Book of Common Prayer
Yesu Ni Mkuu Kuliko Musa
3 Hivyo, kaka na dada zangu, ninyi mliochaguliwa na Mungu muwe watu wake watakatifu, mfikirieni Yesu. Yeye ndiye tunayeamini kuwa Mungu alimtuma kuja kutuokoa na awe kuhani wetu mkuu. 2 Mungu akamfanya kuhani wetu mkuu, naye akawa mwaminifu kwa Mungu kama Musa alivyokuwa. Naye alifanya kila kitu ambacho Mungu alimtaka akifanye katika nyumba ya Mungu. 3 Mtu anapojenga nyumba, watu watamheshimu mjenzi zaidi kuliko ile nyumba. Ndivyo ilivyo kwa Yesu. Anastahili heshima kubwa kuliko Musa. 4 Kila nyumba huwa imejengwa na mtu fulani, lakini Mungu alijenga kila kitu. 5 Musa alikuwa mwaminifu kama mtumishi katika nyumba yote ya Mungu. Aliwajulisha watu yale ambayo Mungu angeyasema katika siku zijazo. 6 Lakini Kristo ni mwaminifu katika kuitawala nyumba ya Mungu kama Mwana. Nasi tu nyumba ya Mungu, kama tukibaki wajasiri katika tumaini kuu tunalofurahia kusema kuwa tunalo.
Tunapaswa Kuendelea Kumfuata Mungu
7 Ni kama vile anavyosema Roho Mtakatifu:
“Kama leo mtaisikia sauti ya Mungu,
8 msiifanye migumu mioyo yenu kama hapo zamani,
mlipomgeuka Mungu.
Hiyo ndiyo siku ulipomjaribu Mungu mle jangwani.
9 Kwa miaka 40 jangwani, watu wako wakaona niliyoyatenda.
Lakini walinijaribu na ustahimilivu wangu.
10 Hivyo nikawakasirikia.
Nikasema, ‘Mawazo yao siku zote hayako sahihi.
Hawajawahi kamwe kuzielewa njia zangu.’
11 Hivyo nilikasirika na kuweka ahadi:
‘Kamwe hawataingia katika sehemu yangu ya pumziko.’”(A)
Yesu Asafisha Eneo la Hekalu
(Mt 21:12-13; Mk 11:15-17; Lk 19:45-46)
13 Kipindi hicho wakati wa kusherehekea Pasaka ya Wayahudi ulikaribia, hivyo ikampasa Yesu kwenda Yerusalemu. 14 Katika eneo la Hekalu aliwaona watu wakiuza ng'ombe, mbuzi na njiwa. Aliwaona wengine wakikalia meza na kufanya biashara ya kubadili fedha za watu. 15 Yesu akatengeneza kiboko kwa kutumia vipande vya kamba. Kisha akawafukuza watu wote, kondoo na ng'ombe watoke katika eneo la Hekalu. Akazipindua meza za wafanya biashara wa kubadilisha fedha na kuzitawanya fedha zao. 16 Baada ya hapo akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, “Viondoeni humu vitu hivi! Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa kununua na kuuza!”
17 Haya yaliwafanya wafuasi wake kukumbuka maneno yaliyoandikwa kwenye Maandiko: “Upendo wangu mkuu kwa Hekalu lako utaniangamiza.”(A)
18 Baadhi ya Wayahudi wakamwambia Yesu, “Tuoneshe muujiza mmoja kama ishara kutoka kwa Mungu. Thibitisha kwamba unayo haki ya kufanya mambo haya.”
19 Yesu akajibu, “Bomoeni hekalu hili nami nitalijenga tena kwa muda wa siku tatu.” 20 Wakajibu, “Watu walifanya kazi kwa miaka 46 kulijenga Hekalu hili! Je, ni kweli unaamini kwamba unaweza kulijenga tena kwa siku tatu?”
21 Lakini Yesu aliposema “hekalu hili”, alikuwa anazungumzia mwili wake. 22 Baada ya kufufuliwa kutoka katika wafu, wafuasi wake wakakumbuka kwamba alikuwa ameyasema hayo. Hivyo wakayaamini Maandiko, na pia wakayaamini yale aliyoyasema Yesu.
© 2017 Bible League International