Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

M’Cheyne Bible Reading Plan

The classic M'Cheyne plan--read the Old Testament, New Testament, and Psalms or Gospels every day.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: Exod for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Yohana 18

Yesu Akamatwa

18 Baada ya sala hii Yesu aliondoka na wanafunzi wake waka vuka kijito cha Kidroni wakaingia katika bustani iliyokuwa upande wa pili. Yuda, ambaye alimsaliti Yesu, pia alipafahamu mahali hapo kwani Yesu alikuwa akikutana na wanafunzi wake hapo mara kwa mara. Kwa hiyo Yuda akaja kwenye bustani hiyo akiongoza kikundi cha askari wa Kirumi na walinzi wa Hekalu kutoka kwa makuhani wakuu na Mafarisayo wakiwa na taa na silaha. Yesu alijua yata kayompata, kwa hiyo akawasogelea akawauliza, “Mnamtafuta nani?” Wao wakamjibu, “Yesu wa Nazareti.” Yesu akawaambia, “Ni mimi.” Yuda ambaye alimsaliti alikuwa amesimama na wale askari. Yesu alipowaambia, ‘Ni mimi,’ walirudi nyuma wakaanguka chini! Akawauliza tena, “Mnamtafuta nani?” Nao wakajibu, “Yesu wa Nazareti .” Yesu akawaambia, “Nimekwisha waeleza kuwa ni mimi; kwa hiyo kama mnanitafuta mimi waachilieni hawa wengine waende.” Alisema haya ili lile neno alilosema lipate kutimia, ‘Kati ya wale ulionipa sikupoteza hata mmoja.’ 10 Ndipo Simoni Petro akachomoa upanga aliokuwa amechukua akamkata sikio la kulia mtumishi wa kuhani mkuu. Jina la mtumishi huyo lilikuwa Malko. 11 Yesu akamwambia Petro, “Rudisha upanga wako kwenye ala. Je, nisinywe kikombe cha mateso alichonipa Baba?” 12 Kwa hiyo mkuu wa kikosi na askari wake pamoja na wale walinzi wa Hekalu waliot umwa na viongozi wa Wayahudi, wakamkamata Yesu wakamfunga mikono. 13 Kisha wakampeleka kwanza kwa Anasi mkwewe Kayafa ambaye ali kuwa ndiye kuhani mkuu mwaka ule. 14 Kayafa ndiye aliyekuwa amewashauri viongozi wengine wa Kiyahudi kwamba ingekuwa afadhali mtu mmoja afe kwa ajili ya watu.

Petro Anamkana Yesu

15 Simoni Petro pamoja na mwanafunzi mwingine walimfuata Yesu. Huyu mwanafunzi mwingine alikuwa anafahamika kwa kuhani mkuu kwa hiyo aliingia ndani ya ukumbi pamoja na Yesu. 16 Lakini Petro alisimama nje karibu na mlango. Ndipo yule mwanafunzi mwin gine akazungumza na msichana aliyekuwa analinda mlangoni, akamru husu amwingize Petro ndani. 17 Yule msichana akamwuliza Petro, “Je, wewe pia ni mmoja wa wanafunzi wa mtu huyu?” Petro aka jibu, “Hata! Mimi sio.” 18 Wale watumishi na askari walikuwa wamesimama wakiota moto wa mkaa ambao walikuwa wamewasha kwa sababu pale ukumbini palikuwa na baridi kali. Petro naye alikuwa amesimama pamoja nao akiota moto.

Kuhani Mkuu Amhoji Yesu

19 Kuhani mkuu akamwuliza Yesu maswali kuhusu wanafunzi wake na mafundisho yake. 20 Yesu akamjibu, “Nimekuwa nikizungumza wazi wazi mbele ya watu wote. Nimefundisha katika masinagogi na Hekaluni ambapo Wayahudi wote hukusanyika. Sijasema jambo lo lote kwa siri. 21 Mbona unaniuliza mimi maswali? Waulize walionisiki liza nimewaambia nini. Wao wanajua niliyosema.” 22 Mmoja wa wale walinzi akampiga Yesu kofi, kisha akasema, “Unathubutuje kumjibu kuhani mkuu hivyo?” 23 Yesu akamjibu, “Kama nimesema jambo baya waeleze watu wote hapa ubaya niliosema. Lakini kama nimesema yaliyo kweli, mbona umenipiga?” 24 Ndipo Anasi akampeleka Yesu kwa kuhani mkuu Kayafa, akiwa bado amefungwa.

Petro Amkana Yesu Tena

25 Wakati huo Simoni Petro alikuwa amesimama akiota moto. Baadhi ya wale waliokuwepo wakamwuliza, “Wewe ni mmoja wa wana funzi wake?” Petro akakana, akasema, “Mimi sio.” 26 Mmoja wa watumishi wa kuhani mkuu, ndugu yake yule mtu ambaye Petro alim kata sikio, akamwuliza, “Je, sikukuona kule bustanini ukiwa na Yesu?” 27 Kwa mara nyingine tena Petro akakataa kwamba alimfa hamu Yesu. Wakati huo huo jogoo akawika.

Yesu Apelekwa Kwa Pilato

28 Ndipo Wayahudi wakamchukua Yesu kutoka kwa Kayafa wakampeleka kwenye ikulu ya gavana wa Kirumi. Ilikuwa ni alfa jiri. Wayahudi waliokuwa wanamshtaki Yesu hawakuingia ndani kwa sababu ya sheria za kiyahudi. Wangehesabiwa kuwa wachafu kama wangeingia nyumbani mwa mtu asiye Myahudi na wasingeruhusiwa kushiriki katika sikukuu ya Pasaka. 29 Kwa hiyo Pilato akatoka nje kuwaona akawauliza, “Mmeleta mashtaka gani kumhusu mtu huyu?” 30 Wao wakamjibu, “Kama huyu mtu hakuwa ametenda maovu tusingemleta kwako.” 31 Pilato akawaambia, “Basi mchukueni ninyi mkamhukumu kwa kufuata sheria zenu.” Wayahudi wakamjibu, “Sisi haturuhusiwi kutoa hukumu ya kifo kwa mtu ye yote.” 32 Walisema hivyo ili yale maneno aliyosema Yesu kuhusu atakavy okufa, yapate kutimia. 33 Kwa hiyo Pilato akaingia ndani akam wita Yesu akamwuliza, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” 34 Yesu akamjibu, “Je, unauliza swali hili kutokana na mawazo yako mwe nyewe au kutokana na ulivyoambiwa kunihusu mimi?” 35 Pilato akamjibu, “Unadhani mimi ni Myahudi? Watu wa taifa lako na maku hani wao wakuu wamekushtaki kwangu. Umefanya kosa gani?” 36 Ndipo Yesu akamwambia, “Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Ingekuwa hivyo, watumishi wangu wangenipigania na kuhakikisha kuwa siwekwi mikononi mwa Wayahudi; lakini Ufalme wangu hautoki ulimwenguni.” 37 Pilato akasema, “Kwa hiyo wewe ni mfalme?” Yesu akajibu, “Wewe umesema mimi ni mfalme. Nimezaliwa na nime kuja ulimwenguni kwa makusudi ya kushuhudia kweli. Mtu ye yote anayepokea yaliyo ya kweli anakubaliana na mafundisho yangu.” 38 Pilato akamwuliza Yesu, “Kweli ni nini?” Baada ya kusema haya Pilato akaenda nje tena akawaambia wale viongozi wa Wayahudi waliomshtaki Yesu, “Sioni kosa lo lote ali lotenda mtu huyu.

39 Lakini kuna desturi yenu kwamba wakati wa Pasaka nimwachilie huru mfungwa mmoja mnayemtaka. Je, mngependa nimwachilie huru huyu ‘Mfalme wa Wayahudi?” ’ 40 Wao wakapiga kelele wakisema, “Hapana, usimwachilie huyo. Tufungulie Bar aba!” Baraba alikuwa mnyang’anyi.

Error: Book name not found: Prov for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Wafilipi 2

Unyenyekevu Na Ukuu Wa Kristo

Ikiwa mmepata faraja kwa kuwa mmeunganishwa na Kristo, kama mmevutwa na upendo wake na kushiriki Roho wake, kama mnaoneana huruma na kusaidiana; basi kamilisheni furaha yangu kwa kuwa na nia moja, upendo mmoja na kuwa wamoja katika roho na shabaha. Msifanye jambo lo lote kwa ajili ya ubinafsi au kwa kujiona, bali kuweni wanyenyekevu, mkiwahesabu wengine kuwa bora kuliko ninyi. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu ajishughulishe pia kwa faida ya wengine. Muwe na nia kama ile aliyokuwa nayo Kristo Yesu; yeye kwa asili alikuwa sawa na Mungu, lakini hakuona kwamba kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kush ikilia sana. Bali alikubali kuacha vyote, akachukua hali ya mtumishi, akazaliwa na umbo la wanadamu. Alipochukua umbo la mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii mpaka kufa, tena kifo cha msalaba. Kwa sababu hiyo, Mungu alimwinua juu kabisa, akampa jina ambalo ni kuu kuliko majina yote; 10 ili kwa jina la Yesu, kila goti lipigwe, mbinguni na duniani na kuzimu; 11 na kila ulimi ukiri kwamba Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu

Ng’aeni Kama Nyota

12 Basi rafiki zangu wapendwa, kama ambavyo mmekuwa mkitii nilipokuwa nanyi, nawasihi mwendelee kunitii vivyo hivyo, na hata zaidi sasa kwa kuwa sipo pamoja nanyi. Endeleeni kufanya bidii kwa ajili ya wokovu wenu huku mkitetemeka na kuogopa. 13 Kwa maana ni Mungu ambaye anatenda kazi ndani yenu, akiwapa nia ya kutimiza mapenzi yake na kuwawezesha kutenda yale yanayompendeza 14 Fanyeni mambo yote bila manung’uniko au mabishano 15 ili msiwe na lawama au kosa bali muwe wana wa Mungu wasio na kasoro katika ulimwengu uliopotoka, mking’aa kama nyota angani, 16 na kusisitiza neno la uzima. Mkifanya hivyo siku ya Kristo nitajisi fia kwamba sikupiga mbio au kufanya kazi bure. 17 Hata kama damu yangu itamwagwa kama sadaka juu ya dhabihu na huduma inayotokana na imani yenu, mimi ninafurahi na kushangilia pamoja nanyi nyote. 18 Vivyo hivyo, nanyi pia mnapaswa kufurahi na kushangilia pamoja nami.

Safari Ya Timotheo Na Epafrodita

19 Nina matumaini katika Bwana Yesu ya kumtuma Timotheo hivi karibuni aje kwenu, ili nipate habari za kunitia moyo kutoka kwenu. 20 Sina mtu mwingine hapa kama yeye, anayewatakieni mema kwa moyo wote. 21 Wengine wanajishughulisha zaidi na mambo yao wenyewe na hawajali lo lote kuhusu kazi ya Yesu Kristo. 22 Lakini ninyi wenyewe mnajua jinsi Timotheo alivyojithibit isha, kwa maana amefanya kazi ya Injili pamoja nami kama vile mtoto na baba yake. 23 Kwa hiyo, natumaini kumtuma Timotheo kwenu mara tu nipatapo habari kuhusu mambo yangu yatakavyokuwa. 24 Nami naamini katika Bwana kwamba mimi mwenyewe nitakuja kwenu hivi karibuni.

25 Nimeona vema kumrudisha ndugu yangu Epafrodita kwenu. Yeye ni mtumishi na askari mwenzangu, ambaye pia ni mjumbe wenu mliyemtuma anihudumie katika mahitaji yangu. 26 Yeye ana hamu kuwaoneni ninyi nyote, na amesikitishwa kwa sababu mlipata habari kwamba alikuwa mgonjwa. 27 Hakika alikuwa mgonjwa, tena karibu ya kufa. Lakini Mungu alimhurumia, na si yeye tu, bali hata na mimi alinihurumia, nisipatwe na huzuni juu ya huzuni . 28 Kwa hiyo napenda kumtuma kwenu ili mtakapomwona kwa mara nyingine, mpate kufurahi, na mimi nipunguziwe wasiwasi wangu. 29 Kwa hiyo mpokeeni katika Bwana kwa furaha kubwa; na wapeni heshima watu kama hawa. 30 Kwa maana alikaribia kufa kwa ajili ya kazi ya Kristo; alihatarisha maisha yake ili aweze kunipa msaada ambao ninyi msingeweza kunipa.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica