Yesu Ahudhuria Sikukuu Ya Vibanda Yerusalemu

Baada ya mambo haya, Yesu alikwenda sehemu mbalimbali za Galilaya. Aliamua kutokwenda Yudea kwa sababu Wayahudi huko wali taka kumwua. Sikukuu ya Vibanda ilipokaribia, ndugu zake Yesu walimwambia, “Ni vema utoke hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wapate kuona miujiza unayofanya. Mtu anayetaka kujulikana, hafanyi mambo yake kwa siri. Kwa kuwa unafanya mambo haya, jion yeshe kwa ulimwengu.” Hata ndugu zake hawakumwamini.

Yesu akawajibu, “Wakati wangu wa kwenda huko haujafika. Ninyi mnaweza kwenda wakati wo wote. Ulimwengu hauwachukii ninyi lakini unanichukia mimi kwa sababu ninawashuhudia kwamba matendo yao ni maovu. Ninyi nendeni kwenye sikukuu, lakini mimi sitahudhuria sikukuu hii kwa sababu wakati wangu haujawadia.” Baada ya kusema hivyo, akabaki Galilaya. 10 Lakini ndugu zake walipokwisha kuondoka kwenda kwenye sikukuu, yeye pia alikwenda kwa siri. 11 Huko kwenye sikukuu viongozi wa Wayahudi walikuwa wakimtafuta na kuulizana, “Yuko wapi?”

12 Kulikuwa na minong’ono iliyoenea kumhusu Yesu. Baadhi ya watu walisema, “Ni mtu mwema” na wengine wakasema, “Sio, ana wadanganya watu.” 13 Lakini hakuna aliyemsema wazi wazi maana wote waliwaogopa viongozi wa Wayahudi.

Yesu Atangaza Mamlaka Yake

14 Katikati ya sikukuu, Yesu alikwenda Hekaluni akaanza kuwafundisha watu. 15 Viongozi wa Wayahudi walistaajabia mafund isho yake wakasema, “Amefahamuje mambo haya naye hakusoma?”

16 Yesu akawajibu , “Mafundisho yangu hayatoki kwangu. Yanatoka kwake yeye aliyenituma. 17 Mtu ye yote akipenda kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu au ninasema kwa mamlaka yangu mwenyewe. 18 Mtu anayesema kwa mamlaka yake mwenyewe hufanya hivyo kwa kutaka kujitukuza. Lakini mtu anayetafuta kumtukuza Mungu aliyemtuma, ni mwaminifu na hana udhalimu wo wote. 19 Kwani Musa hakuwapeni sheria? Mbona hakuna hata mmoja wenu anayetii sheria? Kwa nini mnataka kuniua?”

21 Yesu akawajibu, “Nimefanya muujiza mmoja na nyote mkas taajabu. 22 Lakini kwa kuwa Musa aliwaamuru kutahiri watoto wenu wa kiume, ingawa kwa kweli si Musa aliyeanzisha desturi hii ila ni mababu zenu, mnamtahiri mtoto hata siku ya sabato. 23 Ikiwa mtu aweza kutahiriwa siku ya sabato kusudi sheria ya Musa isi vunjwe, kwa nini mnanikasirikia kwa kumfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya sabato? 24 Msitoe hukumu kwa kuangalia mambo juu juu. Hukumuni kwa haki.”

25 Baadhi ya wakazi wa Yerusalemu wakasemezana, “Tazameni, huyu si yule mtu wanayetaka kumwua? 26 Mbona anazungumza hadhar ani na wala hawasemi lo lote? Je, inawezekana wanafahamu kwa kweli kama yeye ndiye Kristo? 27 Lakini huyu mtu tunafahamu ana kotoka, nasi tunajua ya kuwa Kristo atakapokuja hakuna atakayefa hamu atokako.”

28 Yesu, akiendelea kufundisha Hekaluni, akatangaza kwa sauti, “Hivi kweli mnanifahamu na kufahamu ninakotoka? Mimi sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe. Yeye aliyenituma ni wa kweli na wala ninyi hamumjui. 29 Lakini mimi namjua kwa kuwa nimetoka kwake, na ndiye aliyenituma.”

30 Basi viongozi wa Wayahudi wakajaribu kumkamata, lakini hakuna aliyethubutu kumshika kwa sababu wakati wake ulikuwa bado haujatimia.

31 Watu wengi kati ya wale waliokuwepo, walimwamini, wakasema, “Hivi Kristo akija, atafanya miujiza mikuu zaidi kuliko aliyoifanya huyu?”

Walinzi Wanatumwa Kumkamata Yesu

32 Mafarisayo waliposikia minong’ono hii, wao pamoja na makuhani wakuu, waliwatuma walinzi wa Hekalu waende kumkamata.

33 Yesu akasema, “Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitarudi kwake aliyenituma. 34 Mtanitafuta lakini hamtaniona kwa kuwa huko nitakapokuwa, ninyi hamwezi kufika.” 35 Basi viongozi wa Wayahudi wakaulizana, “Huyu mtu anataka kwenda wapi ambapo hatuwezi kumpata? Au anataka kwenda katika miji ya Wagiriki ambapo baadhi ya watu wetu wametawanyikia, akawafundishe Wagiriki 36 Ana maana gani anaposema, ‘Mtanitafuta lakini hamtaniona, na huko nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika ?”’

Vijito Vya Maji Yaletayo Uzima

37 Siku ya mwisho ya sikukuu, ambayo kwa kawaida ndio ili kuwa kilele cha sherehe, Yesu alisimama akasema kwa sauti kuu, “Mtu ye yote mwenye kiu na aje kwangu anywe. 38 Kama Maandiko yasemavyo, ye yote aniaminiye, vijito vya maji yaletayo uzima vitatiririka kutoka moyoni mwake.” 39 Yesu alisema haya kuhusu Roho Mtakatifu ambaye wote waliomwamini Yesu wangempokea, kwani mpaka wakati huo, Roho alikuwa bado hajatolewa, kwa kuwa Yesu alikuwa bado hajainuliwa na kutukuzwa.

40 Waliposikia maneno hayo, baadhi ya watu walisema, “Hakika huyu ndiye yule Nabii.” 41 Wengine wakasema, “Huyu ni Masihi!” Lakini wengine wakauliza, “Kwani Masihi kwao ni Gali laya? 42 Je, Maandiko hayakusema kuwa Masihi atakuwa mzao wa Daudi na kwamba atazaliwa Bethlehemu, mji alioishi Daudi?” 43 Kwa hiyo kukawa na mgawanyiko kati ya watu kumhusu Yesu. 44 Baadhi yao walitaka kumkamata, lakini hakuna aliyethubutu kumgusa.

Kutokuamini Kwa Viongozi Wa Wayahudi

45 Hatimaye wale walinzi wa Hekalu waliokuwa wametumwa kum kamata Yesu, walirudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo. Wakauli zwa, “Mbona hamkumleta ?”

46 Wale walinzi wakajibu, “Hakuna mtu ambaye amewahi kufundisha kama yeye.” 47 Mafarisayo wakajibu, “Ameweza kuwa danganya hata ninyi? 48 Je, mmewahi kuona kiongozi ye yote au mmoja wa Mafarisayo ambaye amemwamini? 49 Lakini huu umati wa watu wasiojua sheria ya Musa, wamelaaniwa.”

50 Ndipo Nikodemo, yule aliyemwendea Yesu siku moja, ambaye alikuwa kati yao akauliza, 51 “Je, sheria zetu zinaturuhusu kumhukumu mtu kabla ya kumsikiliza na kufahamu alilotenda?”

52 Wakamjibu, “Je, wewe pia unatoka Galilaya? Chunguza Maandiko nawe utaona kwamba hakuna nabii anayetokea Galilaya!” [ 53 Kisha wakaondoka, kila mtu akarudi nyumbani kwake.

Yesu na Ndugu Zake

Baada ya hayo, Yesu alitembea kuizunguka miji ya Galilaya. Hakutaka kutembelea Uyahudi, kwa sababu viongozi wa Kiyahudi kule walitaka kumuua. Huu ulikuwa ni wakati wa sherehe za sikukuu ya Wayahudi ya Vibanda. Hivyo ndugu zake wakamwambia, “Unapaswa kuondoka hapa na kwenda kwenye sikukuu Uyahudi. Kisha wafuasi wako kule wataweza kuona ishara unazofanya. Ikiwa unataka kujulikana, basi usiyafiche mambo unayoyafanya. Ikiwa unaweza kufanya mambo ya ajabu hivi, acha ulimwengu wote uone.” Ndugu zake Yesu walisema hivi kwa kuwa hata wao hawakumwamini.

Yesu akawaambia, “Wakati unaonifaa kufanya hivyo haujafika, lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa. Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi. Bali ulimwengu unanichukia mimi kwa sababu nawaambia watu ulimwenguni ya kwamba wanafanya maovu. Hivyo ninyi nendeni kwenye sikukuu. Mimi sitaenda sasa, kwa sababu wakati unaonifaa haujafika.” Baada ya Yesu kusema hayo, akabaki Galilaya.

10 Ndugu zake nao wakaondoka kwenda kwenye sikukuu ya Wayahudi ya Vibanda. Baada ya kuondoka kwao Yesu naye akaenda huko, ingawa hakutaka watu wamwone. 11 Baada ya sikukuu ile kupita viongozi wa Kiyahudi wakawa wanamtafuta Yesu. Wakasema, “Yuko wapi huyo Yesu?”

12 Lilikuwepo kundi la watu wengi mahali pale. Wengi kati yao walikuwa wakizungumza kwa siri kuhusu Yesu. Wengine wakasema, “Huyu ni mtu mzuri.” Lakini wengine wakakataa na kusema, “Hapana, mtu huyo huwadanganya watu.” 13 Pamoja na hayo hakuwepo mtu aliyekuwa na busara zaidi kati yao kusema na Yesu kwa uwazi. Kwani waliwaogopa viongozi wa Wayahudi.

Yesu Afundisha Yerusalemu

14 Sherehe ile ilipokaribia kuisha, Yesu akaenda katika maeneo ya Hekalu na kuanza kufundisha. 15 Viongozi wa Kiyahudi waliomsikiliza walishangazwa na kusema, “Mtu huyu amejifunza wapi mambo haya yote? Yeye hakuwahi kupata mafundisho kama yale tuliyonayo.”

16 Yesu akajibu, “Ninayofundisha siyo yangu. Mafundisho yangu yanatoka kwake Yeye aliyenituma. 17 Watu wanaotaka kufanya kwa uhakika kama anavyotaka Mungu watafahamu kuwa mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu. Watafahamu kwamba mafundisho haya siyo yangu. 18 Kama ningeyafundisha mawazo yangu, ningekuwa najitafutia heshima yangu mwenyewe. Lakini kama najaribu kumletea heshima Yeye aliyenituma, basi naweza kuaminiwa. Yeyote anayefanya kama hivyo hawezi kusema uongo. 19 Musa aliwapa sheria, sivyo? Lakini hamuitii hiyo sheria. Kama mnaitii, kwa nini basi mnataka kuniua?”

20 Watu wakamjibu Yesu, “Pepo amekuchanganya akili! Sisi hatuna mipango ya kukuua!”

21 Yesu akawambia, “Nilitenda ishara moja siku ya Sabato, na wote mkashangaa. 22 Lakini mnatii sheria aliyowapa Musa kuhusu kutahiriwa; nanyi mnatahiri hata siku ya Sabato! (Lakini hakika, Musa siye aliyewatahiri. Tohara Ilitoka kwa baba zenu walioishi kabla ya Musa.) Ndiyo, siku zote mnatahiri wana wenu hata siku ya Sabato. 23 Hii inaonesha kuwa mtu anaweza kutahiriwa siku ya Sabato ili kuitimiza sheria ya Musa. Sasa kwa nini mnanikasirikia mimi kwa kuuponya mwili wote wa mtu siku ya Sabato? 24 Acheni kuhukumu mambo ya watu kwa jinsi mnavyoyaona. Muwe makini kutoa kuhukumu kwa njia ya haki kabisa.”

Watu Wajiuliza Ikiwa Yesu Ni Masihi

25 Kisha baadhi ya watu waliokuwepo Yerusalemu wakasema, “Huyo ndiye mtu wanayetaka kumuua. 26 Lakini anafundisha mahali ambapo kila mtu anaweza kumwona na kumsikia. Wala hakuna anayejaribu kumzuia kufundisha. Inawezekana viongozi wamekubali kuwa kweli yeye ni Masihi. 27 Lakini Masihi halisi atakapokuja, hakuna atakayejua anakotoka. Nasi tunajua nyumbani kwake mtu huyu ni wapi.”

28 Yesu alikuwa bado anafundisha katika eneo la Hekalu aliposema kwa sauti, “Ni kweli mnanijua mimi na kule ninakotoka? Niko hapa, lakini siyo kwa matakwa yangu. Nilitumwa na Yeye aliye wa kweli. Lakini ninyi hamumjui. 29 Mimi namfahamu kwa sababu ninatoka kwake. Naye Ndiye aliyenituma.”

30 Yesu aliposema hivi, watu wakajaribu kumkamata. Lakini hakuna aliyethubutu hata kumgusa, kwa sababu wakati unaofaa kufanya hivyo ulikuwa bado haujafika. 31 Hata hivyo watu wengi wakamwamini Yesu. Wakasema, “Je, tunafikiri kuna haja ya kuendelea kumngojea Masihi mwingine aje atakayetenda ishara nyingine zaidi ya zile alizotenda mtu huyu?”

Viongozi wa Kiyahudi Wajaribu Kumkamata Yesu

32 Mafarisayo wakasikia yale ambayo watu walikuwa wakiyasema juu ya Yesu. Kwa sababu hiyo viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakawatuma walinzi wa Hekalu kwenda kumkamata. 33 Kisha Yesu akasema, “Nitakuwa nanyi kwa muda mfupi. Kisha nitarudi kwake Yeye aliyenituma. 34 Ninyi mtanitafuta, lakini hamtaniona. Nanyi hamwezi kuja kule nitakapokuwa.”

35 Hawa Wayahudi wakaambiana wao kwa wao, “Huyu mtu atakwenda wapi sisi tusikoweza kufika? Je, anaweza kwenda kwenye miji ya Wayunani wanamoishi watu wetu? Je, atawafundisha Wayunani katika miji hiyo? 36 Anasema, ‘Mtanitafuta, lakini hamtaniona.’ Vile vile anasema, ‘Hamwezi kuja kule nitakapokwenda.’ Maana yake ni nini?”

Yesu Azungumza Juu ya Roho Mtakatifu

37 Siku ya mwisho ya kusherehekea sikukuu ikafika. Nayo Ilikuwa siku muhimu zaidi. Katika siku hiyo Yesu alisimama na kusema kwa sauti kubwa, “Yeyote aliye na kiu aje kwangu anywe. 38 Kama mtu ataniamini, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka ndani ya moyo wake. Ndivyo Maandiko yanavyosema.” 39 Yesu alikuwa anazungumza juu ya Roho Mtakatifu ambaye alikuwa hajatolewa kwa watu bado, kwa sababu Yesu naye alikuwa bado hajatukuzwa. Ingawa baadaye, wale waliomwamini Yesu wangempokea huyo Roho.

Watu Wanabishana Juu ya Yesu

40 Watu waliposikia maneno aliyosema Yesu, baadhi yao wakasema, “Hakika mtu huyu ni nabii.”[a]

41 Wengine wakasema, “Huyu ni Masihi.”

Na wengine wakasema, “Masihi hawezi kutoka Galilaya. 42 Maandiko yanasema kwamba Masihi atatoka katika ukoo wa Daudi. Na wanasema kwamba atatoka Bethlehemu, mji alimoishi Daudi.” 43 Kwa jinsi hiyo watu hawakukubaliana wao kwa wao kuhusu Yesu. 44 Baadhi yao wakataka kumkamata. Lakini hakuna aliyejaribu kufanya hivyo.

Baadhi ya Viongozi wa Kiyahudi Wakataa Kuamini

45 Walinzi wa Hekalu wakarudi kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo. Makuhani na Mafarisayo wakawauliza, “Kwa nini hamjamleta Yesu?”

46 Walinzi wa Hekalu wakajibu, “Hatujawahi kumsikia mtu akisema mambo ya ajabu kiasi hicho!”

47 Mafarisayo wakajibu, “Kwa hiyo Yesu amewadanganya hata ninyi? 48 Hamuoni kuwa hakuna kiongozi yeyote wala sisi Mafarisayo anayemwamini? 49 Lakini watu hao walio nje wasiojua sheria wamo katika laana ya Mungu.”

50 Lakini Nikodemu alikuwa katika kundi lile. Naye ndiye yule aliyekwenda kumwona Yesu pale mwanzo.[b] Naye akasema, 51 “Sheria yetu haitaturuhusu kumhukumu mtu na kumtia hatiani kabla ya kumsikiliza kwanza na kuyaona aliyotenda?”

52 Viongozi wa Kiyahudi wakajibu, “Wewe nawe utakuwa umetoka Galilaya. Jifunze Maandiko. Hutapata lolote kuhusu nabii[c] anayetoka Galilaya.”

Mwanamke Afumaniwa Akizini

53 Kisha wote wakaondoka na kwenda nyumbani.

Footnotes

  1. 7:40 nabii Huenda walikuwa na maana nabii ambaye Mungu, alimwambia Musa ya kwamba atamtuma. Tazama Kum 18:15-19.
  2. 7:50 Naye ndiye … mwanzo Hadithi juu ya Nikodemo kwenda na kuongea na Yesu katika Yh 3:1-21.
  3. 7:52 kuhusu nabii Nakala mbili za kale za Kiyunani zina “Nabii”, ambayo ina maana “nabii kama vile Musa” anayetajwa katika Kum 18:15. Katika Mdo 3:22 na 7:37 hii inaeleweka kuwa ni Masihi kama katika mstari wa 40 hapo juu.