Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

M’Cheyne Bible Reading Plan

The classic M'Cheyne plan--read the Old Testament, New Testament, and Psalms or Gospels every day.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: Judg for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Matendo Ya Mitume 15

Wayahudi. 28 Wakakaa huko na wale wanafunzi kwa muda mrefu.

Baraza La Yerusalemu

15 Watu wengine walikuja Antiokia kutoka Yudea wakawa wakiwa fundisha ndugu walioamini kwamba, “Kama hamkutahiriwa kufuatana na desturi iliyofundishwa na Musa hamwezi kuokolewa.” Paulo na Barnaba walikuwa na mabishano makali nao wakipinga mafundisho haya. Ikaamuliwa kwamba Paulo na Barnaba na waamini wengine waende Yerusalemu wakawaulize mitume na wazee juu ya jambo hili. Kwa hiyo, wakiwa wametumwa na kanisa, njiani walipitia makanisa ya Foenike na Samaria wakatoa taarifa jinsi watu wa mataifa men gine walivyokuwa wakimgeukia Bwana. Habari hizi ziliwafurahisha sana hao ndugu. Walipofika Yerusalemu walipokelewa na kanisa, mitume na wazee; nao wakatoa taarifa kuhusu mambo yote ambayo Mungu aliyafanya kwa kuwatumia wao. Lakini baadhi ya waamini waliokuwa wakishikilia desturi za Mafarisayo wakasema, “Ni lazima watahiriwe na wafundishwe kushika sheria ya Musa.”

Mitume na wazee wa kanisa wakakutana kushauriana juu ya jambo hili. Baada ya majadiliano marefu, Petro akasimama na kusema, “Ndugu zangu, mnajua kwamba siku za mwanzo Mungu alini chagua ili kwa midomo yangu watu wa mataifa mengine wapate kusi kia Habari Njema na kuamini. Na Mungu ambaye anajua mioyo ya watu alishuhudia kwamba anawakubali watu wa mataifa kwa kuwapa Roho Mtakatifu kama alivyotupa na sisi. Mungu hakutofautisha kati yetu na wao, bali alitakasa mioyo yao kwa sababu waliamini. 10 Sasa basi, mbona mnataka kumjaribu Mungu kwa kuwatwika hawa ndugu wanafunzi mzigo wa sheria ambao baba zetu na sisi tumesh indwa kuubeba? 11 Sisi tunaamini ya kuwa tunaokolewa kwa neema ya Bwana wetu Yesu, kama na wao wanavyookolewa.” 12 Baraza lote likakaa kimya; wakawasikiliza Paulo na Barnaba wakieleza jinsi Mungu alivyowatumia kutenda ishara na maajabu kwa watu wa mataifa. 13 Walipomaliza maelezo yao, Yakobo akasema, “Ndugu zangu, nisikilizeni. 14 Simoni amekwisha kutueleza jinsi, kwa mara ya kwanza, Mungu amejichagulia waamini kutoka kwa watu wa mataifa. 15 Hata maneno ya manabii yanakubaliana kabisa na jambo hili. Kama ilivyoandikwa: 16 ‘ Baada ya mambo haya nitarudi, nami nitajenga upya nyumba ya Daudi ambayo imeanguka. Nitajenga tena magofu yake na kuisimamisha, 17 ili binadamu wengine wote wamtafute Bwana, pamoja na watu wa mataifa yote ambao wanaitwa kwa jina langu; 18 asema Bwana, ambaye ametufahamisha mambo hayo tangu kale.’

19 “Kwa hiyo uamuzi wangu ni kwamba, tusiwasumbue watu wa mataifa wanaomgeukia Mungu kwa desturi zetu; 20 badala yake, tuwaandikie barua tuwaambie wajiepushe na uchafu wa ibada za sanamu, na zinaa na waache kula nyama ya wanyama walionyongwa au kunywa damu. 21 Kwa maana sheria za Musa zimekuwa zikihubiriwa katika kila mji na kusomwa katika masinagogi kila sabato tangu vizazi vya awali.”

Barua Kwa Waamini Wa Mataifa Mengine

22 Mitume na wazee na kanisa zima wakakubaliana. Wakachagua watu waongozane na Paulo na Barnaba kwenda Antiokia. Walimchagua Yuda aitwaye Barsaba na Sila. Hawa wawili walikuwa viongozi wal ioheshimiwa miongoni mwa ndugu wote. 23 Wakatumwa na barua ifu atayo: “Sisi mitume na wazee, ndugu zenu, tunawasalimu ninyi wa mataifa mlioamini huko Antiokia, Siria na Kilikia. 24 Kwa kuwa tumesikia kwamba kuna baadhi ya watu kati yetu waliokuja huko bila kibali chetu kutatanisha mawazo yenu kwa maneno yao, 25 tumeona ni vyema, kwa kauli moja, kuwachagua watu waje huko pamoja na wapendwa wetu Barnaba na Paulo, 26 ambao wamehatarisha maisha yao kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo. 27 Tumewatuma hawa ndugu, Yuda na Sila, wawaeleze kwa mdomo mambo haya tunayow aandikia. 28 Kwa maana Roho Mtakatifu ameona vyema na sisi tume kubaliana tusiwatwike mzigo mkubwa zaidi ya mambo yafuatayo ambayo ni ya lazima: 29 kwamba msile cho chote kilichotolewa sadaka katika ibada za sanamu, kunywa damu, nyama ya wanyama wal ionyongwa; na muepukane na uasherati. Mkijitenga na mambo haya mtakuwa mmefanya vyema. Kwaherini.”

30 Wale wajumbe walipokwisha kuagwa, wakaondoka wakaenda Antiokia, wakakusanya ushirika wote wa waamini, wakawapa ile barua. 31 Nao watu walipokwisha kuisoma, wakafurahishwa sana na ujumbe wake wa kutia moyo. 32 Yuda na Sila, ambao walikuwa mana bii wa kawapa ushauri mwingi wa kuwatia moyo na kuwajenga katika imani. 33 Wakakaa Antiokia kwa muda na kisha waamini wakawaaga. Wakarudi kwa amani kwa wale waliowatuma. [ 34 Lakini Sila aliona ni vema kukaa huko.] 35 Lakini Paulo na Barnaba walibaki Anti okia pamoja na wengine wengi wakifundisha na kuhubiri neno la

Paulo Na Barnaba Wanatengana

36 Baada ya siku chache Paulo alimwambia Barnaba, “Twende tukawatembelee ndugu katika miji yote ambamo tulihubiri neno la Bwana tuone jinsi waamini wanavyoendelea.” 37 Barnaba alitaka wamchukue Yohana Marko waende naye. 38 Lakini Paulo aliona si vizuri kumchukua kwa sababu aliwahi kuwakimbia walipokuwa huko Pamfilia, akakataa kuendelea kufanya kazi nao. 39 Pakatokea ubishi mkali kati ya Paulo na Barnaba juu ya jambo hili, wakaten gana. Barnaba akamchukua Yohana Marko akaenda naye Kipro. 40 Paulo akamchagua Sila akaondoka baada ya ndugu kuwatakia neema ya Bwana. 41 Naye akapitia Siria na Kilikia wakaimarisha makanisa ya huko.

Error: Book name not found: Jer for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Marko 10

Yesu Afundisha Kuhusu Talaka

10 Yesu akaondoka mahali pale akavuka mto wa Yordani, akaenda sehemu ya Yudea. Umati wa watu ukamfuata tena na kama kawaida yake akawafundisha.

Baadhi ya Mafarisayo wakamjia wakitaka kumtega, wakamwul iza, “Ni halali mtu kumwacha mke wake?”

Yesu akawajibu, “Musa aliwaamuruje?” Wakamjibu, “Musa aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”

Yesu akawaambia, “Musa aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mume na mke. Na kwa sababu hii mume atamwacha baba yake na mama yake na hao wawili, watakuwa mwili mmoja.’ Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena bali mwili mmoja. Basi, alichokiun ganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”

10 Baadaye waliporudi nyumbani , wanafunzi wa Yesu walimwul iza kuhusu jambo hili.

11 Akawajibu, “Mtu ye yote anayempa mkewe talaka na kuoa mke mwingine, anazini kwa yule mke aliyempa talaka. 12 Na mwa namke anayempa mumewe talaka na kuolewa na mume mwingine, anazini pia.”

Yesu Anawabariki Watoto Wadogo

13 Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse lakini wanafunzi wake wakawakemea. 14 Yesu alipoona yaliyokuwa yakitokea alichukizwa, akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa watu kama hawa! 15 Ninawahakikishieni kwamba, mtu ye yote ambaye hataukubali Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.” 16 Akawakumbatia wale watoto wadogo, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.

Mtu Tajiri

17 Yesu alipoanza tena safari yake, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake akamwuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini niurithi Ufalme wa milele?”

18 Yesu akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna ali yemwema isipokuwa Mungu peke yake. 19 Unazifahamu amri ‘Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Usidanganye. Waheshimu baba yako na mama yako .”’

20 Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”

21 Yesu akamtazama kwa moyo wa upendo akamwambia, “Umepun gukiwa na kitu kimoja tu. Nenda ukauze vitu vyote ulivyo navyo uwape maskini fedha utakazopata, nawe utakuwa na utajiri mbin guni; kisha njoo, unifuate.”

22 Yule mtu aliposikia hayo, alisikitika sana, akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa tajiri sana.

23 Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa

Mungu!”

24 Wanafunzi wake wakashtushwa sana na maneno hayo. Lakini Yesu akasema tena, “Wanangu, ni vigumu sana kuingia katika Ufalme wa Mungu. 25 Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”

26 Wanafunzi wake wakashangaa mno. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi anaweza kuokolewa?”

27 Yesu akawatazama akawaambia, “Kwa wanadamu haiwezekani, lakini kwa Mungu si hivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.” 28 Petro akaanza kumwambia, “Sisi tumeacha kila kitu tukakufu ata!”

29 Yesu akajibu, “Ninawaambieni hakika, hakuna mtu ye yote aliyeacha nyumba, kaka, dada, mama, baba, watoto au shamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya kuitangaza Habari Njema, 30 ambaye hatalipwa katika ulimwengu huu mara mia zaidi: nyumba, kaka, dada, mama, watoto, mashamba na mateso pia; na kupewa uzima wa milele katika ulimwengu ujao. 31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”

Yesu Azungumzia Tena Kifo Chake

32 Walikuwa njiani kuelekea Yerusalemu na Yesu alikuwa ame tangulia. Wanafunzi wake walikuwa wamejawa na hofu, na watu wal iowafuata walikuwa wanaogopa. Yesu akawachukua tena wale wana funzi wake kumi na wawili kando akawaambia yatakayompata. 33 Akasema, “Tunakwenda Yerusalemu, na Mimi Mwana wa Adamu nitapelekwa kwa makuhani wakuu na walimu wa sheria; nao watanihu kumu adhabu ya kifo na kunikabidhi kwa mataifa. 34 Wao watanid hihaki na kunitemea mate na kunipiga na kuniua. Baada ya siku tatu, nitafufuka.”

Ombi La Yakobo Na Yohana

35 Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo wakamwendea Yesu wakamwambia, “Bwana, kuna jambo moja tungependa kukuomba.”

36 Akawauliza, “Mngependa niwafanyie jambo gani?”

37 Wakamjibu, “ Tunakuomba utakapoketi katika ufalme wako wa utukufu, uturuhusu tuketi pamoja nawe, mmoja wetu mkono wako wa kulia na mwingine mkono wako wa kushoto.”

38 Yesu akawaambia, “Hamjui mnaloliomba. Mko tayari kunywea kikombe cha mateso nitakachokunywa? Mnaweza kubatizwa ubatizo nitakaobatizwa?”

39 Wakamjibu, “ Tunaweza.” Yesu akawaambia, “Mtakunywa katika kikombe nitakachokunywa na kubatizwa ubatizo nitakaobati zwa. 40 Lakini kuhusu kuketi mkono wangu wa kulia au wa kushoto si juu yangu mimi kuwaruhusu. Mungu atatoa nafasi hizo kwa watu aliowaandalia.”

41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, waliwaka sirikia Yakobo na Yohana. 42 Yesu akawaita wanafunzi wake wote pamoja akawaambia, “Mnafahamu kwamba watu wanaotawala watu wa mataifa hutumia mabavu, na viongozi wa vyeo vya juu hupenda kuon yesha wana madaraka! 43 Lakini haipasi kuwa hivyo kati yenu. Badala yake, anayetaka kuwa mkuu kati yenu hana budi kuwa mtum ishi wenu, 44 na ye yote anayetaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa mtumishi wa wote. 45 Kwa maana hata mimi Mwana wa Adamu sikuja ili nitumikiwe, bali nilikuja ili niwe mtumishi na kutoa maisha yangu yawe fidia kwa ajili ya watu wengi.”

Yesu Amponya Kipofu Bartimayo

46 Wakafika Yeriko. Na Yesu alipokuwa akiondoka pamoja na Wanafunzi wake na umati wa watu, kipofu mmoja, jina lake Barti mayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando kando ya njia, akiomba.

47 Aliposikia kuwa Yesu wa Nazareti alikuwa akipita, akaanza kupiga kelele, “Yesu, Mwana wa Daudi, nionee huruma!”

48 Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya. Lakini yeye alipiga kelele zaidi, “Mwana wa Daudi, nionee huruma!”

49 Yesu akasimama akawaambia, “Mwiteni.” Wakamwita wakamwambia, “Changamka! Usimame, anakuita.”

50 Akatupa vazi lake kando, akaruka juu, akamwendea Yesu. 51 Yesu akamwuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona tena.” 52 Yesu akamwambia, “Nenda, imani yako imekuponya.” Wakati huo huo akaweza kuona, akamfuata Yesu njiani.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica