Nafasi Ya Pekee Ya Waisraeli

Ninasema kweli katika Kristo na dhamiri yangu inanishuhudia kwa njia ya Roho Mtakatifu kuwa sisemi uongo. Nina huzuni sana na uchungu usiokwisha moyoni mwangu. Kwa maana ningetamani hata mimi nilaaniwe na kutengwa na Kristo kama kufanya hivyo kungeweza kuwasaidia ndugu zangu tulio wa kabila moja. Nazungumza kuhusu Waisraeli ambao Mungu aliwateua kuwa wana wake, wakapewa utukufu wake, maagano yake, sheria yake, ibada ya kweli, na ahadi zake. Wao ni wa uzao wa mababu wa kwanza, na katika taifa lao Kristo alitoka kama mwanadamu; yeye ambaye ni Mungu aliye juu ya vyote, atukuzwaye milele! Amina.

Lakini hii haina maana kwamba ahadi ya Mungu kwa wana wa Israeli imeshindwa. Kwa maana si wote ambao ni wa uzao wa Israeli ambao ni wa Israeli. Wala si wazaliwa wote wa kizazi cha Abra hamu ambao ni watoto wake. Ahadi ya Mungu kwa Abrahamu ilikuwa: “Watoto wako watatoka katika uzao wa Isaki.” Kwa maneno men gine, si wale watoto waliozaliwa na Ibrahimu kimwili ambao ni wana wa Mungu; bali ni wale watoto wa ahadi ambao wanahesabiwa kuwa kizazi cha Abrahamu. Kwa maana ahadi yenyewe ilisema, “Nitarudi tena wakati kama huu na Sara atapata mtoto wa kiume.”

10 Na si hivyo tu bali pia wakati Rebeka alipozaa watoto na mume mmoja, Isaki, 11 hata kabla watoto wake mapacha hawajazal iwa wala kutenda jema au baya ili mpango wa Mungu wa kuchagua uendelee, si kwa kutegemea matendo mema bali kwa kufuatana na wito wake - 12 Rebeka aliambiwa, “Mkubwa atamhudumia mdogo.” 13 Kama Maandiko yasemavyo: “Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia.”

Mungu Hana Upendeleo

14 Tusemeje basi? Kwamba Mungu ana upendeleo? La, sivyo. 15 Kwa maana Mungu alimwambia Musa, “Nitamrehemu nipendaye kumrehemu; na nitamhurumia nipendaye kumhurumia.” 16 Kwa hiyo haitegemei mapenzi ya mtu au jitihada ya mtu, bali hutegemea huruma ya Mungu. 17 Kwa maana katika Maandiko Farao anaambiwa, “Nilikuinua kwa makusudi ya kudhihirisha nguvu zangu kwako na jina langu lipate kutangazwa duniani pote.” 18 Kwa hiyo basi, Mungu humhurumia mtu ye yote apendaye kumhurumia na huufanya mgumu moyo wa mtu ye yote atakaye.

19 Bila shaka mtaniuliza, “Kama ni hivyo, kwa nini Mungu anatulaumu? Kwa maana ni nani awezaye kushindana na mapenzi yake? 20 Lakini wewe mwanadamu, una haki gani ya kumhoji Mungu? Je, kilichotengenezwa kinaweza kumwuliza aliyekitengeneza, “Kwa nini umenitengeneza hivi?” 21 Je, mfinyanzi hana haki ya kufa nya apendavyo na udongo wake? Je, si anaweza kabisa kutumia sehemu ya udongo huo kutengeneza chombo kimoja kitumikacho kwa kupamba na kutoka katika udongo huo huo akatengeneza kingine kwa matumizi ya kawaida?

22 Tunajuaje kama Mungu, kwa kutaka kuonyesha ghadhabu yake na nguvu yake, amewavumilia kwa uvumilivu mkuu wale waliomkasi risha, ambao wameandaliwa kuangamizwa? 23 Na tunajuaje kama Mungu alifanya hivi ili kuwadhihirishia utajiri wa utukufu wake wale anaowahurumia, ambao aliwaandaa tangu mwanzo kupokea utu kufu? 24 Na sisi ndio hao walioitwa, si kutoka kwa Wayahudi tu bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.

Yote Yalitabiriwa Katika Maandiko

25 Hivi ndivyo Mungu asemavyo katika kitabu cha Hosea, “Wale ambao hawakuwa watu wangu, nitawaita ‘watu wangu,’ na wale ambao hawakuwa wapendwa wangu, nitawaita ‘wapendwa wangu’.” 26 Na pale pale walipoambiwa,“Ninyi si ‘watu wangu,’ ndipo watakapoitwa, ‘Wana wa Mungu aliye hai’.” 27 Na Isaya anasema hivi kuhusu Israeli: “Ijapokuwa wana wa Israeli watakuwa wengi kama mchanga wa bahari, ni wachache tu miongoni mwao watakaooko lewa;

28 kwa maana Mungu ataitekeleza hukumu yakejuu ya ulimwengu mara moja na kuikamilisha.” 29 Na tena kama alivyotabiri Isaya,“Kama Bwana wa majeshi asingetuachia uzao, tungalikuwa kama Sodoma, na kufanywa kama Gomora.”

30 Kwa hiyo tusemeje basi? Watu wa mataifa ambao hawakuta futa kupata haki wamepewa haki kwa njia ya imani. 31 Lakini Waisraeli ambao wametafuta kupata haki kwa msingi wa sheria, hawakuipata kwa maana hawakutimiza sheria. 32 Kwa nini? Kwa sababu hawakuitafuta kwa imani bali kwa kutegemea matendo. Wali jikwaa kwenye lile ‘jiwe la kujikwaa.’ 33 Kama ilivyoandikwa kwe nye Maandiko,“Tazama naweka jiwe huko Sayuni ambalo linawafanya watu kujikwaa na mwamba utakaowaangusha, na wale watakaomtegemea hawataaibika kamwe.”

Kutokuamini Kwa Waisraeli

10 Ndugu zangu, shauku ya moyo wangu na maombi yangu kwa Mungu ni kwamba Waisraeli waokolewe. Ninashuhudia wazi kwamba wao wanajuhudi kubwa ya kumtumikia Mungu, lakini juhudi yao haitokani na kuelewa. Wameshindwa kuelewa haki itokayo kwa Mu ngu, na badala yake wakajaribu kujiwekea ya kwao; kwa hiyo hawa kutii haki ya Mungu. Kwa maana Kristo amekamilisha sheria ili kila mtu mwenye imani ahesabiwe haki.

Wokovu Ni Kwa Wote

Musa anaandika kwamba mtu anayejaribu kutenda haki kwa msingi wa sheria ataishi kwa sheria. Lakini haki itokanayo na imani husema hivi, “Usiseme nafsini mwako, ‘Ni nani atapaa mbi nguni?”’ yaani kumleta Kristo duniani, au “‘Ni nani atashuka kuzimuni?”’yaani kumleta Kristo kutoka kwa wafu. Bali inasema hivi, “Neno la Mungu liko karibu nawe; liko mdomoni mwako na moyoni mwako,” yaani, neno la imani tunayohubiri. Kama ukikiri kwa kinywa chako kuwa Yesu ni Bwana na ukiamini moyoni mwako kuwa Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka. 10 Kwa maana mtu ana poamini moyoni mwake huhesabiwa haki, na anapokiri kwa kinywa chake, huokolewa. 11 Kama yasemavyo Maandiko, “Hakuna amwami niye ambaye ataaibika.” 12 Kwa maana hakuna tofauti kati ya wote naye huwabariki wote wamwitao. 13 Kwa maana, “Kila mtu atakayeliita Jina la Bwana, ataokoka.”

14 Lakini watu watamwitaje yeye ambaye hawajamwamini? Na watamwaminije yeye ambaye hawajawahi kumsikia? Na watamsikiaje kama mtu hakuwahubiria? 15 Na watu watahubirije kama hawaku tumwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri mno miguu ya hao wanaohubiri Habari Njema!”

16 Lakini si wote walioipokea Habari Njema. Kwa maana Isaya alisema:“Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?” 17 Basi, chanzo cha imani ni kusikia, na kusikia huja kwa kuhubiri neno la Kristo. 18 Lakini nauliza, hivi wao hawajasikia? Hakika wame sikia; kwa maana Maandiko yanasema: “Sauti yao imeenea duniani kote, na maneno yao yamefika miisho ya ulimwengu.” 19 Nauliza tena, je, Waisraeli hawakuelewa? Kwanza Musa anasema, “Nitawa fanya muone wivu kwa ajili ya wale ambao hawajawa taifa bado; nitawafanya mkasirike kwa ajili ya taifa la watu wasio elewa.” 20 Na Isaya anasema kwa ujasiri, “Wale ambao wali kuwa hawanitafuti, wamenipata. Nimejidhihirisha kwa wale ambao walikuwa hawaniulizii.” 21 Lakini kuhusu wana wa Israeli anasema: “Mchana kutwa nimewanyooshea mikono watu wakaidi na wasiotii.”

Huruma Ya Mungu Kwa Waisraeli

11 Kwa hiyo nauliza, je, Mungu amewakataa watu wake? La, sivyo. Mimi mwenyewe ni Mwisraeli, wa uzao wa Ibrahimu na wa kabila la Benjamini. Mungu hajawakataa watu wake ambao aliwajua tokea mwanzo. Hamfahamu Maandiko yanavyosema kuhusu Eliya, jinsi alivyomlalamikia Mungu kuhusu Waisraeli akisema, “Bwana, wamewaua manabii wako na kuziharibu madhabahu zako, nimebaki mimi peke yangu, nao wanataka kuniua? Na Mungu alimjibuje? “Nime bakiza kwa ajili yangu watu elfu saba ambao hawajapiga magoti kumwabudu Baali.” Ndivyo ilivyo hata sasa; wapo wachache wal iosalia ambao Mungu amewachagua kwa neema yake. Lakini ikiwa wamechaguliwa kwa neema, haiwezekani tena wakachaguliwa kwa msingi wa matendo. Kama ingekuwa hivyo, neema isingekuwa neema tena.

Tusemeje basi? Waisraeli walishindwa kupata kile ambacho walikitafutakwa bidii. Lakini waliochaguliwa walikipata. Wa liobaki walifanywa wagumu, kama Maandiko yasemavyo, “Mungu ali wapa mioyo mizito, na macho ambayo hayawezi kuona, na masikio ambayo hayawezi kusikia, hata mpaka leo.” Naye Daudi anasema: “Karamu zao na ziwe mtego wa kuwanasa, na kitu cha kuwakwaza waanguke na kuadhibiwa, 10 Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona, na migongo yao ipinde kwa taabu daima.”

Kurejeshwa Kwa Waisraeli

11 Nauliza tena, je, Waisraeli walipojikwaa walianguka na kuangamia kabisa? La sivyo! Lakini kwa sababu ya uhalifu wao, wokovu umewafikia watu wa mataifa mengine, ili Waisraeli waone wivu. 12 Ikiwa uhalifu wao umeleta utajiri mkubwa kwa ulimwe ngu, na kama kuanguka kwao kumeleta utajiri kwa watu wasiomjua Mungu, basi Waisraeli wote watakapoongoka itakuwa ni baraka kub wa zaidi.

13 Sasa ninasema nanyi watu wa mataifa mengine. Mimi ni mtume kwa watu wa mataifa na ninajivunia huduma hiyo 14 ili kuwafanya Wayahudi wenzangu waone wivu, na hivyo niwaokoe baadhi yao. 15 Kwa kuwa ikiwa kukataliwa kwao kumefanya ulimwengu wote upatanishwe na Mungu, kuokolewa kwao je, si kutakuwa ni uhai kutoka kwa wafu? 16 Na kama sehemu ya kwanza ya unga ulioumuliwa ni wakfu, basi unga wote ni wakfu; na kama shina ni wakfu, matawi nayo yatakuwa wakfu.

17 Lakini kama baadhi ya matawi yamekatwa, na ninyi kama mizeituni mwitu mkapandwa katika shina, mkashiriki pamoja na matawi mengine chakula kutoka katika shina la mzeituni, 18 msi jivune mbele ya hayo matawi. Kama mkijisifu mkumbuke kuwa si ninyi mnaoshikilia shina, bali ni shina linalowashikilia ninyi. 19 Pengine mtasema, “Matawi yalikatwa ili nipate nafasi ya kupandikizwa katika shina.” 20 Hii ni kweli. Lakini kumbuka kuwa matawi hayo yalikatwa kwa sababu ya kutokuamini; na wewe umesimama imara kwa sababu ya imani. Kwa hiyo usijisifu, bali ujinyenyekeze na kuogopa. 21 Kwa maana kama Mungu hakuyahurumia matawi ya asili, hatakuacha wewe, atakuondoa. 22 Tafakari basi kuhusu wema na ukali wa Mungu. Yeye ni mkali kwa wale walio anguka, bali amekuonyesha wewe wema wake, kama utadumu katika wema wake. Vinginevyo, na wewe utakatiliwa mbali. 23 Na hata hao Waisraeli, kama wakiacha kudumu katika kutokuamini kwao, atawar udisha kwenye shina, kwa maana Mungu anao uwezo wa kuwarejesha. 24 Ikiwa ninyi mmekatwa kutoka katika mizeituni mwitu, na ki nyume cha asilia mkapandikizwa kwenye mzeituni uliopandwa, ita kuwa ni rahisi kiasi gani matawi haya ya asili kurejeshwa kwenye shina lake?

Huruma Ya Mungu Ni Kwa Wote

25 Ndugu zangu, napenda mfahamu siri hii, msije mkaanza kujiona. Waisraeli wamekuwa na mioyo migumu kwa kiasi fulani mpaka idadi kamili ya watu wa mataifa mengine watakapoamini. 26 Na ndipo Waisrael wote wataokoka kama ilivyoandikwa, “Mko mbozi atakuja kutoka Sayuni, na kuuondoa uasi wote kutoka katika uzao wa Yakobo. 27 Na hii itakuwa ni agano langu nao, nitakapoondoa dhambi zao.”

28 Basi Waisraeli ni maadui wa Mungu kwa sababu ya Injili. Hii ni kwa faida yenu. Lakini kuhusu uchaguzi, Waisraeli bado ni wapendwa wa Mungu kwa sababu ya ahadi yake kwa Abrahmu, Isaki na Yakobo. 29 Kwa maana karama za Mungu na wito wake hazifutiki. 30 Kama ninyi zamani mlivyokuwa mmemwasi Mungu na sasa mmepokea rehema kwa sababu ya kutokutii kwao, 31 hivyo nao Waisraeli wamekuwa waasi kwa ajili ya rehema mliyopata kutoka kwa Mungu, ili wao pia wapate rehema. 32 Kwa maana Mungu amewaachia wana damu wote wawe katika uasi, ili aweze kuwahurumia wote.

Wimbo Wa Shukrani

33 Jinsi utajiri wa Mungu ulivyo mkuu! Hekima yake na maarifa yake hayana mwisho. Njia zake na maamuzi yake hayachu nguziki! 34 Kwa maana ni nani amepata kufahamu mawazo ya Mungu au kuwa mshauri wake? 35 Au ni nani amewahi kumpa cho chote ili arudishiwe? 36 Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake na vipo kwa ajili yake na vyote vinadumu kwake. Utukufu ni wake milele. Amina.

Nafasi Ya Pekee Ya Waisraeli

Ninasema kweli katika Kristo na dhamiri yangu inanishuhudia kwa njia ya Roho Mtakatifu kuwa sisemi uongo. Nina huzuni sana na uchungu usiokwisha moyoni mwangu. Kwa maana ningetamani hata mimi nilaaniwe na kutengwa na Kristo kama kufanya hivyo kungeweza kuwasaidia ndugu zangu tulio wa kabila moja. Nazungumza kuhusu Waisraeli ambao Mungu aliwateua kuwa wana wake, wakapewa utukufu wake, maagano yake, sheria yake, ibada ya kweli, na ahadi zake. Wao ni wa uzao wa mababu wa kwanza, na katika taifa lao Kristo alitoka kama mwanadamu; yeye ambaye ni Mungu aliye juu ya vyote, atukuzwaye milele! Amina.

Lakini hii haina maana kwamba ahadi ya Mungu kwa wana wa Israeli imeshindwa. Kwa maana si wote ambao ni wa uzao wa Israeli ambao ni wa Israeli. Wala si wazaliwa wote wa kizazi cha Abra hamu ambao ni watoto wake. Ahadi ya Mungu kwa Abrahamu ilikuwa: “Watoto wako watatoka katika uzao wa Isaki.” Kwa maneno men gine, si wale watoto waliozaliwa na Ibrahimu kimwili ambao ni wana wa Mungu; bali ni wale watoto wa ahadi ambao wanahesabiwa kuwa kizazi cha Abrahamu. Kwa maana ahadi yenyewe ilisema, “Nitarudi tena wakati kama huu na Sara atapata mtoto wa kiume.”

10 Na si hivyo tu bali pia wakati Rebeka alipozaa watoto na mume mmoja, Isaki, 11 hata kabla watoto wake mapacha hawajazal iwa wala kutenda jema au baya ili mpango wa Mungu wa kuchagua uendelee, si kwa kutegemea matendo mema bali kwa kufuatana na wito wake - 12 Rebeka aliambiwa, “Mkubwa atamhudumia mdogo.” 13 Kama Maandiko yasemavyo: “Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia.”

Mungu Hana Upendeleo

14 Tusemeje basi? Kwamba Mungu ana upendeleo? La, sivyo. 15 Kwa maana Mungu alimwambia Musa, “Nitamrehemu nipendaye kumrehemu; na nitamhurumia nipendaye kumhurumia.” 16 Kwa hiyo haitegemei mapenzi ya mtu au jitihada ya mtu, bali hutegemea huruma ya Mungu. 17 Kwa maana katika Maandiko Farao anaambiwa, “Nilikuinua kwa makusudi ya kudhihirisha nguvu zangu kwako na jina langu lipate kutangazwa duniani pote.” 18 Kwa hiyo basi, Mungu humhurumia mtu ye yote apendaye kumhurumia na huufanya mgumu moyo wa mtu ye yote atakaye.

19 Bila shaka mtaniuliza, “Kama ni hivyo, kwa nini Mungu anatulaumu? Kwa maana ni nani awezaye kushindana na mapenzi yake? 20 Lakini wewe mwanadamu, una haki gani ya kumhoji Mungu? Je, kilichotengenezwa kinaweza kumwuliza aliyekitengeneza, “Kwa nini umenitengeneza hivi?” 21 Je, mfinyanzi hana haki ya kufa nya apendavyo na udongo wake? Je, si anaweza kabisa kutumia sehemu ya udongo huo kutengeneza chombo kimoja kitumikacho kwa kupamba na kutoka katika udongo huo huo akatengeneza kingine kwa matumizi ya kawaida?

22 Tunajuaje kama Mungu, kwa kutaka kuonyesha ghadhabu yake na nguvu yake, amewavumilia kwa uvumilivu mkuu wale waliomkasi risha, ambao wameandaliwa kuangamizwa? 23 Na tunajuaje kama Mungu alifanya hivi ili kuwadhihirishia utajiri wa utukufu wake wale anaowahurumia, ambao aliwaandaa tangu mwanzo kupokea utu kufu? 24 Na sisi ndio hao walioitwa, si kutoka kwa Wayahudi tu bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.

Yote Yalitabiriwa Katika Maandiko

25 Hivi ndivyo Mungu asemavyo katika kitabu cha Hosea, “Wale ambao hawakuwa watu wangu, nitawaita ‘watu wangu,’ na wale ambao hawakuwa wapendwa wangu, nitawaita ‘wapendwa wangu’.” 26 Na pale pale walipoambiwa,“Ninyi si ‘watu wangu,’ ndipo watakapoitwa, ‘Wana wa Mungu aliye hai’.” 27 Na Isaya anasema hivi kuhusu Israeli: “Ijapokuwa wana wa Israeli watakuwa wengi kama mchanga wa bahari, ni wachache tu miongoni mwao watakaooko lewa;

28 kwa maana Mungu ataitekeleza hukumu yakejuu ya ulimwengu mara moja na kuikamilisha.” 29 Na tena kama alivyotabiri Isaya,“Kama Bwana wa majeshi asingetuachia uzao, tungalikuwa kama Sodoma, na kufanywa kama Gomora.”

30 Kwa hiyo tusemeje basi? Watu wa mataifa ambao hawakuta futa kupata haki wamepewa haki kwa njia ya imani. 31 Lakini Waisraeli ambao wametafuta kupata haki kwa msingi wa sheria, hawakuipata kwa maana hawakutimiza sheria. 32 Kwa nini? Kwa sababu hawakuitafuta kwa imani bali kwa kutegemea matendo. Wali jikwaa kwenye lile ‘jiwe la kujikwaa.’ 33 Kama ilivyoandikwa kwe nye Maandiko,“Tazama naweka jiwe huko Sayuni ambalo linawafanya watu kujikwaa na mwamba utakaowaangusha, na wale watakaomtegemea hawataaibika kamwe.”