Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

M’Cheyne Bible Reading Plan

The classic M'Cheyne plan--read the Old Testament, New Testament, and Psalms or Gospels every day.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: 2Chr for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Ufunua wa Yohana 22

Mto Wa Maji Ya Uzima

22 Kisha yule malaika akanionyesha mto wa maji ya uzima ung’aao kama kioo na kutiririka kutoka kwenye kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo, kupitia katikati ya barabara kuu ya mji huo. Katika pande zote za mto huo kulikuwa na mti wa uzima utoao matunda ya aina kumi na mbili, na kuzaa matunda yake kila mwezi. Majani yake ni ya kuwaponya watu wa mataifa. Katika mji huo hakutakuwa na kitu cho chote kilicholaaniwa, bali kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo humo na watumishi wake watamwabudu. Watamwona uso wake na jina lake litakuwa kwe nye vipaji vya nyuso zao. Usiku hautakuwapo tena; wala hawata hitaji mwanga wa taa au wa jua, maana Bwana Mungu atakuwa nuru yao, watatawala milele na milele.

Bwana Yesu Anakuja

Kisha yule malaika akaniambia, “Maneno haya ni ya kuami nika na ya kweli. Bwana, Mungu wa roho za manabii, amemtuma mal aika wake kuwaonyesha watumishi wake yale ambayo hayana budi kutokea karibuni. Tazama, ninakuja upesi! Amebarikiwa anayesh ika maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki.”

Mimi Yohana, ndiye niliyesikia na kuona mambo haya. Na nil ipokwisha kuyasikia na kuyaona, nilianguka kifudifudi penye miguu ya yule malaika aliyenionyesha mambo hayo, nimwabudu. Lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi pamoja na wewe na ndugu zako manabii na wote wanaoshika maneno ya kitabu hiki. Mwabudu Mungu!”

10 Kisha akaniambia, “Usiyawekee muhuri maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki maana wakati umekaribia. 11 Mwache atendaye uovu aendelee kutenda uovu, na aliye mchafu aendelee kuwa mchafu; na atendaye mema aendelee kutenda mema na aliye mta katifu aendelee kuwa mtakatifu.”

12 “Tazama, Ninakuja upesi! Nakuja na tuzo yangu, nimpe tuzo kila mtu kulingana na matendo yake. 13 Mimi ni Alfa na Omega, wa kwanza na wa wisho, Mwanzo na Mwisho.” 14 Wamebari kiwa wanaoosha mavazi yao ili wapate haki ya kushiriki mti wa uzima na wapate kuingia katika ule mji kupitia kwenye milango yake. 15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye udanganyifu na kuutenda. 16 Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia mambo haya kwa ajili ya makanisa. Mimi ni Shina na Mzao wa ukoo wa Daudi. Mimi ni Nyota ya asubuhi ing’aayo.”

17 Roho na bibi harusi wanasema, “Njoo!” Na kila mtu asi kiaye na aseme, “Njoo!” Na mtu ye yote mwenye kiu na aje, na kila anayetaka na apokee zawadi ya maji ya uzima bure. .

18 Namwonya kila mtu asikiaye maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki: mtu ye yote akiyaongezea cho chote, Mungu atamwongezea maafa yaliyoandikwa katika kitabu hiki. 19 Na kama mtu ye yote akipunguza cho chote katika maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, Mungu atamnyang’anya sehemu yake katika mti wa uzima na katika mji mtakatifu, ambayo yameelezwa katika kitabu hiki.

20 Yeye anayeshuhudia mambo haya anasema, “Hakika ninakuja upesi!” Amina. Njoo, Bwana Yesu!

Error: Book name not found: Mal for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Yohana 21

Yesu Ajitambulisha Kwa Wanafunzi Saba

21 Baada ya haya Yesu alijitambulisha tena kwa wanafunzi wake kando ya bahari ya Tiberia. Ilitokea hivi: Simoni Petro, Tomaso aitwaye Pacha, Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja. Simoni Petro aka waambia wenzake, “Mimi nakwenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua. Lakini usiku ule hawakupata cho chote. Kulipopambazuka, Yesu alisimama ufukoni, lakini wale wana funzi hawakumtambua. Yesu akawaambia, “Wanangu, mmepata samaki wo wote?” Wakamjibu, “La.” Akawaambia, “Shusheni wavu upande wa kulia wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Walivyofa nya hivyo walipata samaki wengi mno hata wakashindwa kuingiza ule wavu uliojaa samaki katika mashua! Kisha yule mwanafunzi ali yependwa na Yesu akamwambia Petro, “Ni Bwana!” Petro aliposikia haya akajifunga nguo yake, kwa kuwa alikuwa amevua wakati wakifa nya kazi, akajitosa baharini, akaogelea kuelekea ufukoni. Wale wanafunzi wengine wakaja kwa ile mashua huku wakivuta ule wavu uliojaa samaki. Hapo walipokuwa wakivua hapakuwa mbali na nchi kavu; ilikuwa kama hatua mia moja hivi.

Walipowasili nchi kavu, wakaona moto wa mkaa na samaki wakiokwa juu yake, na mikate. 10 Yesu akawaambia, “Leteni baadhi ya samaki mliovua.” 11 Simoni Petro akaenda akauvuta ule wavu ambao ulikuwa umejaa samaki wakubwa mia moja hamsini na tatu, akauleta ufukoni. Ingawa samaki walikuwa wengi kiasi hicho, ule wavu haukuchanika. 12 Yesu akawaambia, “Njooni mle.” Hakuna hata mmoja wao aliyethubutu kumwuliza, “Wewe ni nani?” Walijua hakika ya kuwa ni Bwana. 13 Yesu akaenda akachu kua ile mikate na baadaye samaki, akawagawia. 14 Hii ilikuwa ni mara ya tatu Yesu kujitambulisha kwa wanafunzi wake tangu afufuke kutoka kwa wafu.

Yesu Amwuliza Petro Kama Anampenda

15 Walipokwisha kula, Yesu akamwuliza Simoni Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?” Yeye akamjibu, “Ndio Bwana, wewe unajua ya kuwa nakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wana kondoo wangu.” 16 Kwa mara nyingine Yesu akamwul iza Simoni Petro, “Simoni, mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akajibu, “Ndio Bwana, wewe unajua ya kuwa nakupenda.” Akamwam bia, “Chunga kondoo wangu.” 17 Kwa mara ya tatu Yesu akamwul iza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akahuzu nika sana kwa kuwa Yesu alimwuliza mara ya tatu, ‘Unanipenda?’ Akamjibu, “Bwana, wewe unajua kila kitu. Unajua ya kuwa naku penda.” Yesu akamwambia, “Lisha kondoo wangu. 18 Nakuambia wazi, ulipokuwa kijana ulivaa na kwenda unakotaka; lakini ukiwa mzee utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvika nguo na kukupeleka usipotaka kwenda.” 19 Alisema haya ili kumfahamisha Petro jinsi atakavyokufa, na kwa kifo hicho Mungu atukuzwe. Kisha Yesu akamwambia Petro, “Nifuate.” 20 Petro akageuka akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akiwafuata. Huyu mwanafunzi ndiye yule aliyekaa karibu kabisa na Yesu alipokula naye chakula cha mwisho akauliza, ‘Bwana, ni nani atakayekusaliti?’ 21 Petro alipomwona huyo mwanafunzi akamwuliza Yesu, “Bwana, na huyu je?” 22 Yesu akamjibu, “ Ikiwa nataka aishi mpaka nitakapo rudi, inakuhusu nini? Wewe nifuate!” 23 Kwa sababu ya maneno haya ya Yesu, uvumi ukaenea kati ya ndugu kwamba huyu mwanafunzi hangekufa. Lakini Yesu hakusema kuwa hangekufa. Yeye alisema tu kwamba, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini?”

24 Huyu ndiye yule mwanafunzi ambaye anashuhudia mambo haya na ndiye ambaye ameandika habari hizi. Nasi tunajua ya kuwa ushu huda wake ni wa kweli.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica