,
    naye atakuwa mwanangu.”(B)

Na kisha, pale Mungu anapomtambulisha Mwanaye mzaliwa wa kwanza ulimwenguni,[b] anasema,

“Basi malaika wote wa Mungu wamwabudu yeye.”[c]

Hivi ndivyo Mungu alivyosema kuhusu malaika:

“Yeye huwabadilisha malaika zake kuwa upepo[d]
    na watumishi wake kuwa miali ya moto.”(C)

Lakini hivi ndivyo alivyosema kuhusu Mwana wake:

“Mungu, ufalme wako utadumu milele na milele.
    Unatumia mamlaka yako kwa haki.
Unapenda kilicho sahihi na kuchukia kilicho na makosa.
    Hivyo Mungu, Mungu wako, amekuchagua wewe,
    na amekupa heshima na furaha zaidi kupita yeyote aliye kama wewe.”(D)

10 Pia Mungu alisema,

“Ee Bwana, mwanzo uliiumba dunia,
    na mikono yako ikaliumba anga.
11 Vitu hivi vitatoweka, lakini wewe utaendelea kuwepo.
    Vyote vitachakaa kama mavazi makuu kuu.
12 Utavikunja hivyo kama koti,
    navyo vitabadilishwa kama mavazi.
Lakini wewe hubadiliki,
    na uhai wako hautafikia mwisho.”(E)

13 Na Mungu hakuwahi kusema haya kwa malaika:

“Ukae mkono wangu wa kuume
    hadi nitakapowaweka adui zako chini ya uwezo wako.”[e](F)

14 Malaika wote ni roho ambao humtumikia Mungu nao hutumwa kuwasaidia wale watakaoupokea wokovu.

Wokovu Wetu ni Mkuu Kuliko Sheria

Hivyo tunapaswa kuwa makini zaidi kuzingatia yale tuliyofundishwa. Tunapaswa kuwa makini ili tusiondolewe polepole kutoka katika njia iliyo ya kweli. Fundisho kwamba Mungu alizungumza kupitia malaika limedhihirishwa kuwa ni la kweli. Na kila mara watu wake walipotenda jambo kinyume na fundisho lake, waliadhibiwa kwa yale waliyofanya. Waliadhibiwa walipoacha kutii fundisho hilo. Hivyo kwa hakika hata nasi tutaadhibiwa kama hatutauzingatia wokovu mkuu tulionao. Alikuwa ni Bwana Yesu aliyewaambia watu kwa mara ya kwanza juu ya wokovu huo. Na wale waliomsikiliza walithibitisha kwetu kuwa yale mambo yalikuwa ni kweli. Mungu alithibitisha hayo pia kwa kutumia ishara, maajabu, na aina zingine zote za miujiza. Na alithibitisha hayo kwa kuwapa watu vipawa tofauti kwa njia ya Roho Mtakatifu kwa namna ile aliyotaka.

Kristo Akawa Kama Watu Ili Awaokoe

Mungu hakuwachagua malaika wawe watawala juu ya ulimwengu mpya unaokuja. Ulimwengu huo ujao ni ndiyo ambao tumekuwa tukiuzungumzia. Imeandikwa mahali fulani katika Maandiko:

“Kwa nini watu ni muhimu sana kwako?
    Kwa nini hata unafikiri juu yao?
Kwa nini unamjali mwana wa mwanadamu?[f]
    Je, yeye ni muhimu kiasi hicho?
Kwa muda mfupi ulimfanya awe chini kuliko malaika.
    Ukamvisha taji yenye utukufu na heshima.
Ukaweka kila kitu chini ya udhibiti wake.”[g](G)

Kama Mungu aliweka vitu vyote chini ya udhibiti wake, basi hakikuwepo chochote kilichoachwa ambacho hakukitawala. Lakini bado hatujamwona akitawala juu ya vyote. Kwa kipindi kifupi Yesu aliwekwa chini kuliko malaika, lakini sasa tunamwona akiwa amevaa taji ya utukufu na heshima kwa sababu aliteseka na kufa. Kwa sababu ya neema ya Mungu, Yesu alikufa kwa ajili ya kila mmoja.

10 Mungu aliyeumba vitu vyote na ambaye kwa utukufu wake vitu vyote vipo; alitaka watu wengi wawe watoto wake na kuushiriki utukufu wake. Hivyo alifanya yale aliyohitaji kuyafanya. Alimkamilisha yeye anayewaongoza watu hao kuuelekea wokovu. Kwa njia ya mateso yake Mungu alimfanya Yesu kuwa Mwokozi mkamilifu.

11 Yesu, ambaye anawafanya watu kuwa watakatifu, na wale wanaofanywa kuwa watakatifu wanatoka katika familia moja. Hivyo haoni aibu kuwaita kaka na dada zake. 12 Anasema,

“Mungu, nitawaeleza kaka na dada zangu habari zako.
    Mbele za watu wako wote nitaziimba sifa zako.”(H)

13 Pia anasema,

“Nitamwamini Mungu.”(I)

Na pia anasema,

“Nipo hapa, na pamoja ni wapo watoto
    niliopewa na Mungu.”(J)

14 Watoto hawa ni watu walio na miili ya damu na nyama. Hivyo Yesu mwenyewe akawa kama wao na akapata uzoefu ule ule waliokuwa nao. Yesu alifanya hivi ili, kwa kufa kwake, aweze kumharibu yeye aliye na nguvu ya mauti, Ibilisi. 15 Yesu akawa kama watu hawa na akafa ili aweze kuwaweka huru. Walikuwa kama watumwa maisha yao yote kwa sababu ya kuogopa kwao kifo. 16 Kwa uwazi, siyo malaika ambao Yesu huwasaidia. Yeye huwasaidia watu waliotoka kwa Ibrahimu. 17 Kwa sababu hii, Yesu alifanyika kama sisi, kaka na dada zake kwa kila namna. Akawa kama sisi ili aweze kuhudumu kwa niaba yetu mbele za Mungu wa kuhani mkuu aliye mwaminifu na mwenye rehema. Ndipo angetoa sadaka ya kuziondoa dhambi za watu. 18 Na sasa anaweza kuwasaidia wale wanaojaribiwa. Yuko radhi kuwasaidia kwa sababu yeye mwenyewe aliteseka na alijaribiwa.

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International