Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

M’Cheyne Bible Reading Plan

The classic M'Cheyne plan--read the Old Testament, New Testament, and Psalms or Gospels every day.
Duration: 365 days
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Version
Error: Book name not found: Gen for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Matayo 1

Ukoo Wa Yesu Kristo

Kumbukumbu ya vizazi vya ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi na wa Abrahamu: Abrahamu alikuwa baba yake Isaka; Isaka alikuwa baba yake Yakobo; na Yakobo alikuwa baba yake Yuda na ndugu zake. Yuda alikuwa baba yake Peresi na Zera ambao mama yao alikuwa Tamari; Peresi alikuwa baba yake Esroni; Esroni alikuwa baba yake Aramu; Aramu alikuwa baba yake Aminadabu; Aminadabu alikuwa baba yake Nashoni; Nashoni alikuwa baba yake Salmoni; Salmoni alikuwa baba yake Boazi na mama yake Salmoni alikuwa Rahabu. Boazi alikuwa baba yake Obedi, ambaye mama yake alikuwa Ruti; Obedi alikuwa baba yake Yese; Yese alikuwa baba yake Daudi ambaye alikuwa mfalme. Daudi alikuwa baba yake Solomoni ambaye mama yake ni yule aliyekuwa mke wa Uria; Solomoni alikuwa baba yake Rehoboamu; Rehoboamu alikuwa baba yake Abiya; Abiya alikuwa baba yake Asa; Asa alikuwa baba yake Yehoshafati; Yehoshafati alikuwa baba yake Yoramu; Yoramu alikuwa baba yake Uzia; Uzia alikuwa baba yake Yothamu; Yothamu alikuwa baba yake Ahazi; Ahazi alikuwa baba yake Hezekia; 10 Hezekia alikuwa baba yake Manase; Manase alikuwa baba yake Amoni; Amoni alikuwa baba yake Yosia; 11 wakati wa uhamisho wa Babiloni, Yosia alimzaa Yekonia na ndugu zake; 12 na baada ya uhamisho wa Babiloni Yekonia alimzaa Shealtieli; Shealtieli alikuwa baba yake Zerubabeli; 13 Zeru babeli alikuwa baba yake Abihudi; Abihudi alikuwa baba yake Eliakimu ; Eliakimu alikuwa baba yake Azori; 14 Azori alikuwa baba yake Zadoki; Zadoki alikuwa baba yake Akimu; Akimu alikuwa baba yake Eliudi; 15 Eliudi alikuwa baba yake Elieza; Elieza alikuwa baba yake Matani; Matani alikuwa baba yake Yakobo; 16 Yakobo alikuwa baba yake Yosefu ambaye alikuwa mumewe Mar ia, aliyemzaa Yesu anayeitwa Kristo. 17 Basi, kulikuwepo vizazi kumi na vinne tangu Abrahamu mpaka wakati wa mfalme Daudi; na vizazi kumi na vinne tangu mfalme Daudi hadi wakati wa uhamisho wa Babiloni na vizazi kumi na vinne tangu wakati wa uhamisho hadi Kristo.

Kuzaliwa Kwa Yesu Kristo

18 Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi: Maria mama yake, alikuwa ameposwa na Yosefu. Lakini kabla ya ndoa yao, Mar ia akiwa bado bikira, alipata mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu. 19 Kwa kuwa Yosefu alikuwa mtu mwema hakutaka kumwaibisha mchumba wake Maria hadharani. Kwa hiyo aliamua kuvunja uchumba wao kwa siri. 20 Lakini alipokuwa bado anawaza juu ya jambo hili, malaika wa Bwana akamtokea katika ndoto akasema, “Yosefu mwana wa Daudi, usisite kumwoa Maria mchumba wako kwa maana mimba aliyo nayo ameipata kwa uweza wa Roho Mtakatifu. 21 Naye atamzaa mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yesu; kwa maana yeye ndiye atakayewaokoa watu wake kutoka katika dhambi zao.”

22 Hayo yote yalitokea ili kutimiza maneno ya Mungu yaliyos emwa na nabii wake: 23 “Tazama bikira atachukua mimba, naye atamzaa mtoto wa kiume nao watamwita Imanueli,” maana yake, “Mungu pamoja nasi”. 24 Yosefu alipoamka usingizini, alifanya kama alivyoagizwa na malaika wa Bwana; akamchukua mkewe Maria nyumbani kwake, 25 lakini hawakukaribiana mpaka Maria alipoji fungua mtoto wa kiume. Yosefu akamwita jina lake Yesu.

Error: Book name not found: Ezra for the version: Neno: Bibilia Takatifu
Matendo Ya Mitume 1

Mpendwa Teofilo, Katika Kitabu changu cha kwanza nilikuan dikia kuhusu mambo yote aliyotenda Yesu, hadi wakati alipopaa mbinguni. Kabla hajachukuliwa juu, aliwapa mitume wake maagizo kwa njia ya Roho Mtakatifu. Alijionyesha kwao akiwa hai muda wa siku arobaini baada ya kufufuka kwake. Akawahakikishia kwa njia nyingi ya kuwa ni yeye na akaongea nao kuhusu Ufalme wa Mungu.

Wakati mmoja alipokuwa nao, aliwapa amri hii, “Msiondoke Yerusalemu, mpaka mtakapopokea ahadi aliyotoa Baba, ambayo mmeni sikia nikiizungumzia. Kwa maana Yohana aliwabatiza kwa maji lakini baada ya siku chache mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”

Yesu Apaa Mbinguni

Mitume walipokutana na Yesu walimwuliza, “Bwana, wakati huu ndipo utawarudishia Waisraeli ufalme ?”

Yesu akawaambia, “Si juu yenu kufahamu wakati na majira ambayo yamewekwa na Baba kwa mamlaka yake. Lakini mtapokea nguvu akishawajilia Roho Mtakatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu na Yudea yote na Samaria, hadi mwisho wa dunia.”

Baada ya kusema haya, wakiwa wanatazama, alichukuliwa juu, na wingu likamficha wasimwone tena. 10 Walikuwa bado wakikaza macho yao mawinguni alipokuwa akienda, ndipo ghafla, wanaume wawili waliovaa mavazi meupe walisimama karibu nao, 11 wakasema, “Ninyi watu wa Galilaya, mbona mnasimama hapa mkitazama mbin guni? Yesu huyu huyu aliyechukuliwa mbinguni atarudi tena kama mlivyomwona akienda mbinguni.”

12 Ndipo mitume waliporudi Yerusalemu kutoka mlima wa Mizeituni ulioko umbali wa kama kilometa moja kutoka mjini. 13 Walipoingia mjini Yerusalemu walikwenda katika chumba cha ghorofani walipokuwa wakiishi: Petro, Yohana, Yakobo na Andrea, Filipo, Tomaso, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo na Simoni aliyeitwa Mzalendo, na Yuda mwana wa Yakobo.

14 Hawa wote waliamua kwa kauli moja kutumia muda wao wote kusali, wakiwa pamoja na wale akina mama, Mariamu mama yake Yesu pamoja na ndugu zake.

15 Ilikuwa ni katika siku hizo ambapo Petro alisimama kati ya waamini wote, watu wapatao mia moja na ishirini, 16 akasema, “Ndugu zangu, ilibidi Maandiko ambayo Roho Mtakatifu alitabiri kupitia kwa Daudi kumhusu Yuda aliyewaongoza wale waliomkamata Yesu, yatimie. 17 Yuda alikuwa mmoja wetu, kwa maana na yeye alichaguliwa ashiriki katika huduma hii.” 18 Yuda alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na uovu wake na akiwa huko shambani alianguka kifudifudi akapasuka na matumbo yote yakatoka nje. 19 Kila mkazi wa Yerusalemu alisikia habari hizi, kwa hiyo wakapaita mahali hapo kwa lugha yao, Akeldama, yaani ‘shamba la Damu.’ 20 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Zab uri, ‘Mahali pake pasiwe na kitu wala asiwepo mtu atakayekaa hapo,’ na, ‘Nafasi yake ichukuliwe na mwingine.”’

Mathiya Achaguliwa

21 “Kwa hiyo inatubidi tumchague mtu mwingine kati ya wale ambao wamekuwa pamoja nasi 22 tangu wakati Yesu alipobatizwa na Yohana mpaka siku aliyochukuliwa mbinguni. Mmoja wao inabidi aun gane nasi kama shahidi wa ufufuo wa Yesu.”

23 Wakapendekeza majina ya watu wawili. Yusufu, aitwaye Barsaba, pia alijulikana kama Yusto, na Mathiya. 24 Wakaomba, “Bwana ujuaye mioyo ya watu wote, tunakuomba utuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua 25 achukue nafasi ya huduma na utume ambayo Yuda aliiacha akaenda panapomstahili.”

26 Kisha wakapiga kura na Mathiya akachaguliwa. Basi akain gizwa katika kundi la wale mitume kumi na mmoja.

Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Copyright © 1989 by Biblica