Warumi 7
Neno: Bibilia Takatifu
Mkristo Hafungwi Na Sheria
7 Ndugu zangu, kwa kuwa sasa ninasema na wale wanaoifahamu sheria, bila shaka mnaelewa kwamba mtu akifa hafungwi tena na sheria. 2 Kwa mfano, mwanamke aliyeolewa hufungwa kisheria kwa mumewe wakati wote mumewe akiwa hai. Lakini mumewe akifa mwanamke huyo hafungwi tena na sheria ya ndoa. 3 Endapo mwanamke huyo ataishi namwanaume mwingine wakati mumewe yu hai, ataitwa mzinzi. Lakini mumewe akifa, mwanamke huyo hafungwi tena na she ria ya ndoa, na akiolewa na mtu mwingine haitwi mzinzi.
Kazi Ya Sheria
4 Kadhalika ndugu zangu, ninyi pia mmekufa kuhusu maagizo ya sheria kwa njia ya mwili wa Kristo. Sasa ninyi ni mali yake yeye aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, ili tumzalie Mungu matunda. 5 Tulipokuwa tukitawaliwa na hali yetu ya dhambi, tamaa zetu za dhambi zikiwa zinachochewa na sheria, zilikuwa zikifanya kazi katika miili yetu, tukatumikishwa katika huduma ya dhambi ambayo matunda yake ni kifo. 6 Lakini sasa tumekuwa huru kutoka katika kifungo cha sheria kwa kuwa tumekufa kuhusu yale mambo yaliyotu funga, ili tuhudumu katika maisha mapya ya Roho na wala si katika ile njia ya zamani ya sheria iliyoandikwa.
7 Tusemeje basi? Kwamba sheria ni dhambi? La, sivyo! Kama isingekuwapo sheria, nisingalifahamu dhambi ni nini. Hakika nisi ngalijua tamaa ni nini kama sheria haikusema, “Usitamani.” 8 Lakini dhambi ilipata nafasi katika amri hii ikazaa ndani yangu kila aina ya tamaa. Kwa maana pasipo sheria, dhambi ime kufa. 9 Kabla ya kuwapo sheria, nilikuwa hai pasipo sheria, lakini amri ilipowasili dhambi nayo ilikuwa hai, nami nikafa. 10 Ile amri iliyokusudiwa kuleta uzima, ilileta kifo. 11 Dhambi ilipata nafasi katika amri, ikanidanganya, na kwa kutumia amri, ikaniletea kifo.
12 Kwa hiyo sheria yenyewe ni takatifu na amri ni takatifu, na ya haki, tena ni njema.
13 Je, hii ina maana kwamba sheria ambayo ni njema ilinile tea kifo? La, sivyo. Lakini ili dhambi itambuliwe kuwa ni dhambi, iliniletea kifo kwa njia ya sheria ambayo ni nzuri; kusudi kwa njia ya sheria, dhambi ionekane kuwa mbaya kabisa.
Mgongano Kati Ya Mwili Na Roho
14 Tunafahamu kwamba sheria ni ya kiroho. Lakini mimi si wa kiroho; mimi nimeuzwa utumwani, ni mtumwa wa dhambi. 15 Sielewi nitendalo: kwa maana lile ninalotaka kulifanya, sifanyi; badala yake, ninafanya lile ambalo nachukia kulifanya. 16 Kwa hiyo kama ninafanya lile nisilopenda kufanya, hii ina maana kwamba nakubali kuwa sheria ni njema. 17 Basi, kwa kweli si mimi hasa nitendaye lile nisilolipenda bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu. 18 Kwa maana ninafahamu kwamba hakuna wema wo wote ndani yangu mimi, yaani katika mwili wangu wa asili. Ingawa nina nia ya kutenda lililo jema, lakini ninashindwa kulitenda. 19 Sitendi lile jema nipendalo bali lile ovu nisilopenda, ndilo nitendalo. 20 Basi kama ninafanya lile nisilopenda kufanya, si mimi tena nifanyaye hivyo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu.
