M’Cheyne Bible Reading Plan
15 Basi watoza kodi na wenye dhambi wakaja kwa Yesu ili wapate kumsikiliza. 2 Mafarisayo na walimu wa sheria wakaanza kunung’unika, “Huyu mtu anawakaribisha wenye dhambi na kula nao!” 3 Ndipo Yesu akawaambia mfano huu: 4 “Tuseme mmoja wenu ana kondoo mia moja halafu mmoja wao apotee. Si ana waacha wale tisini na tisa malishoni aende kumtafuta huyo aliyepotea mpaka ampate? 5 Akisha kumpata atambeba mabegani mwake na kwenda nyum bani. 6 Kisha atawaita marafiki na majirani na kuwaambia, ‘Fura hini pamoja nami; nimempata kondoo wangu aliyepotea.’ 7 Nawaam bieni, vivyo hivyo kutakuwa na furaha zaidi mbinguni kwa sababu ya mwenye dhambi mmoja atubuye na kuacha dhambi zake, kuliko ilivyo kwa wenye haki tisini na tisa ambao hawana haja ya kutubu.”
Shilingi Iliyopotea
8 “Au tuseme mwanamke ana shilingi kumi halafu apoteze moja. Si atawasha taa afagie nyumba na kutafuta kwa uangalifu mpaka aipate? 9 Na akisha kuipata atawaita marafiki zake na majirani na kuwaambia, ‘Furahini pamoja nami; nimeipata ile shilingi yangu iliyopotea!’ 10 Vivyo hivyo nawaambia, kuna furaha mbele ya mal aika wa Mungu kwa sababu ya mwenye dhambi mmoja atubuye na kuacha dhambi.”
Mwana Mpotevu
11 Yesu akaendelea kusema, “Kulikuwa na mtu aliyekuwa na watoto wawili wa kiume. 12 Yule mdogo akamwambia baba yake, ‘Baba, nipe urithi wangu.’ Basi huyo baba akagawanya mali yake kati yao.
13 “Baada ya muda mfupi yule mdogo akakusanya vitu vyote alivyokuwa navyo akaenda nchi ya mbali akaitapanya mali yake kwa maisha ya anasa. 14 Baada ya kutumia kila kitu alichokuwa nacho, kukawa na njaa kali katika nchi ile yote naye akawa hana cho chote. 15 Kwa hiyo akaomba kibarua kwa raia mmoja wa nchi hiyo aliyemtuma shambani kwake kulisha nguruwe. 16 Akatamani kujish ibisha kwa maganda waliyokuwa wanakula nguruwe, wala hakuna mtu aliyempa cho chote cha kula.
17 “Hatimaye akili zikamrudia, akasema, ‘Ni watumishi wan gapi walioajiriwa na baba yangu ambao wana chakula cha kuwatosha na kusaza nami hapa nakufa kwa njaa! 18 Nitaondoka nirudi kwa baba yangu nikamwambie, ‘Baba, nimetenda dhambi mbele ya Mungu na mbele yako. 19 Sistahili kuitwa mwanao tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako.’ 20 Basi akaondoka, akaenda kwa baba yake. Lakini alipokuwa bado yuko mbali, baba yake akamwona, moyo wake ukajawa na huruma. Akamkimbilia mwanae, akamkumbatia na kumbusu. 21 Yule mtoto akasema, ‘Baba, nimekosa mbele ya Mungu na mbele yako. Sistahili kuitwa mwanao tena.’ 22 Lakini baba yake aka waambia watumishi, ‘Leteni upesi kanzu iliyo bora mumvalishe. Pia mvalisheni pete na viatu. 23 Kisha mleteni yule ndama aliyenona mkamchinje; ili tule tusherehekee. 24 Kwa maana huyu mwanangu alikuwa amekufa, na sasa yu hai tena; alikuwa amepotea na sasa amepatikana.’ Basi wakaanza sherehe.
25 “Wakati huo kaka yake alikuwa shambani. Alipokuwa ana karibia nyumbani akasikia sauti ya nyimbo na ngoma. 26 Akamwita mmoja wa watumishi akamwuliza, ‘Kuna nini?’ 27 Akamwambia, ‘Mdogo wako amekuja, na baba yako amemchinja yule ndama aliyenona kwa sababu amempata mwanawe akiwa mzima.’ 28 Yule kaka akakasi rika, akakataa kuingia ndani. Basi baba yake akaenda nje akaanza kumbembeleza. 29 Lakini yeye akamjibu baba yake, ‘Angalia, miaka yote hii nimekutumikia na hata siku moja sijaacha kutii amri zako, lakini hujanipa hata mwana mbuzi ili nisherehekee na mara fiki zangu. 30 1Lakini huyu mwanao ambaye ametapanya mali yako kwa makahaba amerudi nyumbani nawe umemchinjia ndama aliyenona!’
31 “Baba yake akamwambia, ‘Mwanangu, umekuwa nami siku zote na vyote nilivyo navyo ni vyako. 32 Lakini ilitubidi tufurahi na kusherehekea kwa sababu mdogo wako alikuwa amekufa na sasa yu hai tena, alikuwa amepotea naye amepatikana.”’ Mfano Wa Meneja Mjanja
Matoleo Kwa Ajili Ya Waamini
16 Na sasa kuhusu matoleo kwa ajili ya kuwasaidia watu wa Mungu. Kama nilivyoagiza makanisa ya Galatia, fanyeni vivyo hivyo. 2 Siku ya kwanza ya juma kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha, kulingana na mapato yake, na fedha hiyo aiweke ili nitaka pokuja pasiwepo na haja ya kufanya mchango. 3 Nikishafika nita wapa wale mtakaowachagua barua za kuwatambulisha, ili waweze kupeleka zawadi yenu Yerusalemu. 4 Kama ikionekana ni vyema na mimi niende, basi hao watu watafuatana nami.
Mipango Ya Paulo
5 Baada ya kupitia Makedonia, nitakuja kwenu; maana natazamia kupitia Makedonia. 6 Pengine nitakaa nanyi kwa muda, au hata nitakaa nanyi kipindi chote cha baridi, ili muweze kunisaidia katika safari zangu, po pote niendapo. 7 Kwa maana sipendi niwaone sasa nikiwa napita; natarajia kuwa na muda wa kutosha wa kukaa nanyi, kama Bwana akiruhusu. 8 Lakini nitakaa Efeso mpaka wakati wa Pentekoste. 9 Kwa maana mlango umefunguliwa kwangu kufanya kazi yenye matunda, na huko kuna wapinzani wengi . 10 Ikiwa Timotheo atakuja kwenu mkaribisheni asiwe na woga wo wote akiwa nanyi kwa sababu anaendeleza kazi ya Bwana, kama mimi nifanyavyo. 11 Basi asiwepo mtu atakayemdharau. Msafirisheni kwa amani ili aweze kunirudia. Namtegemea yeye pamoja na hao ndugu.
12 Na sasa, kuhusu ndugu yetu Apolo. Nilimsihi sana awa tembelee pamoja na wale ndugu wengine, lakini haikuwa mapenzi yake kuja huko wakati huu. Atakuja apatapo nafasi.
Maneno Ya Mwisho
13 Kesheni; simameni imara katika imani, muwe shujaa na hodari. 14 Fanyeni kila kitu katika upendo. 15 Sasa ndugu zangu, mnafahamu kwamba watu wa nyumbani kwa Stefana walikuwa waamini wa kwanza katika Akaya, nao wamejitoa kuwasaidia watu wa Mungu. 16 Nawasihi mnyenyekee na kufuata uongozi wa watu kama hawa, na wa kila mtendakazi mwenzenu na kila anayejibidisha katika kazi. 17 Nilifurahi wakati Stefana, Fortunato na Akaiko walipofika, kwa maana hawa wamenisaidia yale niliyopungukiwa kutoka kwenu. 18 Wao wameburudisha roho yangu na yenu pia. Watu kama hawa, wanastahili kutambuliwa. 19 Makanisa ya Asia wanawas alimu. Akila na Priska, pamoja na kanisa lililoko nyumbani kwao wanawasalimu katika Bwana. 20 Pia ndugu wote wanawasalimu. Sali mianeni kwa busu takatifu. 21 Mimi Paulo, kwa mkono wangu mwe nyewe, naandika salamu hii. 22 Kama mtu ye yote hampendi Bwana, na alaaniwe. ‘Maranatha.’ Bwana wetu, njoo! 23 Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
Copyright © 1989 by Biblica