M’Cheyne Bible Reading Plan
Yesu Afundisha Kuhusu Talaka
10 Yesu akaondoka mahali pale akavuka mto wa Yordani, akaenda sehemu ya Yudea. Umati wa watu ukamfuata tena na kama kawaida yake akawafundisha.
2 Baadhi ya Mafarisayo wakamjia wakitaka kumtega, wakamwul iza, “Ni halali mtu kumwacha mke wake?”
3 Yesu akawajibu, “Musa aliwaamuruje?” 4 Wakamjibu, “Musa aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
5 Yesu akawaambia, “Musa aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. 6 Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mume na mke. 7 Na kwa sababu hii mume atamwacha baba yake na mama yake na hao wawili, watakuwa mwili mmoja.’ 8 Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena bali mwili mmoja. 9 Basi, alichokiun ganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
10 Baadaye waliporudi nyumbani , wanafunzi wa Yesu walimwul iza kuhusu jambo hili.
11 Akawajibu, “Mtu ye yote anayempa mkewe talaka na kuoa mke mwingine, anazini kwa yule mke aliyempa talaka. 12 Na mwa namke anayempa mumewe talaka na kuolewa na mume mwingine, anazini pia.”
Yesu Anawabariki Watoto Wadogo
13 Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse lakini wanafunzi wake wakawakemea. 14 Yesu alipoona yaliyokuwa yakitokea alichukizwa, akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa watu kama hawa! 15 Ninawahakikishieni kwamba, mtu ye yote ambaye hataukubali Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.” 16 Akawakumbatia wale watoto wadogo, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.
Mtu Tajiri
17 Yesu alipoanza tena safari yake, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake akamwuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini niurithi Ufalme wa milele?”
18 Yesu akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna ali yemwema isipokuwa Mungu peke yake. 19 Unazifahamu amri ‘Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Usidanganye. Waheshimu baba yako na mama yako .”’
20 Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”
21 Yesu akamtazama kwa moyo wa upendo akamwambia, “Umepun gukiwa na kitu kimoja tu. Nenda ukauze vitu vyote ulivyo navyo uwape maskini fedha utakazopata, nawe utakuwa na utajiri mbin guni; kisha njoo, unifuate.”
22 Yule mtu aliposikia hayo, alisikitika sana, akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa tajiri sana.
23 Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa
Mungu!”
24 Wanafunzi wake wakashtushwa sana na maneno hayo. Lakini Yesu akasema tena, “Wanangu, ni vigumu sana kuingia katika Ufalme wa Mungu. 25 Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
26 Wanafunzi wake wakashangaa mno. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi anaweza kuokolewa?”
27 Yesu akawatazama akawaambia, “Kwa wanadamu haiwezekani, lakini kwa Mungu si hivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.” 28 Petro akaanza kumwambia, “Sisi tumeacha kila kitu tukakufu ata!”
29 Yesu akajibu, “Ninawaambieni hakika, hakuna mtu ye yote aliyeacha nyumba, kaka, dada, mama, baba, watoto au shamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya kuitangaza Habari Njema, 30 ambaye hatalipwa katika ulimwengu huu mara mia zaidi: nyumba, kaka, dada, mama, watoto, mashamba na mateso pia; na kupewa uzima wa milele katika ulimwengu ujao. 31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
Yesu Azungumzia Tena Kifo Chake
32 Walikuwa njiani kuelekea Yerusalemu na Yesu alikuwa ame tangulia. Wanafunzi wake walikuwa wamejawa na hofu, na watu wal iowafuata walikuwa wanaogopa. Yesu akawachukua tena wale wana funzi wake kumi na wawili kando akawaambia yatakayompata. 33 Akasema, “Tunakwenda Yerusalemu, na Mimi Mwana wa Adamu nitapelekwa kwa makuhani wakuu na walimu wa sheria; nao watanihu kumu adhabu ya kifo na kunikabidhi kwa mataifa. 34 Wao watanid hihaki na kunitemea mate na kunipiga na kuniua. Baada ya siku tatu, nitafufuka.”
Ombi La Yakobo Na Yohana
35 Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo wakamwendea Yesu wakamwambia, “Bwana, kuna jambo moja tungependa kukuomba.”
36 Akawauliza, “Mngependa niwafanyie jambo gani?”
37 Wakamjibu, “ Tunakuomba utakapoketi katika ufalme wako wa utukufu, uturuhusu tuketi pamoja nawe, mmoja wetu mkono wako wa kulia na mwingine mkono wako wa kushoto.”
38 Yesu akawaambia, “Hamjui mnaloliomba. Mko tayari kunywea kikombe cha mateso nitakachokunywa? Mnaweza kubatizwa ubatizo nitakaobatizwa?”
39 Wakamjibu, “ Tunaweza.” Yesu akawaambia, “Mtakunywa katika kikombe nitakachokunywa na kubatizwa ubatizo nitakaobati zwa. 40 Lakini kuhusu kuketi mkono wangu wa kulia au wa kushoto si juu yangu mimi kuwaruhusu. Mungu atatoa nafasi hizo kwa watu aliowaandalia.”
41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, waliwaka sirikia Yakobo na Yohana. 42 Yesu akawaita wanafunzi wake wote pamoja akawaambia, “Mnafahamu kwamba watu wanaotawala watu wa mataifa hutumia mabavu, na viongozi wa vyeo vya juu hupenda kuon yesha wana madaraka! 43 Lakini haipasi kuwa hivyo kati yenu. Badala yake, anayetaka kuwa mkuu kati yenu hana budi kuwa mtum ishi wenu, 44 na ye yote anayetaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa mtumishi wa wote. 45 Kwa maana hata mimi Mwana wa Adamu sikuja ili nitumikiwe, bali nilikuja ili niwe mtumishi na kutoa maisha yangu yawe fidia kwa ajili ya watu wengi.”
Yesu Amponya Kipofu Bartimayo
46 Wakafika Yeriko. Na Yesu alipokuwa akiondoka pamoja na Wanafunzi wake na umati wa watu, kipofu mmoja, jina lake Barti mayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando kando ya njia, akiomba.
47 Aliposikia kuwa Yesu wa Nazareti alikuwa akipita, akaanza kupiga kelele, “Yesu, Mwana wa Daudi, nionee huruma!”
48 Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya. Lakini yeye alipiga kelele zaidi, “Mwana wa Daudi, nionee huruma!”
49 Yesu akasimama akawaambia, “Mwiteni.” Wakamwita wakamwambia, “Changamka! Usimame, anakuita.”
50 Akatupa vazi lake kando, akaruka juu, akamwendea Yesu. 51 Yesu akamwuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona tena.” 52 Yesu akamwambia, “Nenda, imani yako imekuponya.” Wakati huo huo akaweza kuona, akamfuata Yesu njiani.
Kutokuamini Kwa Waisraeli
10 Ndugu zangu, shauku ya moyo wangu na maombi yangu kwa Mungu ni kwamba Waisraeli waokolewe. 2 Ninashuhudia wazi kwamba wao wanajuhudi kubwa ya kumtumikia Mungu, lakini juhudi yao haitokani na kuelewa. 3 Wameshindwa kuelewa haki itokayo kwa Mu ngu, na badala yake wakajaribu kujiwekea ya kwao; kwa hiyo hawa kutii haki ya Mungu. 4 Kwa maana Kristo amekamilisha sheria ili kila mtu mwenye imani ahesabiwe haki.
Wokovu Ni Kwa Wote
5 Musa anaandika kwamba mtu anayejaribu kutenda haki kwa msingi wa sheria ataishi kwa sheria. 6 Lakini haki itokanayo na imani husema hivi, “Usiseme nafsini mwako, ‘Ni nani atapaa mbi nguni?”’ yaani kumleta Kristo duniani, 7 au “‘Ni nani atashuka kuzimuni?”’yaani kumleta Kristo kutoka kwa wafu. 8 Bali inasema hivi, “Neno la Mungu liko karibu nawe; liko mdomoni mwako na moyoni mwako,” yaani, neno la imani tunayohubiri. 9 Kama ukikiri kwa kinywa chako kuwa Yesu ni Bwana na ukiamini moyoni mwako kuwa Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka. 10 Kwa maana mtu ana poamini moyoni mwake huhesabiwa haki, na anapokiri kwa kinywa chake, huokolewa. 11 Kama yasemavyo Maandiko, “Hakuna amwami niye ambaye ataaibika.” 12 Kwa maana hakuna tofauti kati ya wote naye huwabariki wote wamwitao. 13 Kwa maana, “Kila mtu atakayeliita Jina la Bwana, ataokoka.”
14 Lakini watu watamwitaje yeye ambaye hawajamwamini? Na watamwaminije yeye ambaye hawajawahi kumsikia? Na watamsikiaje kama mtu hakuwahubiria? 15 Na watu watahubirije kama hawaku tumwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri mno miguu ya hao wanaohubiri Habari Njema!”
16 Lakini si wote walioipokea Habari Njema. Kwa maana Isaya alisema:“Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?” 17 Basi, chanzo cha imani ni kusikia, na kusikia huja kwa kuhubiri neno la Kristo. 18 Lakini nauliza, hivi wao hawajasikia? Hakika wame sikia; kwa maana Maandiko yanasema: “Sauti yao imeenea duniani kote, na maneno yao yamefika miisho ya ulimwengu.” 19 Nauliza tena, je, Waisraeli hawakuelewa? Kwanza Musa anasema, “Nitawa fanya muone wivu kwa ajili ya wale ambao hawajawa taifa bado; nitawafanya mkasirike kwa ajili ya taifa la watu wasio elewa.” 20 Na Isaya anasema kwa ujasiri, “Wale ambao wali kuwa hawanitafuti, wamenipata. Nimejidhihirisha kwa wale ambao walikuwa hawaniulizii.” 21 Lakini kuhusu wana wa Israeli anasema: “Mchana kutwa nimewanyooshea mikono watu wakaidi na wasiotii.”
Copyright © 1989 by Biblica