Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

M’Cheyne Bible Reading Plan

The classic M'Cheyne plan--read the Old Testament, New Testament, and Psalms or Gospels every day.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: Exod for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Luka 8

Baada ya haya Yesu alikwenda katika miji na vijiji akifu atana na wanafunzi wake. Kila alipokwenda alihubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu.

Baadhi ya wanawake aliokuwa amewatoa pepo wachafu na kuwa ponya walifuatana naye. Miongoni mwao alikuwepo Mariamu ambaye aliitwa Magdalena, aliyetolewa pepo saba; Yohana mke wa Chuza -msimamizi wa ikulu ya Herode; Susana, na wengine wengi. Wana wake hawa walimhudumia Yesu na wanafunzi wake kutokana na mapato yao wenyewe.

Watu wengi walimiminika kutoka katika kila mji na umati mkubwa ulipokusanyika, Yesu akawaambia mfano huu: “Mkulima mmoja alikwenda shambani kwake kupanda mbegu. Alipokuwa akitawa nya mbegu, nyingine zilianguka njiani zikakanyagwa kanyagwa; na ndege wakazila. Na mbegu nyingine zilianguka penye miamba na zilipomea zikakauka kwa kukosa unyevu. Na mbegu nyingine zil ianguka kwenye miiba, ikazisonga zikafa. Mbegu nyingine zilian guka penye udongo mzuri, nazo zikamea na kutoa mazao mara mia zaidi ya mbegu alizopanda.” Baada ya kutoa mfano huu akasema: “Mwenye nia ya kusikia na asikie!”

Wanafunzi wake wakamwuliza maana ya mfano huu. 10 Naye akawajibu, “Ninyi mmejaliwa kufahamu siri za Ufalme wa Mungu, lakini kwa wengine nazungumza kwa mifano ili, ‘Kuangalia waan galie lakini wasione, kusikia wasikie, lakini wasielewe.’ 11 Maana ya mfano huu ni hii: Mbegu ni neno la Mungu. 12 Ile njia zilipoanguka baadhi ya mbegu, ni mfano wa watu wanaolisikia neno la Mungu lakini shetani huja akalichukua kutoka katika mioyo yao, ili wasiamini na kuokolewa. 13 Ile miamba ambamo mbegu nyingine zilianguka ni sawa na watu ambao hufurahia kusikia mahu biri lakini neno la Mungu halipenyi ndani ya mioyo yao. Hawa huamini kwa muda mfupi lakini wanapojaribiwa hupoteza imani yao. 14 Na ile miiba ambamo mbegu nyingine zilianguka ni sawa na wale wanaosikia neno la Mungu lakini baadaye imani yao inasongwa na mahangaiko ya maisha, utajiri, shughuli na anasa; wasiweze kukua. 15 Bali ule udongo mzuri ambamo mbegu nyingine zilianguka ni sawa na wale ambao hulisikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mwema na wa utii, wakavumilia na kuzaa matunda.”

Mfano Wa Taa

16 “Ni nani anayewasha taa kisha akaifunika, au akaiweka uvunguni, badala ya kuiweka mahali ambapo mwanga wake utaonekana? 17 Hakuna siri ambayo haitafichuliwa, wala hakuna jambo lililo fichika ambalo halitajulikana na kuwekwa wazi. 18 Kwa hiyo muwe waangalifu mnaposikiliza, kwa sababu, yeye aliye na kitu ataonge zewa, naye ambaye hana, atanyang’anywa hata kile anachodhania anacho.”

Ndugu Wa Kweli

19 Wakati mmoja mama yake Yesu na ndugu zake walikuja kum wona lakini hawakuweza kumfikia kwa sababu ya msongamano wa watu. 20 Mtu mmoja akamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje wanataka kukuona.” 21 Yesu akamjibu, “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wote wanaolisikia neno la Mungu na kulitii.”

Bwana Yesu Atuliza Dhoruba

22 Siku moja Yesu alipanda mashua na wanafunzi wake akawaam bia, “Twendeni ng’ambo ya pili ya ziwa.” Kwa hiyo wakaanza kuvuka. Walipokuwa wakivuka, akalala usingizi. Upepo mkali ukawa unavuma na mashua yao ikaanza kujaa maji; wakawa katika hatari ya kuzama.

24 Wale wanafunzi wakamkimbilia Yesu wakamwamsha wakisema, “Bwana, Bwana, tunazama!” Ndipo akaamka akaukemea ule upepo na yale mawimbi vikakoma, pakawa shwari. 25 Kisha akawauliza, “Imani yenu iko wapi?” Wakashangaa na kuogopa. Wakaulizana, “Ni mtu wa namna gani huyu ambaye anaamuru upepo na mawimbi navyo vikamtii?”

Yesu Amponya Mtu Mwenye Pepo

26 Basi wakawasili ng’ambo ya pili katika jimbo la Wagerasi. 27 Na aliposhuka katika mashua alikutana na mtu mmoja wa mji ule aliyepagawa na pepo. Kwa muda mrefu mtu huyu alikuwa havai nguo wala kuishi nyumbani, bali aliishi makaburini. 28 Alipomwona Yesu alipiga kelele, akajitupa chini mbele yake, na kusema kwa sauti kuu, “Unataka nini kwangu, Yesu Mwana wa Mungu Aliye Juu?

Nakuomba, tafadhali usinitese!”

29 Wakati huo Yesu alikuwa ameanza kumwamuru yule pepo mchafu amtoke. Mara nyingi pepo huyo alimwingia na hata alipo fungwa na minyororo na kuwekwa chini ya ulinzi aliivunjilia mbali minyororo hiyo na kukimbilia jangwani akiwa ametawaliwa kabisa na pepo huyo. 30 Yesu akamwuliza, “Jina lako ni nani?” Akamjibu, “Jeshi’ 31 Wale pepo wachafu wakamsihi sana asiwaamuru kwenda shimoni kwenye kifungo cha mashetani.

32 Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe hapo karibu wakilisha kando kando ya mlima. Wale pepo wakamsihi Yesu awaruhusu wawaingie hao nguruwe. Akawaruhusu.

33 Kwa hiyo wakamtoka yule mtu wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe likatimka mbio katika ule mteremko mkali wakatumbukia ziwani na kuzama. 34 Watu waliokuwa wakichunga lile kundi la nguruwe waliona yaliyotokea, wakakimbia wakaeneza habari hizi mjini na mashambani.

35 Watu wakatoka kwenda kujionea wenyewe yaliyotokea. Wali pofika hapo alipokuwa Yesu wakamwona yule mtu aliyetokwa na pepo amekaa karibu na Yesu, akiwa amevaa nguo na mwenye akili timamu! Wakaogopa sana. 36 Wale walioona mambo yalivyotokea wakawasimu lia wenzao jinsi yule mtu alivyoponywa. 37 Watu wote wa jimbo hilo la Wagerasi wakamwomba Yesu aondoke kwao, kwa sababu wali kuwa wamejawa na woga. Basi akaingia katika mtumbwi akaondoka.

38 Yule mtu aliyetolewa pepo akamsihi Yesu afuatane naye. Lakini Yesu akakataa, akamwambia: 39 “Rudi nyumbani ukawaeleze mambo makuu aliyokufanyia Mungu.” Kwa hiyo yule mtu akaenda, akatangaza mji mzima mambo makuu Yesu aliyomfanyia.

Yesu Amfufua Binti Wa Yairo

40 Yesu aliporudi ng’ambo ya pili umati mkubwa wa watu ukam pokea kwa furaha, kwani walikuwa wakimngojea.

41 Wakati huo akaja mtu mmoja jina lake Yairo, kiongozi wa sinagogi. Akapiga magoti mbele ya Yesu akamwomba afike nyumbani kwake, 42 kwa kuwa binti yake mwenye umri wa miaka kumi na mbili, aliyekuwa mtoto wake wa pekee, alikuwa mgonjwa mahututi, karibu ya kufa. Yesu alipokuwa akienda, umati ulimsonga sana.

43 Katika umati huo alikuwepo mama mmoja ambaye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, wala hakuna mganga aliyeweza kumponya. 44 Akaja nyuma ya Yesu, akam gusa pindo la vazi lake. Mara damu iliyokuwa ikimtoka ikakauka, akapona. 45 Yesu akauliza: “Nani amenigusa?” Kila mtu alipo kana Petro akasema, “Bwana, watu ni wengi mno wanaokusonga kila upande.” 46 Yesu akasema: “Kuna mtu aliyenigusa maana naona ya kuwa nguvu za kuponya zimenitoka.” 47 Yule mama alipofahamu ya kuwa amegundulika akaja huku akitetemeka akapiga magoti mbele ya Yesu. Akamweleza Yesu mbele ya watu wote kilichomfanya amguse, na jinsi alivyoponywa mara. 48 Basi Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani.” 49 Wakati Yesu alipo kuwa bado anasema, akaja mtumishi kutoka nyumbani kwa Yairo kum wambia, “Binti yako amefariki. Hakuna sababu ya kuendelea kum sumbua Mwalimu.” 50 Lakini Yesu aliposikia haya alimwambia Yairo, “Usiogope. Uwe na imani na binti yako atapona.” 51 Wal ipofika kwa Yairo akawazuia watu wote wasiingie ndani isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, na baba na mama wa yule binti. 52 Watu waliokuwepo walikuwa wakilia na kuomboleza lakini Yesu akawaam bia, “Acheni kulia! Huyu binti hajafa ila amelala!” 53 Wao wakamcheka kwa dharau maana walijua amekwisha kufa. 54 Yesu akamshika yule binti mkono akamwita: “Binti, amka!” 55 Uhai ukamrudia, naye akasimama mara moja. Yesu akaamuru apewe chakula. 56 Wazazi wake wakastaajabu sana lakini Yesu akawakataza wasim wambie mtu alivyomfufua binti yao.

Error: Book name not found: Job for the version: Neno: Bibilia Takatifu
1 Wakorintho 9

Haki Za Mtume

Je, mimi si huru? Je, mimi si mtume? Je, mimi sikumwona Yesu, Bwana wetu? Je, ninyi si matunda ya kazi yangu katika Bwana? Hata kama mimi si mtume kwa wengine, hakika mimi ni mtume kwenu, kwa maana ninyi ni uthibitisho wa utume wangu katika Bwana. Huu ndio utetezi wangu kwa hao wanaokaa kunihukumu. Je? hatuna haki ya kupewa chakula na cha kunywa? Je, hatuna haki ya kusafiri na mke anayeamini kama wanavyofanya mitume wengine na ndugu zake Bwana na Kefa? Au ni Barnaba na mimi tu ambao tunal azimika kufanya kazi ili tuweze kupata mahitaji yetu?

Ni askari yupi anayelipa gharama zake mwenyewe akiwa kam bini? Ni mkulima gani anayepanda mizabibu na hali matunda yake? Ni mfugaji yupi asiyekunywa maziwa ya kundi la wanyama wake? Mnadhani nasema haya kwa kutumia mifano ya kila siku tu? Je, sheria haisemi vivyo hivyo? Kwa maana sheria ya Musa inasema, “Usimfunge ng’ombe kinywa wakati anapopura nafaka.” Je? Mnad hani ni ng’ombe ambaye Mungu anamfikiria? 10 Je, Mungu hasemi haya hasa kwa ajili yetu? Kwa kweli haya yalisemwa kwa ajili yetu kwa sababu mtu anapolima na mwingine akapura nafaka, wote wana paswa kufanya hivyo wakiwa na matumaini ya kupata sehemu ya mavuno. 11 Je, ikiwa sisi tumepanda mbegu ya kiroho kati yenu, itakuwa ni kitu kikubwa sana iwapo tutavuna mahitaji ya mwili kutoka kwenu? 12 Kama wengine wana haki ya kupata msaada kutoka kwenu, sisi je, isingepasa tuwe na haki hiyo hata zaidi? Lakini sisi hatukupenda kutumia haki hii, bali tunavumilia kila kitu ili tusije tukaweka kizuizi kwenye Injili ya Kristo.

13 Hamjui kwamba, watu walioajiriwa kazi Hekaluni wanapata chak ula chao hekaluni, na wale wanaohudumu madhabahuni wanapata sehemu ya sadaka zinazotolewa? 14 Vivyo hivyo, Bwana aliagiza kwamba wale wanaohubiri Injili watapata chakula chao kutokana na Injili. 15 Lakini mimi sikutumia haki hizi, na wala siandiki haya ili kudai haki zangu. Ni afadhali nife, kuliko mtu aniondolee haki hii ya kujisifu. 16 Ninapohubiri Injili, siwezi kujisifu kwa sababu ninalazimika kuhubiri. Ole wangu nisipohubiri Injili! 17 Nikihubiri kwa hiari ningetegemea kupata tuzo; lakini ikiwa nalazimika kufanya hivyo, basi ninachofanya ni kutekeleza wajibu wangu. 18 Kwa hali hii tuzo yangu ni nini? Tuzo yangu ni hii, kwamba katika kuhubiri kwangu, nitangaze Injili pasipo kudai cho chote na hivyo nisitumie haki zangu katika kuhubiri Injili.

19 Ingawa mimi ni huru, na si mtumwa wa mtu ye yote, nimeji fanya kuwa mtumwa wa wote, ili niweze kuwavuta wengi iwezeka navyo. 20 Kwa Wayahudi, nilikuwa kama Myahudi ili niweze kuwa vuta Wayahudi. Kwa watu wanaotawaliwa na sheria, nilikuwa kama niliye chini ya sheria, ingawa mimi siko chini ya sheria, ili niweze kuwavuta walio chini ya sheria. 21 Kwa watu wasioijua sheria nilikuwa kama nisiye na sheria, ingawa hii haina maana kwamba sizishiki amri za Mungu, bali niko chini ya sheria ya Kristo, ili niweze kuwavuta wasio na sheria. 22 Kwa wadhaifu nilikuwa mdhaifu ili niweze kuwavuta wadhaifu. Nimekuwa mdhaifu ili niweze kuwavuta wadhaifu. Nimekuwa mtu wa hali zote kwa watu wote ili kwa njia zote nipate kuwaokoa baadhi yao. 23 Nafanya haya yote kwa ajili ya Injili, ili nishiriki baraka zake.

24 Mnajua kwamba katika mashindano ya riadha wote wanao shindana hukimbia, lakini ni mmoja wao tu anayepata tuzo. Kwa hiyo kimbieni katika mashindano kwa njia itakayowapatia tuzo. 25 Kila mwana-riadha anayeshiriki katika michezo ya mashindano hufanya mazoezi makali. Wanafanya hivyo ili kupokea tuzo ambayo haidumu, lakini sisi tunafanya hivyo ili kupata tuzo isiyohari bika kamwe. 26 Mimi sikimbii pasipo kuwa na lengo. Sipigani kama mtu anayepiga hewa; 27 lakini nauimarisha mwili wangu na kuutawala, ili baada ya kuwahubiria wengine, mimi mwenyewe nisije nikakataliwa.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica