Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

M’Cheyne Bible Reading Plan

The classic M'Cheyne plan--read the Old Testament, New Testament, and Psalms or Gospels every day.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: Exod for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Luka 6

Bwana Wa Sabato

Siku moja ya sabato Yesu alikuwa akipita katika mashamba ya ngano. Wanafunzi wake wakawa wakivunja masuke ya ngano, wakayafi kicha na kula punje zake. Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnavunja sheria kwa kuvuna ngano siku ya sabato?”

Yesu akawajibu, “Ninyi hamsomi Maandiko? Hamjasoma alicho fanya Mfalme Daudi wakati yeye na wafuasi wake walipokuwa na njaa? Aliingia Hekaluni, akachukua ile mikate ya madhabahuni -ambayo huliwa na makuhani peke yao -akala, kisha akawapa na wafuasi wake wakala!” Akaongezea kusema, “Mimi Mwana wa Adamu ni Bwana wa sabato.”

Ikawa siku nyingine ya sabato Yesu alikuwa akifundisha katika sinagogi, na alikuwepo mtu ambaye mkono wake wa kuume uli kuwa umepooza. Walimu wa sheria na Mafarisayo wakawa wanangoja waone kama atamponya mtu siku ya sabato ili wapate sababu ya kumshtaki. Lakini Yesu alifahamu mawazo yao. Kwa hiyo akamwam bia yule aliyepooza mkono, ’Njoo usimame hapa mbele ili kila mtu akuone.” Yule mtu akaja mbele. Kisha Yesu akawageukia wale walimu wa sheria na Mafarisayo akasema, “Nawauliza ninyi, ni lipi lililo halali siku ya sabato - kutenda mema au kutenda mabaya? Kuokoa maisha au kuyaangamiza?” 10 Akawatazama watu wote waliokuwepo. Kisha akamwambia yule aliyepooza mkono, “Nyoosha mkono wako!” Akaunyoosha na mkono wake ukapona kabisa! 11 Wale wakuu wakakasirika sana. Wakaanza kushauriana, “Tumfa nye nini huyu Yesu?’ ’

Kuchaguliwa Kwa Mitume Kumi Na Wawili

12 Siku moja Yesu alikwenda milimani kuomba, akakesha usiku kucha akimwomba Mungu. 13 Asubuhi akawaita wanafunzi wake, na kati yao akachagua kumi na wawili akawapa cheo cha “mitume.” Majina yao ni haya: 14 Simoni, aliyemwita Petro; Andrea, nduguye Simoni; Yakobo; Yohana; Filipo; Bartholomayo; 15 Mathayo; Tomaso; Yakobo, mwana wa Alfayo; Simoni, aliyeitwa Mzalendo; 16 Yuda, mwana wa Yakobo; na Yuda Iskariote, ambaye baadaye alimsaliti Yesu.

Yesu Aponya Wengi

17 Akashuka pamoja nao akasimama mahali penye uwanja tambar are. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu waliotoka sehemu zote za Yudea na Yerusalemu na kutoka pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walikuwa wamekuja kumsiki liza na kuponywa magonjwa yao. 18 Hata wale waliokuwa wakiteswa na pepo wachafu nao walimjia akawaponya. 19 Na watu wote wali kuwa wanajitahidi kumgusa kwa maana walipofanya hivyo, nguvu zil ikuwa zikimtoka na kuwaponya wote.

20 Kisha akawatazama wanafunzi wake akasema, “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini kwa sababu Ufalme wa mbinguni ni wenu! 21 Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashibishwa! Mmebarikiwa ninyi mnaolia sasa, kwa sababu mtacheka. 22 Mmebari kiwa ninyi watu watakapowachukia na kuwakataa na kuwatukana na kuharibu sifa yenu kwa ajili yangu. 23 Yatakapotokea haya fura hini na kuruka ruka kwa furaha kwa sababu zawadi kubwa imewekwa mbinguni kwa ajili yenu. Hata baba zao waliwatendea manabii wa zamani vivyo hivyo.