21 Kwa hiyo imekuwa kama ni sheria: kila ninapotaka kufanya jambo jema, jambo ovu hujitokeza. 22 Kwa maana ndani yangu ninaifurahia sheria ya Mungu. 23 Lakini ninaona kuna sheria nyin gine mwilini mwangu inayopingana na ile sheria ninayoikubali akilini mwangu. Sheria hii inanifanya kuwa mateka wa sheria ya dhambi ambayo inafanya kazi mwilini mwangu.
24 Ole wangu, mimi mnyonge! Ni nani atakayeniokoa na huu mwili wa kifo? 25 Ninamshukuru Mungu kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa hiyo basi, mimi kwa moyo wangu, ninaitumikia sheria ya Mungu, lakini kwa mwili wangu wa asili ninaitumikia sheria ya dhambi.
罗马书 7
Chinese Contemporary Bible (Simplified)
婚姻关系的例子
7 弟兄姊妹,我现在对那些熟悉律法的人说:你们难道不知道律法只在人活着的时候管辖人吗? 2 比方说,一个妇人结了婚,只要丈夫还在世,她就受律法的约束要与丈夫在一起。如果丈夫死了,她就脱离了与丈夫的婚姻关系。 3 丈夫还活着的时候,她若与别的男人发生性关系,便算淫妇。丈夫若死了,她就脱离了与丈夫的婚姻关系,即使改嫁,也不是淫妇。
4 我的弟兄姊妹,同样,你们借着基督的身体向着律法也死了,使你们可以归于那位从死里复活的基督,好为上帝结果子。 5 从前我们受自己罪恶本性[a]的控制,因律法而激发的罪恶欲望在我们身上发作,以致结出死亡的果子。 6 但现在,我们既然向着一度捆绑我们的律法死了,就脱离了律法的控制,能够以圣灵所赐的新样式,而不是以拘守教条的旧样式事奉上帝。
律法使人知罪
7 那么,我们可以说律法本身是罪吗?当然不是!没有律法,我们就不知道什么是罪。律法若不说“不可贪心”,我就不知道什么是贪心。 8 然而,罪却趁机利用诫命在我里面生出各种贪念,因为没有律法,罪是死的。 9 我没认识律法之前是活的,但律法来了之后,罪就活了,而我却死了。 10 我发现那本来要使人活的诫命反而叫我死, 11 因为罪利用诫命趁机引诱我,而且借着诫命杀了我。
12 其实律法是圣洁的,诫命也是圣洁、公义、良善的。 13 既然如此,难道是良善的诫命叫我死吗?当然不是!是罪借着良善的诫命叫我死。这样,罪借着诫命叫我死就显出它实在是邪恶至极!
善恶相争
14 我们知道律法是属灵的,我却属乎肉体,已经卖给罪做奴隶了。 15 我不明白自己的所作所为,因为我想做的,我做不到;而我憎恨的恶事,我偏偏去做! 16 既然我不想做的,我反倒去做,我就得承认律法是好的。 17 其实那并不是我做的,而是住在我里面的罪做的。 18 我也知道,在我的罪恶本性里面毫无良善,我有行善的心愿,却没有行善的力量。 19 我想行善,却不能行;我不想作恶,反倒去作。 20 如果我不想做的,我反倒去做,这就不是我自己做的,而是住在我里面的罪做的。
21 因此,我发现一个律:我想行善的时候,恶就不放过我。 22 按着我里面的意思[b],我喜爱上帝的律。 23 然而,我发觉在我身体内另有一个律和我心中的律作战,将我俘虏,使我服从身体内犯罪的律。 24 我真是苦啊!谁能救我脱离这个被死亡控制的身体呢? 25 感谢上帝,祂借着我们的主耶稣基督救了我!这样看来,我的内心服从上帝的律法,但我罪恶的本性却服从犯罪的律。
Copyright © 1989 by Biblica
Chinese Contemporary Bible Copyright © 1979, 2005, 2007, 2011 by Biblica® Used by permission. All rights reserved worldwide.