Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

M’Cheyne Bible Reading Plan

The classic M'Cheyne plan--read the Old Testament, New Testament, and Psalms or Gospels every day.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: Gen for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Matayo 24

Dalili Za Siku Za Mwisho

24 Yesu aliondoka Hekaluni na alipokuwa akienda zake, wana funzi wakamwendea ili wakamwonyeshe majengo ya Hekalu. Lakini yeye akawaambia, “Mnayaona haya yote? Nawaambieni kweli, hakuna hata jiwe moja hapa litakalobaki juu ya jingine, yote yatatupwa chini.”

Yesu alipokuwa ameketi kwenye mlima wa Mizeituni wanafunzi wake walimwendea faraghani, wakamwuliza, “Tueleze, mambo haya yatatokea lini na ni dalili gani zitaonyesha kuja kwako na mwisho wa dunia?”

Yesu akawajibu, “Jihadharini, mtu asije akawadanganya. Kwa maana wengi watakuja kwa jina langu wakisema, ‘Mimi ndiye Kristo’ nao watawapotosha wengi. Mtasikia habari za vita na tetesi za vita, msitishike; kwa maana haya hayana budi kutokea; lakini mwisho utakuwa bado. Taifa kwa taifa na nchi kwa nchi zitapigana. Kutakuwa na njaa na tetemeko la ardhi sehemu mbalim bali. Haya yote yatakuwa kama mwanzo wa uchungu wa uzazi.

“Kisha mtasalitiwa, mtateswa na kuuawa na mtachukiwa na watu wa mataifa yote kwa ajili ya jina langu. 10 Wakati huo, wengi wataacha imani yao, watasalitiana na kuchukiana, 11 na watatokea manabii wengi wa uongo ambao watawapotosha watu. 12 Kwa sababu uovu utakuwa umeenea sana, upendo wa watu wengi utapoa. 13 Lakini mtu atakayesimama imara mpaka mwisho, ataoko lewa. 14 Na hii Habari Njema ya Ufalme itahubiriwa ulimwenguni pote, kama ushuhuda kwa mataifa yote. Ndipo mwisho utafika.

15 “Mtakapoona lile ‘Chukizo la Uharibifu’ linalozungumzwa na nabii Danieli limesimama mahali Patakatifu - msomaji na aelewe - 16 basi wale walioko Yudea wakimbilie milimani. 17 Aliyeko juu ya nyumba asishuke kuchukua vitu vyake ndani. 18 Aliyeko sham bani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake. 19 Ole wao wanawake watakaokuwa na mimba na watakaokuwa wakinyonyesha siku hizo! 20 Ombeni ili mtakapokuwa mnakimbia, isiwe ni kipindi cha baridi au siku ya sabato. 21 Kwa maana kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijawahi kutokea tangu mwanzo wa dunia mpaka sasa na ambayo haitatokea tena. 22 Kama siku hizo zisingepunguzwa, hakuna hata mtu mmoja ambaye angesalimika, lakini kwa ajili ya wale walioteu liwa na Mungu, siku hizo zitapunguzwa. 23 Wakati huo mtu aki waambia, ‘Tazama! Kristo yuko hapa!’ au ‘Kristo yule pale!’ msi sadiki. 24 Kwa maana watatokea makristo na manabii wa uongo na watafanya ishara za ajabu na miujiza mingi ili kuwadanganya, hata ikiwezekana, wateule wa Mungu. 25 Angalieni, nawatahadharisha mapema.

26 “Kwa hiyo wakiwaambia, ‘Yule kule nyikani,’ msitoke. Au wakisema, ‘Yuko chumbani 27 Kwa maana kama vile umeme unavyotokea mashariki na kuangaza mpaka magharibi, ndivyo itakavyokuwa kuja kwangu mimi Mwana wa Adamu. 28 Kwa maana po pote ulipo mzoga, ndipo wakusanyikapo tai.

