Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

M’Cheyne Bible Reading Plan

The classic M'Cheyne plan--read the Old Testament, New Testament, and Psalms or Gospels every day.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: Gen for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Matayo 11

Yohana Atuma Wanafunzi Wake Kwa Yesu

11 Yesu alipomaliza kutoa maagizo yake kwa wale wanafunzi wake kumi na wawili, aliondoka pale akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao. Basi Yohana Mbatizaji aliposikia akiwa gere zani mambo ambayo Yesu alikuwa akifanya, aliwatuma wanafunzi wake wakamwulize, “Wewe ni yule anayekuja, au tumngojee mwin gine?” Yesu akawajibu, “Nendeni mkamweleze Yohana yale mnayo sikia na kuona: vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na maskini wanahubiriwa Habari Njema. Amebarikiwa mtu ambaye hapotezi imani yake kwangu.”

Wale wanafunzi wa Yohana walipoondoka, Yesu akaanza kuwaam bia ule umati wa watu kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mli pokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Unyasi ukitikiswa na upepo? Kama sivyo, mlikwenda huko kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi maridadi? Lakini wanaovaa nguo maridadi wanakaa katika majumba ya wafalme. Basi kwa nini mlikwenda huko? Kumwona nabii? Naam, nawaambieni yeye ni zaidi ya nabii. 10 Huyo ndiye ambaye anaelezwa katika Maandiko kwamba: ‘ Angalia namtuma mjumbe mbele yako, ambaye atakuandalia njia.’ 11 Nawaambieni kweli kwamba kati ya watu wote waliozaliwa na wanawake, hajatokea mtu aliye mkuu zaidi ya Yohana Mbatizaji. Lakini hata hivyo aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa mbinguni, ni mkuu kuliko Yohana. 12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hadi sasa, Ufalme wa Mungu umekuwa ukishambuliwa vikali; na watu wenye jeuri wanajaribu kuuteka kwa nguvu. 13 Kwa maana manabii wote na sheria walita biri mpaka wakati wa Yohana. 14 Na kama mko tayari kusadiki uta biri wao, basi Yohana ndiye Eliya ambaye kuja kwake kulitabiriwa. 15 Mwenye nia ya kusikia na asikie.

16 “Kizazi hiki nikilinganishe na nini?” Kinafanana na waliokaa masokoni wakiwaita wenzao na kuwaambia, 17 ‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza; tuliwaimbia nyimbo za msiba, lakini hamkuomboleza.’ 18 Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja na akawa hali wala hanywi nao wanasema, ‘Amepagawa na pepo’. 19 Mimi mwana wa Adamu nimekuja nikila na kunywa, nao wanasema, ‘Mta zameni mlafi na mlevi; rafiki wa watoza kodi na wenye dhambi!’ Lakini hekima huthibitishwa kwa matendo yake.”

Ole Kwa Korazini Na Bethsaida

20 Yesu akaanza kuikemea miji ambamo alifanya matendo mengi ya ajabu kwa maana watu wake hawakutubu. 21 “Ole wenu watu wa Korazini! Ole wenu watu wa Bethsaida! Kwa maana kama matendo makuu yaliyofanyika kwenye miji yenu yangelifanyika Tiro na Sidoni, watu wa huko wangelikuwa wametubu tangu zamani na kuvaa magunia na kujipaka majivu, kudhihirisha kujuta kwao. 22 Lakini nawaambia, siku ile ya hukumu itakuwa nafuu kwa Tiro na Sidoni kuliko itakavyokuwa kwenu. 23 Na ninyi watu wa Kapernaumu, mnadhani mtainuliwa hadi juu mbinguni? Mtashushwa hadi kuzimuni. Kwa kuwa kama mambo makuu yaliyofanyika kwenu yangalifanyika huko Sodoma, mji huo ungalikuwapo hadi leo. 24 Lakini nawaam bieni hakika, siku ile ya hukumu itakuwa nafuu kwa Sodoma kuliko itakavyokuwa kwenu.”

Hakuna Amjuaye Baba Ila Mwana

25 Wakati huo Yesu alisema, “Ninakushukuru Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, na ukawafunulia watoto wachanga. 26 Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyokupendeza. 27 Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu: na hakuna mtu amjuaye Mwana ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana, na mtu ye yote ambaye Mwana anapenda kumdhihirisha Baba kwake.”

Yesu Awaita Waliolemewa Na Mizigo

28 “Njooni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. 29 Jifungeni nira yangu; jifunzeni kutoka kwangu; kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu. 30 Kwa maana nira yangu ni rahisi, na mzigo wangu ni mwepesi.”

Error: Book name not found: Neh for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Matendo Ya Mitume 11

Petro Aeleza Alivyotumwa Kwa Mataifa

11 Baadaye mitume na waamini wa sehemu zote za Yudea wakapata habari kwamba watu wasiokuwa Wayahudi nao wamepokea neno la Mungu. Kwa hiyo Petro alipokwenda Yerusalemu, wale waliokuwa wakishikilia sheria ya tohara walimshutumu wakasema, “Kwa nini ulikwenda kwa watu wasiotahiriwa na kula pamoja nao?” Ndipo Petro akaanza kuwaeleza mambo yote yalivyotokea akasema, “Nil ikuwa nikiomba katika mji wa Jopa, nikaona katika ndoto kitu kama shuka kubwa ikishushwa chini kwa ncha zake nne, kutoka mbinguni, nayo ikanifikia. Nilipotazama kwa makini nikaona wanyama wa kila aina, wanyama wa mwituni, wanyama watambaao na ndege wa angani. Nikasikia sauti ikiniambia, ‘Amka Petro, chinja, ule!’ Nami nikasema, ‘La, Bwana! Sijawahi kula kitu cho chote kili chokatazwa na sheria zetu.’ Lakini ile sauti kutoka mbinguni ikasema kwa mara ya pili, ‘Usiite kitu cho chote alichokitakasa Mungu kuwa ni uchafu.’ 10 Jambo hili lilitokea mara tatu ndipo vyote vikachukuliwa tena mpaka mbinguni. 11 Wakati huo huo watu watatu waliokuwa wametumwa kutoka Kaisaria wakawasili katika nyumba niliyokuwa nikikaa. 12 Roho akaniambia niende nao bila kusita. Nikaenda nao nikisindikizwa na hawa ndugu sita, tukaingia katika nyumba ya Kornelio. 13 Kornelio akatuambia jinsi malaika alivyomtokea akamwambia, ‘Tuma watu Jopa wakamwite Simoni aitwaye Petro. 14 Yeye anao ujumbe utakaokuokoa wewe na wote walio nyum bani mwako.’ 15 Nami nilipokuwa nikisema nao, Roho Mtakatifu akashuka juu yao kama alivyotushukia sisi mwanzoni. 16 Nami nikakumbuka jinsi Bwana alivyosema, ‘Yohana alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.’ 17 Basi kwa kuwa Mungu ndiye aliyewapa hawa watu karama ile ile aliyotupa sisi tulipomwamini Bwana Yesu, mimi ni nani hata nimpinge Mungu?” 18 Nao waliposikia maneno haya hawakuwa na la kusema. Wakamsifu Mungu, wakasema, “Mungu amewapa watu wa mataifa nafasi ya kutubu na kupokea uzima wa milele.’ ’

Kanisa Laenea Antiokia

19 Wale waamini waliotawanyika kutoka Yerusalemu wakati wa mateso yaliyotokana na kifo cha Stefano, walisafiri hadi Foinike na Kipro na Antiokia. Wakawa wakihubiri Habari Njema kwa Wayahudi peke yake. 20 Lakini baadhi yao walikwenda Antiokia wakitokea Kipro na Kirene. Wakawaambia Wagiriki Habari Njema za Bwana Yesu. 21 Roho wa Bwana alikuwa pamoja nao kwa hiyo watu wengi wakaamini na kumgeukia Bwana. 22 Habari hizi zilipowafikia vion gozi wa kanisa huko Yerusalemu, walimtuma Barnaba aende Antiokia. 23 Alipofika akaona jinsi Mungu alivyokuwa akiwabariki watu kwa neema yake, alifurahi sana akawatia moyo waendelee kwa juhudi kuwa waaminifu kwa Bwana. 24 Barnaba alikuwa mtu mwema aliyejawa Roho Mtakatifu, mwenye imani kuu; na watu wengi waliongoka wakam wamini Bwana. 25 Kisha Barnaba akasafiri kwenda Tarso kumtafuta Sauli. 26 Alipompata akaja naye mpaka Antiokia. Na wote wawili wakakaa huko kwa mwaka mzima, wakiwafundisha wengi walioamini katika kanisa la Antiokia. Hapo Antiokia ndipo waamini waliitwa ‘Wakristo’ kwa mara ya kwanza.

27 Wakati huu manabii walitoka Yerusalemu wakaenda Antiokia. 28 Na mmoja wao, jina lake Agabo, akasimama katika mkutano aka tabiri kwa uweza wa Roho kwamba pangetokea njaa kubwa dunia nzima. Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa mtawala. 29 Waamini wakaamua kwamba kila mtu, kulingana na uwezo alio nao, atoe msaada upelekwe kwa ndugu waliokuwa wanaishi Yudea. 30 Wakafanya hivyo, na misaada ikapelekwa na Barnaba na Sauli kwa wazee wa kanisa.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica