Yohana 5
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Amponya Mtu Bwawani
5 Baadaye, Yesu akaenda Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu maalumu ya Wayahudi. 2 Huko Yerusalemu kulikuwa na bwawa lenye mabaraza matano. Kwa Kiaramu liliitwa Bethzatha.[a] Bwawa hili lilikuwa karibu na Lango la Kondoo. 3 Wagonjwa wengi walikuwa wamelala katika mabaraza pembeni mwa bwawa. Baadhi yao walikuwa wasiyeona, wengine walemavu wa viungo, na wengine waliopooza mwili.[b] 4 Nyakati zingine malaika wa Bwana alishuka bwawani na kuyatibua maji. Baada ya hapo, mtu wa kwanza aliyeingia bwawani aliponywa ugonjwa aliokuwa nao.[c] 5 Mmoja wa watu waliolala hapo alikuwa mgonjwa kwa muda wa miaka thelathini na minane. 6 Yesu alimwona akiwa amelala hapo na kutambua kuwa amekuwa mgonjwa kwa muda mrefu sana. Hivyo akamwuliza, “Je, unataka kuwa mzima?”
7 Yule mgonjwa akajibu, “Bwana, hakuna mtu wa kunisaidia kuingia kwenye bwawa mara maji yanapotibuliwa. Najitahidi kuwa wa kwanza kuingia majini. Lakini ninapojaribu, mtu mwingine huniwahi na kuingia majini kabla yangu.”
8 Kisha Yesu akasema, “Simama juu! Beba kirago chako na utembee.” 9 Mara hiyo, mtu huyo akapona. Akabeba kirago chake na kuanza kutembea.
Siku yalipotokea haya yote ilikuwa ni Siku ya Sabato.[d] 10 Hivyo baadhi ya Wayahudi wakamwambia yule mtu aliyeponywa, “Leo ni Sabato. Kulingana na sheria yetu wewe hauruhusiwi kubeba mkeka katika siku ya Sabato!”
11 Lakini yeye akajibu, “Yule mtu aliyeniponya aliniambia, ‘Beba mkeka wako uende.’”
12 Wakamwuliza, “Ni nani aliyekuambia kubeba mkeka wako na kutembea?”
13 Lakini yule mtu aliyeponywa hakuwa amemfahamu ni nani. Walikuwepo watu wengi hapo, na Yesu alikwisha kuondoka.
14 Baadaye, Yesu akamwona huyo mtu Hekaluni na akamwambia, “Tazama, umepona sasa. Kwa hivyo uache kutenda dhambi tena, la sivyo jambo baya zaidi laweza kukupata.” 15 Kisha huyo mtu akaondoka na kurudi kwa wale Wayahudi waliomuuliza. Naye aliwaeleza kuwa Yesu ndiye aliyemponya.
16 Yesu alikuwa anayafanya yote haya katika siku ya Sabato. Hivyo Wayahudi hao wakaanza kumsumbua asiendelee. 17 Lakini yeye akawaambia, “Baba yangu hajawahi kuacha kufanya kazi, hivyo nami pia nafanya kazi.” 18 Hili likawafanya waongeze juhudi ya kumwua. Wakasema, “Mwanzoni mtu huyu alikuwa anavunja sheria kuhusu siku ya Sabato. Kisha akasema kwamba Mungu ni Baba yake! Yeye anajifanya kuwa yuko sawa na Mungu.”
Yesu Anayo Mamlaka ya Mungu
19 Lakini Yesu akajibu, “Hakika nawaambieni kuwa Mwana hawezi kufanya chochote peke yake. Bali hufanya tu yale anayoona Baba yake anayafanya. Kwa maana Mwana hufanya mambo ambayo Baba huyafanya. 20 Baba anampenda Mwana na humwonesha kila kitu anachofanya. Pia Baba atamwonesha Mwana mambo makuu ya kufanya kuliko hili. Kisha nyote mtashangazwa. 21 Baba huwafufua wafu na kuwapa uzima. Kwa njia hiyo hiyo, Mwana pia huwapa uzima wale anaowataka.”
22 “Vile vile, Baba hamhukumu mtu. Bali amempa Mwana nguvu ya kufanya hukumu zote. 23 Mungu alifanya hivi ili watu wote waweze kumheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Mtu yeyote asiyemheshimu Mwana hamheshimu Baba. Kwani Baba ndiye aliyemtuma Mwana.
24 Kwa hakika nawaambia, yeyote anayesikia ninayosema na kumwamini yule aliyenituma anao uzima wa milele. Hawa hawatahukumiwa kuwa na hatia. Kwani tayari wameshaivuka mauti na kuingia ndani ya uzima. 25 Mniamini, wakati muhimu sana unakuja. Wakati huo tayari upo ambapo watu waliokufa wataisikia sauti ya Mwana wa Mungu. Na hao watakaoisikia watafufuka na kuwa hai. 26 Uzima huja kutoka kwa Baba mwenyewe. Na pia Baba amemruhusu Mwana kutoa uzima. 27 Na Baba amempa Mwana mamlaka ya kuwahukumu watu wote kwa sababu yeye ndiye Mwana wa Adamu.
28 Ninyi msishangazwe na hili. Wakati unakuja ambapo watu wote waliokufa na kuwamo makaburini mwao wataisikia sauti yake. 29 Kisha watatoka nje ya makaburi yao. Wale waliotenda mema watafufuka na kupata uzima wa milele. Lakini wale waliotenda maovu watafufuka na kuhukumiwa kwa kuwa na hatia.
30 Siwezi kufanya jambo lolote peke yangu. Ninahukumu kama vile ninavyoagizwa. Na hukumu yangu ni halali, kwa sababu sitafuti kujifurahisha mwenyewe. Bali ninataka tu kumfurahisha yeye aliyenituma.”
Yesu Asema Zaidi Na Viongozi wa Kiyahudi
31 “Endapo nitawaeleza watu mambo yangu mwenyewe, watu hawatakuwa na uhakika kama yale ninayosema ni kweli. 32 Lakini yupo mwingine anayewaeleza watu mambo yangu, nami nafahamu kuwa yale anayoyasema juu yangu ni kweli.
33 Mliwatuma watu kwa Yohana, naye akawaambia yaliyo kweli. 34 Hivyo sihitaji mtu yeyote wa kuwaeleza watu juu yangu, isipokuwa nawakumbusha ninyi yale aliyoyasema Yohana ili muweze kuokolewa. 35 Yohana alikuwa kama taa iliyowaka na kutoa mwanga, nanyi mlipata raha mkiufurahia mwanga wake japo kwa muda.
36 Hata hivyo uthibitisho nilionao mwenyewe juu yangu ni mkuu kuliko chochote alichokisema Yohana. Mambo ninayofanya ndiyo yanayonithibitisha. Haya ndiyo Baba aliyonipa kufanya. Nayo yanadhihirisha kuwa Baba alinituma. 37 Na Baba aliyenituma yeye mwenyewe ametoa uthibitisho juu yangu. Lakini hamjawahi kabisa kuisikia sauti yake. Hamjawahi pia kuuona uso wake jinsi ulivyo. 38 Mafundisho ya Baba hayakai ndani yenu, kwa sababu hamumwamini yule aliyetumwa na Baba. 39 Mnajifunza Maandiko kwa makini. Nanyi mnafikiri kuwa yanawapa uzima wa milele. Maandiko haya haya yanaeleza habari zangu! 40 Lakini mnakataa kuja kwangu kuupata huo uzima.
41 Sitaki kutukuzwa nanyi ama na mwanadamu mwingine yeyote. 42 Hata hivyo ninawajua ninyi, na ninajua kwamba hamna upendo kwa Mungu. 43 Nimekuja kutoka kwa Baba yangu nami ni msemaji wake, lakini hamnikubali. Lakini watu wengine wakija wakijisemea mambo yao tu, mnawakubali! 44 Ninyi mnapenda kupeana sifa kila mmoja kwa mwenzake. Lakini hamjaribu kupata sifa zinazotoka kwa Mungu wa pekee. Hivyo mtawezaje kuamini? 45 Msifikiri kwamba mimi ndiye nitakayesimama mbele za Baba na kuwashtaki. Musa ndiye atakayewashtaki. Na ndiye mliyetegemea angeliwaokoa. 46 Kama kwa hakika mlimwamini Musa, nami mlipaswa kuniamini, kwa sababu yeye aliandika habari juu yangu. 47 Lakini hamuyaamini aliyoyaandika, hivyo hamuwezi kuyaamini ninayoyasema.”
Footnotes
- 5:2 Bethzatha Pia huitwa Bethsaida au Bethesda. Ama bwawa la maji lililoko kaskazini mwa Hekalu kule.
- 5:3 Nakala zingine za Kiyunani zimeongeza, “na husubiri maji yatibuliwe”.
- 5:4 Nakala zingine za baadaye ziliongeza mstari wa 4, hivyo kutenganisha mstari wa 4 na wa 5: “Nyakati zingine malaika wa Bwana alishuka bwawani na kuyatibua maji. Baada ya hapo, mtu wa kwanza aliyeingia bwawani aliponywa ugonjwa aliokuwa nao.”
- 5:9 Siku ya Sabato Ilikuwa siku maalumu kwa Waisraeli na Wayahudi. Kwa amri ya Mungu siku hiyo ilitengwa kama siku ya mapumziko na ya kumheshimu Mungu.
John 5
English Standard Version
The Healing at the Pool on the Sabbath
5 After this there was a (A)feast of the Jews, and Jesus went up to Jerusalem.
2 Now there is in Jerusalem by (B)the Sheep Gate a pool, in Aramaic[a] called Bethesda,[b] which has five roofed colonnades. 3 In these lay a multitude of invalids—blind, lame, and (C)paralyzed.[c] 5 One man was there who had been an invalid for thirty-eight years. 6 When Jesus saw him lying there and knew that he had already been there a long time, he said to him, “Do you want to be healed?” 7 The sick man answered him, “Sir, I have no one to put me into the pool when the water is stirred up, and while I am going another steps down before me.” 8 Jesus said to him, (D)“Get up, take up your bed, and walk.” 9 (E)And at once the man was healed, and he took up his bed and walked.
(F)Now that day was the Sabbath. 10 So the Jews[d] said to the man who had been healed, “It is the Sabbath, and (G)it is not lawful for you to take up your bed.” 11 But he answered them, “The man who healed me, that man said to me, ‘Take up your bed, and walk.’” 12 They asked him, “Who is the man who said to you, ‘Take up your bed and walk’?” 13 Now the man who had been healed did not know who it was, for (H)Jesus had withdrawn, as there was a crowd in the place. 14 Afterward Jesus found him in the temple and said to him, “See, you are well! (I)Sin no more, (J)that nothing worse may happen to you.” 15 The man went away and told the Jews that it was Jesus who had healed him. 16 And this was why the Jews (K)were persecuting Jesus, (L)because he was doing these things on the Sabbath. 17 But Jesus answered them, “My Father is working until now, and I am working.”
Jesus Is Equal with God
18 This was why the Jews (M)were seeking all the more to kill him, (N)because not only was he (O)breaking the Sabbath, but he was even calling God (P)his own Father, (Q)making himself equal with God.
The Authority of the Son
19 So Jesus said to them, “Truly, truly, I say to you, (R)the Son (S)can do nothing of his own accord, but only what he sees the Father doing. For whatever the Father[e] does, that the Son does likewise. 20 For (T)the Father loves the Son and shows him all that he himself is doing. And (U)greater works than these will he show him, so that (V)you may marvel. 21 For as the Father (W)raises the dead and (X)gives them life, so (Y)also the Son gives life (Z)to whom he will. 22 (AA)For the Father judges no one, but (AB)has given all judgment to the Son, 23 that all may honor the Son, just as they (AC)honor the Father. (AD)Whoever does not honor the Son does not honor the Father who sent him. 24 Truly, truly, I say to you, (AE)whoever hears my word and (AF)believes him who sent me has eternal life. He (AG)does not come into judgment, but (AH)has passed from death to life.
25 “Truly, truly, I say to you, (AI)an hour is coming, and is now here, when (AJ)the dead will hear (AK)the voice of the Son of God, and those who hear (AL)will live. 26 (AM)For as the Father has life in himself, (AN)so he has granted the Son also to have life in himself. 27 And he (AO)has given him authority to execute judgment, because he is the Son of Man. 28 Do not marvel at this, for (AP)an hour is coming when (AQ)all who are in the tombs will hear his voice 29 and come out, (AR)those who have done good to the resurrection of life, and those who have done evil to the resurrection of judgment.
Witnesses to Jesus
30 (AS)“I can do nothing on my own. As I hear, I judge, and (AT)my judgment is just, because (AU)I seek not my own will (AV)but the will of him who sent me. 31 (AW)If I alone bear witness about myself, my testimony is not true. 32 There is (AX)another who bears witness about me, and (AY)I know that the testimony that he bears about me is true. 33 (AZ)You sent to John, and he has borne witness to the truth. 34 Not that (BA)the testimony that I receive is from man, but I say these things so that you may be saved. 35 He was a burning and (BB)shining lamp, and (BC)you were willing to rejoice for a while in his light. 36 But (BD)the testimony that I have is greater than that of John. For (BE)the works that the Father has given me (BF)to accomplish, the very works that I am doing, (BG)bear witness about me that (BH)the Father has sent me. 37 And the Father who sent me (BI)has himself borne witness about me. His voice you have never heard, (BJ)his form you have never seen, 38 and (BK)you do not have his word abiding in you, for you do not believe the one whom he has sent. 39 (BL)You search the Scriptures because you think that in them you have eternal life; and (BM)it is they that bear witness about me, 40 yet (BN)you refuse to come to me that you may have life. 41 (BO)I do not receive glory from people. 42 But (BP)I know that you do not have (BQ)the love of God within you. 43 I have come (BR)in my Father's name, and (BS)you do not receive me. (BT)If another comes in his own name, you will receive him. 44 How can you believe, when you receive glory from one another and (BU)do not seek the glory that comes from (BV)the only God? 45 Do not think that I will accuse you to the Father. There is one who accuses you: Moses, (BW)on whom you have set your hope. 46 For if you believed Moses, you would believe me; for (BX)he wrote of me. 47 But (BY)if you do not believe his writings, how will you believe my words?”
Footnotes
- John 5:2 Or Hebrew
- John 5:2 Some manuscripts Bethsaida
- John 5:3 Some manuscripts insert, wholly or in part, waiting for the moving of the water; 4 for an angel of the Lord went down at certain seasons into the pool, and stirred the water: whoever stepped in first after the stirring of the water was healed of whatever disease he had
- John 5:10 The Greek word Ioudaioi refers specifically here to Jewish religious leaders, and others under their influence, who opposed Jesus in that time; also verses 15, 16, 18
- John 5:19 Greek he
© 2017 Bible League International
The ESV® Bible (The Holy Bible, English Standard Version®), © 2001 by Crossway, a publishing ministry of Good News Publishers. ESV Text Edition: 2025.