24 “Lakini ole wenu ninyi matajiri, kwa sababu mmekwisha pata furaha yenu! Ole wenu ninyi mlioshiba, maana mtaona njaa! 25 Ole wenu ninyi mnaocheka sasa, maana mtalia na kuomboleza! 26 Ole wenu mtakaposifiwa na watu, kwani ndivyo baba zao walivy owasifu manabii wa uongo.”

Wapendeni Adui Zenu

27 “Sikieni niwaambie, wapendeni adui zenu. Watendeeni mema wanaowachukia. 28 Wabarikini wanaowalaani, waombeeni mema wanaowaumiza. 29 Mtu akikupiga kofi, mgeuzie na shavu la pili. Mtu akikunyang’anya koti lako, usimzuie kuchukua na shati lako pia. 30 Aombae mpe, na mtu akichukua mali yako usidai urudishiwe. 31 Watendee wengine unavyopenda nao wakutendee. 32 Je, kuna sifa gani mnapowapenda watu wawapendao? Hata wasiomjua Mungu huwapenda wawapendao. 33 Tena kuna sifa gani mnapowatendea mema wale wanaowatendea mema? Hata wasiomjua Mungu hufanyiana hivyo. 34 Tena mnapowakopesha wale tu ambao mnategemea kuwa watawalipa, kuna sifa gani? Hata watu wasiomjua Mungu huwakopesha wenye dhambi wenzao wakiwa na hakika ya kurudishiwa mali yao yote. 35 Bali, wapendeni adui zenu, watendeeni mema. Wakopesheni bila kutegemea kurudishiwa mlichokopesha. Ndipo mtapata zawadi kubwa nanyi mtakuwa wana wa Mungu Aliye Juu. Yeye ni mwema kwa watu wasio na shukrani na watu waovu. 36 Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.”

Msiwahukumu Wengine

37 “Msiwahukumu wengine nanyi hamtahukumiwa. Msilaani, nanyi hamtalaaniwa. Wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa. 38 Muwe wepesi wa kutoa nanyi mtapokea. Kipimo mtakachotoa mtar udishiwa kikiwa kimejaa na kushindiliwa na kutikiswa na kufurika. Kwa kuwa jinsi mtakavyotoa, ndivyo mtakavyopata.”

Kwa kuwa jinsi mtakavyotoa, ndivyo mtakavyopata.”

39 Pia akawapa mfano akasema, “Je, kipofu anaweza kumwon goza kipofu mwenzake? Si wote wawili watatumbukia shimoni? 40 Mwanafunzi hawezi kuwa mjuzi kuliko mwalimu wake, ila akihi timu, anaweza kuwa bingwa kama mwalimu wake. 41 Mbona unatazama sana kipande kilichoko katika jicho la mwenzako nawe huoni pande lililoko ndani ya jicho lako? 42 Utawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Ndugu yangu, hebu, nikusaidie kutoa kipande hicho ndani ya jicho lako,’ wakati wewe mwenyewe huoni pande hilo lililoko ndani ya jicho lako? Mnafiki wewe! Ondoa kwanza pande hilo ndani ya jicho lako, na ndipo utakapoweza kuona vizuri na kuondoa kipande kili choko ndani ya jicho la ndugu yako.

43 “Hakuna mti bora uzaao matunda hafifu wala hakuna mti hafifu uzaao matunda bora. 44 Kila mti hutambuliwa kwa matunda yake. Tini hazichumwi kwenye michongoma wala zabibu hazichumwi kwenye majani mwitu. 45 Hali kadhalika mtu mwema hutambulikana kwa matendo yake mazuri yatokayo katika moyo mwema. Mtu mwovu pia hutenda maovu yatokanayo na uovu uliojaa ndani ya moyo wake. Mtu hunena yale yaliyojaa moyoni mwake.

46 “Kwa nini mnaniita, ‘Bwana, Bwana’ nanyi hamfanyi ninay owaambia?

47 Nitawaambieni alivyo mtu anayesikia na kufanya ninay osema. 48 Yeye ni kama mtu aliyejenga nyumba akachimba chini na kujenga msingi kwenye mwamba. Mafuriko yalipotokea, yakaikumba ile nyumba wala haikutikisika, kwani ilikuwa na msingi imara. 49 Lakini yeye ayasikiaye maneno yangu na asiyafuate, ni kama mtu aliyejenga nyumba juu ya mchanga bila kuweka msingi. Mafuriko yalipoikumba nyumba ile, ilianguka mara, na kuporomoka kabisa.”

Error: Book name not found: Job for the version: Neno: Bibilia Takatifu
1 Wakorintho 7

Kuhusu Ndoa

Na sasa kuhusu mambo mliyoniandikia. Ni vizuri mtu asioe. Lakini kwa kuwa dhambi ya zinaa imeenea, kila mwanamume awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe.

Mume atimize wajibu wake wa ndoa kwa mkewe; na hali kadhal ika mke kwa mumewe. Kwa maana mke hatawali mwili wake mwe nyewe, bali mume wake ndiye autawalaye. Vivyo hivyo, mume hata wali mwili wake mwenyewe, bali mkewe ndiye anayeutawala. Msiny imane, isipokuwa kama mmekubaliana kufanya hivyo kwa muda mfupi ili muwe na nafasi nzuri ya maombi. Lakini baada ya muda huo rudianeni tena shetani asije akapata nafasi ya kuwajaribu kwa sababu ya kushindwa kujizuia. Nasema haya kama ushauri, na si sheria. Ningalipenda wote wawe kama mimi nilivyo. Lakini kila mtu amepewa karama yake kutoka kwa Mungu, mmoja ana karama hii na mwingine ana karama ile.

Na sasa nasema kwa wale wasioolewa na kwa wajane. Ingekuwa vizuri kama wangeendelea kuishi bila kuoa au kuolewa kama mimi. Lakini kama hawawezi kujizuia, basi waoe. Ni afadhali kuoa kuliko kuwaka kwa tamaa.

10 Kwa wale waliooana ninayo amri, si amri yangu ila ni ya Bwana. Mke asimwache mumewe. 11 Lakini kama akimwacha, ni lazima akae bila kuolewa, ama sivyo apatane tena na mumewe. Na mume asimpe mkewe talaka.

12 Lakini kwa wengine nasema, si Bwana ila ni mimi: kama ndugu ana mke asiyeamini, na huyo mke amekubali kuishi pamoja naye, basi asimpe talaka. 13 Na kama mwanamke mwamini ameolewa na mwanaume asiyeamini, na huyo mwanaume amekubali kuishi naye, basi huyo mwanamke asimpe talaka. 14 Kwa maana huyo mwanaume asiyeamini anatakaswa kwa ajili ya mkewe naye mwanamke asiyeamini anatakaswa kwa ajili ya mumewe anayeamini. Kama isingalikuwa hivyo watoto wao wangalikuwa si safi, lakini ilivyo sasa wao ni watakatifu. 15 Lakini kama yule asiyeamini akitaka kuachana na mwenzake anayeamini, basi na iwe hivyo. Katika hali hiyo mke au mume ambaye ni mwamini hafungwi. Kwa sababu Mungu ametuita tuishi kwa amani. 16 Wewe mke, unajuaje kama hutamwokoa mumeo? Wewe mume unajuaje kama hutamwokoa mkeo?

Kuishi Kama Mlivyoitwa

17 Kila mtu aishi maisha aliyopangiwa na Bwana, na ambayo ameitiwa na Mungu. Hii ndio amri ninayotoa kwa makanisa yote.

18 Kama mtu alikuwa ametahiriwa alipoitwa, basi asijaribu kuondoa alama za kutahiriwa kwake. Na kama mtu alikuwa hajatahi riwa alipoitwa, basi, asitafute kutahiriwa. 19 Kwa kuwa kutahi riwa au kutotahiriwa si kitu. Jambo lililo muhimu ni kutii amri za Mungu . 20 Kila mtu abaki katika nafasi ambayo alikuwa nayo alipoitwa kuamini. 21 Je, wewe ulipoitwa ulikuwa mtumwa? Jambo hilo lisikusumbue. Lakini kama unaweza kuwa huru, utumie nafasi hiyo. 22 Kwa maana aliyeitwa kwa Bwana akiwa mtumwa ni mtu huru wa Bwana. Hali kadhalika mtu aliyekuwa huru alipoitwa ni mtumwa wa Kristo. 23 Mmenunuliwa kwa gharama; msikubali kuwa watumwa wa watu. 24 Kwa hiyo ndugu zangu, kila mmoja wenu akae na Mungu katika nafasi aliyokuwa nayo alipoitwa.

Kwa Hali Ya Sasa, Afadhali Kutokuoa

25 Sasa, kuhusu wale walio bikira. Sina amri yo yote kutoka kwa Bwana, lakini mimi natoa ushauri kama mtu aliyemwaminifu kwa rehema ya Bwana.

26 Kwa sababu ya dhiki iliyopo, nadhani itakuwa vyema mki baki kama mlivyo. 27 Je, umeoa? Basi usitake talaka. Kama hujaoa usitafute mke. 28 Lakini kama ukioa, hujatenda dhambi; na kama bikira akiolewa hajatenda dhambi. Lakini wanaooa watakabil iana na matatizo mengi katika maisha haya, nami ningependa myaep uke kwa kubaki mlivyo.

29 Nikisema hivyo ndugu zangu, nina maana kwamba muda uliobaki ni mfupi. Tangu sasa waliooa waishi kama hawakuoa; 30 na wana oomboleza kama hawaoombolezi; wenye furaha kama hawana furaha; wanaonunua kama walivyonunua si mali yao; 31 na wanaoshughulika na vitu vya dunia hii, kama hawahusiki navyo. Kwa maana dunia hii kama tunavyoiona sasa inatoweka.

32 Ningependa msiwe na wasiwasi. Mwanamume ambaye hajaoa anajishughulisha na mambo ya Bwana, jinsi ya kumpendeza. 33 Lakini mwanamume aliyeoa anajishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi ya kumfurahisha mke wake. 34 Kwa sababu hiyo, ana vutwa huku na huko. Mwanamke asiyeolewa au msichana bikira anaj ishughulisha na kazi ya Bwana, jinsi ya kuwa mtakatifu kimwili na kiroho. Lakini mwanamke aliyeolewa anajishughulisha na mambo ya dunia, jinsi ya kumfurahisha mume wake. 35 Ninasema haya kwa faida yenu na sio kuwawekea vikwazo. Napenda muishi sawa na kumpa Bwana maisha yenu yote. 36 Kama mtu anafikiri kwamba mwenendo wake kwa mchumba wake si sawa, na hasa kama mchumba wake anaanza kuzeeka, na anaona anawajibika kumuoa, basi afanye anavyoona vyema; waoane, si dhambi. 37 Lakini kama mwanamume ameshaamua moyoni mwake kuto kuoa bila kulazimishwa na mtu; kama anaweza kujitawala kabisa, basi anafanya vyema kutokumuoa mchumba wake. 38 Kwa hiyo mwana mume anayeamua kumuoa mchumba wake anafanya vizuri, lakini yule anayeamua kutokumuoa anafanya vizuri zaidi.

39 Mwanamke aliyeolewa amefungwa kwa mume wake maadamu anaishi. Kama mumewe akifa, basi mwanamke huyo yuko huru kuolewa na mume mwingine ampendaye, ila iwe katika Bwana. 40 Lakini kwa upande wangu naona kuwa angekuwa na furaha zaidi akibaki alivyo.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica