Print Page Options
Previous Prev Day Next DayNext

Book of Common Prayer

Daily Old and New Testament readings based on the Book of Common Prayer.
Duration: 861 days
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Version
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Ps for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Job for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Error: Book name not found: Job for the version: Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Ufunuo 18:1-8

Babeli Inaangamizwa

18 Kisha nikaona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni. Malaika huyu alikuwa na nguvu kuu. Utukufu wa malaika ukaing'arisha dunia. Malaika akapaza sauti akasema:

“Ameteketezwa!
    Mji mkuu Babeli umeteketezwa!
Umekuwa nyumba ya mapepo.
    Mji ule umekuwa najisi.
Mji uliojaa kila aina ya ndege najisi.
    Ni mahali ambapo kila mnyama najisi
    na anayechukiwa anaishi.
Watu wote wa dunia wamekunywa mvinyo
    wa uzinzi wake na ghadhabu ya Mungu.
Watawala wa dunia walizini pamoja naye,
    na wafanya biashara wa ulimwengu walitajirika
    kutokana na utajiri wa anasa zake.”

Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema:

“Enyi watu wangu, tokeni katika mji huo,
    ili msishiriki katika dhambi zake.
    Ili msiteseke kwa adhabu yoyote kuu atakayoipata.
Dhambi za mji huo zimerundikana na kufika mbinguni.
    Mungu hajasahau makosa aliyotenda.
Upeni mji huo sawasawa na ulivyowapa wengine.
    Mlipeni mara mbili kadiri ya alivyotenda.
Mwandalieni mvinyo ulio na nguvu mara mbili
    ya mvinyo aliowaandalia wengine.
Alijipa utukufu mwingi na kuishi kitajiri.
    Mpeni mateso mengi na huzuni nyingi.
    Kama vile utukufu na starehe aliyoifurahia.
Hujisemea mwenyewe, ‘Mimi ni malkia nikaaye kwenye kiti changu cha enzi.
    Mimi si mjane;
    Sitakuwa na huzuni.’
Hivyo katika siku moja atateseka
    kwa njaa kuu, maombolezo na kifo.
Atateketezwa kwa moto,
    kwa sababu Bwana Mungu anayemhukumu ni mwenye nguvu.”

Mathayo 5:21-26

Yesu Afundisha Kuhusu Hasira

21 Mmesikia kuwa hapo kale baba zetu waliambiwa, ‘Usimwue yeyote. Na yeyote atakayeua atahukumiwa.’(A) 22 Lakini ninawaambia, msimkasirikie mtu yeyote kwa sababu mkifanya hivyo mtahukumiwa. Na mkimtukana mtu yeyote, vivyo hivyo mtahukumiwa na baraza kuu. Na ukimwita mtu kuwa ni mjinga, utakuwa katika hatari ya kutupwa kwenye moto wa Jehanamu.

23 Unapokwenda kutoa sadaka yako madhabahuni na ukakumbuka kuwa kuna mtu ana jambo dhidi yako. 24 Unapaswa kuiacha sadaka yako kwenye madhabahu na uende kupatana na mtu huyo. Ukiisha patana naye ndipo urudi na kuitoa sadaka hiyo.

25 Akiwepo mtu anayetaka kukushtaki, patana naye haraka. Jitahidi kufanya hivyo kabla ya kufika mahakamani, hata kama bado mpo njiani. Usipofanya hivyo anaweza kukupeleka kwa hakimu. Na hakimu atakupeleka kwa walinzi watakaokufunga gerezani. 26 Ninakuhakikishia kuwa hautatoka huko mpaka umelipa kila kitu unachodaiwa.

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)

© 2017 Bible League International