29 “Mara baada ya dhiki ya wakati huo, jua litatiwa giza, mwezi hautatoa mwanga wake tena, na nyota zitaanguka kutoka mbin guni; nguvu za anga zitatikisika. 30 Ndipo itaonekana ishara ya Mwana wa Adamu angani na watu wote ulimwenguni wataomboleza. Nao wataniona mimi Mwana wa Adamu nikija juu ya mawingu ya angani, katika uwezo na utukufu mkuu. 31 Na nitawatuma malaika zangu kwa sauti kuu ya tarumbeta na watawakusanya wateule wangu kutoka pande zote nne za dunia, kutoka mwisho mmoja wa mbingu hadi mwisho mwingine.

32 “Jifunzeni kutoka kwa mti wa mtini. Matawi yake yana poanza kuwa laini na majani kuchipua, mnafahamu kwamba kiangazi kimekaribia. 33 Basi, pia mkiona dalili hizi, fahamuni kwamba amekaribia kurudi, na yu karibu na mlango. 34 Nawaambieni kweli, hakika kizazi hiki hakitapita kabla mambo haya hayajatokea. 35 Mbingu na dunia zitatoweka, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”

Hakuna Ajuaye Siku Wala Saa

36 “Hakuna ajuaye siku wala saa, hata malaika mbinguni wala Mwana, isipokuwa Baba peke yake. 37 Kama ilivyokuwa wakati wa Nuhu, ndivyo itakavyokuwa atakaporudi Mwana wa Adamu. 38 Kwa maana siku zile kabla ya gharika, watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka siku ile Nuhu alipoingia kwenye safina. 39 Nao hawakujua ni nini kitatokea mpaka gharika ilipokuja ika wakumba wote. Hivyo ndivyo itakavyokuwa nitakapokuja mimi Mwana wa Adamu.

40 “Watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa, mwingine ataachwa. 41 Wanawake wawili watakuwa wanatwanga; mmoja atachukuliwa, mwingine ataachwa.

42 “Kwa hiyo kesheni, kwa maana hamjui ni siku gani ataka pokuja Bwana wenu.

43 “Lakini fahamuni kwamba, kama mwenye nyumba angalifahamu ni saa ngapi za usiku ambapo mwizi atakuja, angalikaa macho asiache nyumba yake ivunjwe. 44 Kwa hiyo ninyi pia lazima muwe tayari kwa maana mimi Mwana wa Adamu nitakuja saa ambayo hamnita zamii.”

Mfano Wa Mtumishi Mwaminifu

45 “Basi, ni nani mtumishi mwaminifu ambaye bwana wake amemweka awe msimamizi wa watumishi wengine nyumbani kwake, awape posho yao kwa wakati wake? 46 Heri mtumishi ambaye atakapokuja bwana wake atamkuta anafanya hivyo. 47 Nawaambieni kweli, atam fanya mtumishi huyo asimamie mali yake yote.

48 “Lakini kama mtumishi huyo ni mwovu atasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu hatarudi kwa muda mrefu,’ 49 na ataanza kuwapiga watumishi wenzake na kula na kunywa na walevi. 50 Bwana wake atakuja wakati ambapo mtumishi huyo hamtazamii na saa ambayo haijui. 51 Ndipo atamwadhibu huyo mtumishi na kumweka katika kundi la wanafiki; huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.”

Error: Book name not found: Esth for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Matendo Ya Mitume 24

Mashtaka Ya Wayahudi Juu Ya Paulo

24 Baada ya siku tano, Kuhani Mkuu Anania akafika pamoja na baadhi ya wazee na wakili mmoja aitwaye Tertulo. Wakatoa mashtaka yao juu ya Paulo mbele ya Gavana. Na Paulo alipoitwa, Tertulo akaanza kutoa mashtaka akasema, “Mtukufu Feliksi, kutokana na uongozi wako wa busara tumekuwa na amani ya kudumu na tunatambua ya kuwa mabadiliko mengi muhimu yaliyotokea katika taifa letu yameletwa na uwezo wako wa kuona mbele. Wakati wote na kila mahali tunapokea mambo haya yote kwa shukrani za dhati. Lakini nisije nikakuchosha, nakuomba kwa hisani yako utusikilize kwa muda mfupi. Tumemwona mtu huyu kuwa ni mfanya fujo ambaye ana chochea maasi kati ya Wayahudi dunia nzima. Yeye ni kiongozi wa dhehebu la Wanazareti. Tena alijaribu kulichafua Hekalu letu lakini tulimkamata [tukataka kumhukumu kwa mujibu wa sheria zetu, lakini jemadari Lisia alikuja akamchukua kutoka kwetu kwa kutu mia nguvu akaamuru wanaomshtaki walete mashtaka yao mbele yako]. Wewe mwenyewe ukimwuliza maswali utathibitisha ukweli wa mashtaka yote tunayoleta mbele yako kumhusu yeye.” Wayahudi wakamwunga mkono wakithibitisha kwamba mashtaka yote yalikuwa ya kweli.

Paulo Ajitetea Mbele Ya Feliksi

10 Gavana Feliksi alipomruhusu Paulo ajitetee, yeye alisema, “Najua kwamba wewe umekuwa hakimu katika taifa hili kwa miaka mingi kwa hiyo natoa utetezi wangu bila wasi wasi. 11 Unaweza kuhakikisha kwa urahisi kuwa hazijapita zaidi ya siku kumi na mbili tangu nilipokwenda Yerusalemu kuabudu. 12 Hawa wanaonish taki hawakunikuta nikibishana na mtu ye yote au nikianzisha fujo katika Hekalu au katika sinagogi au mahali pengine po pote mjini. 13 Wala hawawezi kabisa kuthibitisha mambo haya wanayon ishtaki. 14 Lakini nakiri mbele yako kuwa mimi namwabudu Mungu wa baba zetu kwa kufuata ile ‘Njia’ ambayo wao wanaiita dhehebu. Ninaamini kila kitu kilichoandikwa katika Sheria ya Musa na Mana bii 15 na ninalo tumaini kwa Mungu ambalo hata na wao wanaliku bali, kwamba kutakuwa na ufufuo wa wote, walio na haki na wasio na haki. 16 Kwa hiyo ninafanya kila jitihada kuishi nikiwa na dhamiri safi mbele za Mungu na mbele za wanadamu. 17 Basi, baada ya kuwa nje ya Yerusalemu kwa miaka kadhaa nilikuja mjini kuwale tea watu wa taifa langu sadaka kwa ajili ya maskini na kutoa dha bihu. 18 Nilikuwa nimeshatakaswa waliponikuta Hekaluni nikifanya mambo haya, na hapakuwa na umati wa watu wala fujo yo yote. 19 Lakini kulikuwa na Wayahudi kutoka Asia, nadhani nao walista hili wawepo hapa mbele yako ili watoe mashtaka yao kama wanalo lo lote la kunishtaki. 20 La sivyo, watu hawa waseme ni kosa gani walilogundua nimefanya niliposhtakiwa mbele ya Baraza, 21 isipo kuwa lile jambo nililotangaza wazi wazi nilipojitetea mbele yao, kwamba, ‘Mimi nimeshtakiwa mbele yenu leo kuhusu ufufuo wa wafu.’

22 Ndipo Feliksi ambaye alikuwa anafahamu vizuri habari za Njia, akaamua kuahirishwa kwa kesi, akasema, “Mara jemadari Lisia atakapofika nitatoa hukumu yangu juu ya kesi hii.” 23 Akaamuru askari amweke Paulo kizuizini chini ya ulinzi lakini awe na uhuru kiasi, na marafiki zake wasizuiwe kumhudumia. 24 Baada ya siku chache Feliksi akaja na mkewe Drusila ambaye alikuwa Myahudi. Akatuma Paulo aitwe, wakamsikiliza akizungumza juu ya kumwamini Kristo Yesu. 25 Na Paulo alipokuwa akiwaeleza juu ya kuwa na kiasi na juu ya hukumu ya mwisho, Feliksi aliin giwa na hofu akasema, “Tafadhali sasa nenda, nitakuita tena nikipata nafasi.” 26 Wakati huo huo Feliksi alitazamia kwamba Paulo angempatia hongo, kwa hiyo akawa anamwita mara kwa mara kuzungumza naye. 27 Lakini baada ya miaka miwili kupita, Porkio Festo akachukua nafasi ya Feliksi kama Gavana; na kwa sababu Feliksi alitaka kujipendekeza kwa Wayahudi, akamwacha Paulo gere zani.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica