Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

M’Cheyne Bible Reading Plan

The classic M'Cheyne plan--read the Old Testament, New Testament, and Psalms or Gospels every day.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: Gen for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Matayo 14

Yohana Mbatizaji Akatwa Kichwa

14 Wakati huo, mfalme Herode alisikia habari za Yesu; akawaam bia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji, amefufuka kutoka kwa wafu; ndio sababu nguvu za kutenda miujiza zinafanya kazi ndani yake.”

Herode alikuwa amemkamata Yohana akamfunga na kumweka gere zani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, kaka yake. Kisa che nyewe ni kwamba Yohana alikuwa amemwambia Herode kuwa, “Si halali kwako kumwoa huyo mwanamke.” Herode alitaka sana kumwua Yohana lakini akaogopa watu kwa maana walimtambua kuwa ni nabii. Lakini siku ya kusherehekea sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, binti ya Herodia alicheza mbele ya watu walioalikwa akamfurahisha sana Herode. Naye akaahidi kwa kiapo kumpa huyo binti lo lote atakaloomba. Kwa kushawishiwa na mama yake, huyo binti akasema, “Nipatie kichwa cha Yohana Mbatizaji kwenye sinia.” Mfalme akajuta; lakini kwa ajili ya kile kiapo alichoapa mbele ya wageni, aliamuru kwamba ombi lake litekelezwe. 10 Akaagiza Yohana Mbatizaji akatwe kichwa mle gerezani, 11 na kichwa chake kikaletwa kwenye sinia, akapewa yule binti, naye akampelekea mama yake.

12 Wanafunzi wa Yohana wakaja, wakauchukua mwili wake wakau zika. Kisha wakaenda, wakamwambia Yesu.

Yesu Alisha Zaidi Ya Watu Elfu Tano

13 Yesu aliposikia haya, aliondoka kwa mashua akaenda mahali pasipo na watu ili awe peke yake. Lakini watu wal ipata habari, wakamfuata kwa miguu kupitia nchi kavu, kutoka mij ini. 14 Yesu alipofika kando ya bahari aliona umati mkubwa wa watu, akawahurumia na akawaponya wagonjwa wao.

15 Ilipofika jioni, wanafunzi wake walimfuata wakamwambia, “Mahali hapa ni nyikani, na siku imekwisha. Waage watu waondoke ili wakajinunulie chakula vijijini.” 16 Yesu akasema, “Hakuna sababu ya wao kuondoka. Ninyi wapeni chakula.” 17 Wakamjibu, “Hapa tuna mikate mitano na samaki wawili tu.” 18 Akawaambia, “Leteni hapa.” 19 Akaagiza wale watu wakae chini kwenye nyasi. Akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akainua macho yake akatazama mbinguni, akaibariki. Akaimega ile mikate akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu. 20 Wote wakala, wakatosheka. Na wanafunzi wake wakakusanya vipande vipande vilivyosalia, waka jaza vikapu kumi na viwili. 21 Idadi ya watu waliokula, bila kuhesabu wanawake na watoto, ilikuwa kama wanaume elfu tano.

Yesu Atembea Juu Ya Maji

22 Baadaye Yesu akawaambia wanafunzi wake watangulie kwe nye mashua waende ng’ambo ya pili ya ziwa, wakati yeye anawaaga wale watu. 23 Baada ya kuwaaga, akaenda mlimani peke yake kuomba. Jioni ilipofika, Yesu alikuwa hapo peke yake. 24 Wakati huo ile mashua ilikwisha fika mbali, ikisukwa sukwa na mawimbi kwa sababu upepo ulikuwa mkali.

25 Ilipokaribia alfajiri, Yesu akawaendea wanafunzi wake akiwa anatembea juu ya maji. 26 Lakini wanafunzi wake walipom wona akitembea juu ya maji, waliingiwa na hofu kuu. Wakasema, “Ni mzimu.” Wakapiga mayowe kwa hofu. 27 Lakini mara moja Yesu akasema nao, akawaambia, “Jipeni moyo. Ni mimi; msiogope.”

28 Petro akamjibu, “Bwana, kama ni wewe, niambie nije kwako nikitembea juu ya maji.” 29 Yesu akamwambia, “Njoo.” Basi Petro akatoka katika mashua, akatembea juu ya maji akimfuata Yesu. 30 Lakini alipoona upepo mkali aliingiwa na hofu, akaanza kuzama, huku akipiga kelele, “Bwana, niokoe!”

31 Mara Yesu akanyoosha mkono wake, akamshika, akamwambia, “Wewe mwenye imani haba, kwa nini ulikuwa na shaka?” 32 Na walipoingia katika mashua, upepo ukakoma. 33 Wote waliokuwamo katika mashua wakamwabudu wakisema, “Hakika, wewe ni Mwana wa

Yesu Awaponya Wagonjwa Genesareti

34 Walipokwisha kuvuka, wakafika Genesareti. 35 Watu wa eneo lile walipomtambua Yesu, walipeleka habari sehemu zote za jirani na watu wakawaleta wagonjwa wote kwake 36 wakamsihi awaru husu wagonjwa waguse tu pindo la vazi lake. Na wote waliomgusa, waliponywa.

Error: Book name not found: Neh for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Matendo Ya Mitume 14

Mahubiri ya Injili huko Ikonio

14 Basi huko Ikonio Paulo na Barnaba waliingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi. Wakahubiri kwa uwezo mkuu na umati mkubwa wa watu wakaamini, Wayahudi pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini wale Wayahudi ambao hawakupokea neno la Mungu, waliwa chochea watu wa mataifa dhidi ya wale walioamini. Paulo na Bar naba wakakaa huko kwa muda mrefu wakifundisha kwa ujasiri juu ya Bwana, ambaye alithibitisha kuwa mahubiri yao yalikuwa ni neno la neema yake; akawapa uwezo wa kutenda ishara na maajabu. Hata hivyo watu wa mji ule waligawanyika. Wengine wakaungana na wale Wayahudi na wengine wakawa upande wa mitume. Watu wa mataifa na Wayahudi walijiunga na baadhi ya viongozi wakafanya mpango wa kuwasumbua mitume na kisha kuwapiga mawe. Lakini wao walipopata habari hizi walitoroka wakakimbilia Listra na Derbe, miji ya wilaya ya Likaonia, na sehemu zilizopakana nayo. Huko waliende lea kuhubiri Habari Njema.

Kiwete Aponywa Huko Listra

Katika mji wa Listra, alikuwepo kiwete amekaa, ambaye ali kuwa amelemaa miguu yote miwili tangu alipozaliwa, na hakuwahi kutembea kamwe. Alimsikiliza Paulo alipokuwa akihubiri, na Paulo alipomtazama aliona kuwa anayo imani ya kuponywa. 10 Kwa hiyo Paulo akasema kwa sauti, “Simama kwa miguu yako!” Mara yule mtu akaruka juu akaanza kutembea! 11 Wale watu walipoona maajabu aliyofanya Paulo, wakapiga kelele kwa lugha yao, wakasema, “Miungu imetushukia katika umbo la binadamu!” 12 Wakamwita Barnaba Zeu na Paulo wakamwita Herme kwa kuwa ndiye alikuwa msemaji mkuu. 13 Kuhani mkuu wa Zeu ambaye hekalu lake lilikuwa mbele ya mji, akaleta mafahali na mashada ya maua aki taka kuwatolea sadaka penye lango la mji pamoja na ule umati wa watu. 14 Lakini Paulo na Barnaba waliposikia na kuona mambo haya waliyotaka kufanya, walirarua nguo zao, wakawakimbilia wale watu, wakisema, 15 ‘ ‘Kwa nini mnafanya mambo haya? Sisi ni binadamu tu, kama ninyi! Tumekuja kuwatangazia Habari Njema; mziache hizi ibada zisizo na maana na mumgeukie Mungu aliye hai ambaye aliumba mbingu na nchi na bahari, na vyote vilivyoko. 16 Wakati wa vizazi vilivyopita aliwaachia watu waishi walivyotaka. 17 Hata hivyo hakuacha kuwaonyesha watu uwepo wake. Kwa maana aliwatendea mema akawaletea mvua kutoka mbinguni na mazao kwa majira yake, akawatosheleza kwa vyakula na raha.” 18 Hata pamoja na maneno yote haya haikuwa rahisi kuwazuia wale watu waache kuwatolea sadaka zao.

19 Wakaja watu kutoka Antiokia na Ikonio wakawashawishi wale watu, wakampiga Paulo kwa mawe, wakamkokota hadi nje ya mji, wakidhani amekufa. 20 Lakini waamini walipokusanyika kumzunguka, aliamka, akarudi nao mjini. Kesho yake akaondoka na Barnaba wakaenda mpaka Derbe.

Paulo Na Barnaba Warudi Antiokia

21 Walipokwisha hubiri Habari Njema katika mji ule na watu wengi wakaamini wakawa wanafunzi, walirudi Listra na Ikonio na Antiokia. 22 Huko waliwatia nguvu wanafunzi na kuwashauri waendelee kukua katika imani. Wakawaonya wakisema, “Tunalazimika kuingia katika Ufalme wa Mungu kwa kupitia katika mateso mengi.” 23 Na baada ya kuwachagulia wazee viongozi katika kila kanisa, wakawakabidhi kwa Bwana waliyemwamini kwa maombi na kufunga. 24 Basi wakapitia Pisidia wakafika Pamfilia. 25 Na baada ya kufundisha neno la Mungu huko Perga, walikwenda upande wa kusini hadi Atalia. 26 Kutoka huko wakasafiri kwa mashua mpaka Anti okia, ambako walikuwa wameombewa neema ya Mungu kwa kazi ambayo walikuwa wameikamilisha. 27 Walipowasili Antiokia waliwakusanya waamini pamoja wakawaeleza yale yote ambayo Mungu alikuwa amewa tendea, na jinsi Mungu alivyotoa nafasi ya imani kwa watu wasio Wayahudi. 28 Wakakaa huko na wale wanafunzi kwa muda mrefu.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica