Warumi 7
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Kielelezo Kutoka Katika Ndoa
7 Ndugu zangu, ninyi nyote mnailewa sheria ya Musa. Hivyo kwa hakika mnafahamu kuwa sheria huwatawala watu wanapokuwa hai tu. 2 Ni kama ambavyo sheria kuhusu ndoa inavyosema: ni lazima mwanamke abaki katika ndoa mume wake akiwa hai. Lakini mume wake akifa, atakuwa amewekwa huru kutoka katika sheria ya ndoa. 3 Iwapo ataolewa na mwanaume mwingine, mume wake akiwa angali hai, sheria inasema kuwa ana hatia ya uzinzi. Lakini mumewe akifa, atakuwa amewekwa huru kutoka katika sheria ya ndoa. Hivyo akiolewa na mwanaume mwingine baada ya mumewe kufa, hatakuwa na hatia ya uzinzi.
4 Kwa njia hiyo hiyo, kaka na dada zangu, mliwekwa huru kutoka katika sheria utu wenu wa zamani ulipokufa pamoja na Kristo. Sasa ninyi ni mali yake yeye yule aliyefufuliwa kutoka kwa wafu. Sote ni mali ya Kristo ili tutumike kwa ajili ya huduma kwa Mungu. 5 Hapo zamani tulitawaliwa na udhaifu wetu wa kibinadamu. Sheria ilitufanya tutake kutenda dhambi. Na tamaa hizo za dhambi ziliitawala miili yetu, na yale tuliyofanya yalituletea mauti ya rohoni. 6 Sasa, kama watu waliokufa, tuko huru kutoka katika sheria iliyotushikilia kama wafungwa. Hivyo hatumtumikii Mungu tena kwa jinsi ya zamani, kwa sheria zilizoandikwa. Sasa tunamtumikia Mungu kwa namna mpya, kwa Roho.
Dhambi na Sheria
7 Mnaweza kudhani ninasema ya kwamba dhambi na sheria vinafanana. Sisemi hivyo. Lakini sheria ilikuwa njia pekee ya kunifundisha maana ya dhambi. Nisingeweza kujua kwamba ni kosa kutamani kitu kisichokuwa changu. Lakini sheria inasema, “Usitamani mali ya mtu mwingine.”(A) 8 Na dhambi kwa kutumia amri hiyo, ikanifanya nitamani kila kitu kisichokuwa changu. Hivyo dhambi ilikuja kwangu kutokana na amri hiyo. Lakini bila sheria, dhambi imekufa na haina nguvu. 9 Kabla sijaijua sheria, nilikuwa hai. Lakini nilipoijua sheria, dhambi ikaanza kuishi ndani yangu, 10 na hiyo ikawa na maana ya kifo kwangu. Amri ilikusudiwa kuleta uzima, lakini kwangu iliniletea kifo. 11 Dhambi ilipata njia ya kunidanganya kwa kutumia amri ili nife.
12 Hivyo, sheria ni takatifu na amri ni takatifu, sahihi na nzuri. 13 Je, hii ina maana kuwa kitu ambacho ni kizuri kiliniletea kifo? Hapana, ni dhambi iliyoitumia amri nzuri ndiyo iliyoniletea kifo. Hii inaonesha kwa hakika kuwa dhambi ni dhambi. Dhambi inaweza kutumia amri iliyo nzuri na kuleta matokeo yanayoonesha ubaya wake mkubwa.
Vita ndani Yetu
14 Tunafahamu kuwa sheria ni ya rohoni, lakini mimi si wa rohoni. Mimi ni mwanadamu hasa. Dhambi inanitawala kana kwamba mimi ni mtumwa wake. 15 Sielewi ni kwa nini ninatenda jinsi ninavyotenda. Sitendi mema ninayotaka kuyatenda, bali ninatenda maovu ninayoyachukia. 16 Na ikiwa ninatenda kile nisichotaka kutenda, inamaanisha kuwa ninakubali kuwa sheria ni njema. 17 Lakini kwa hakika siyo mimi mwenyewe ninayetenda maovu. Bali dhambi inayokaa ndani yangu ndiyo inatenda hayo. 18 Ndiyo, ninajua kuwa hakuna kitu chema kinachoishi ndani yangu, nina maana kuwa hakuna kitu chema kinachoishi ndani yangu kisichokuwa cha rohoni. 19 Sitendi mema ninayotaka nitende. Ninatenda maovu nisiyotaka kutenda. 20 Hivyo ikiwa ninatenda yale nisiyotaka kutenda, hakika si mimi ninayeyatenda hayo. Bali dhambi inayoishi ndani yangu ndiyo inayotenda.
21 Hivyo nimejifunza hivi kuhusu sheria: Ninapotaka kutenda mema ambayo sheria inaamrisha, uovu unakuwa hapo hapo pamoja nami. 22 Moyoni mwangu nafurahi kuifuata sheria ya Mungu. 23 Lakini naiona “sheria” nyingine ikitenda kazi ndani yangu, nayo imo vitani dhidi ya sheria inayokubalika akilini mwangu. “Sheria” hii nyingine ni utawala wa dhambi inayonishinda na inanifanya kuwa mfungwa wake. 24 Mimi ni mtu mwenye taabu kiasi gani! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu unaoniletea kifo? 25 Namshukuru Mungu kwa wokovu wake kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu! Hivyo katika ufahamu wangu mimi ni mtumwa wa sheria ya Mungu, lakini katika udhaifu wangu wa kibinadamu mimi ni mtumwa wa sheria ya dhambi.
Romans 7
International Children’s Bible
An Example from Marriage
7 Brothers, all of you understand the law of Moses. So surely you know that the law rules over a person only while he is alive. 2 For example, a woman must stay married to her husband as long as he is alive. But if her husband dies, then she is free from the law of marriage. 3 But if she marries another man while her husband is still alive, the law says she is guilty of adultery. But if her husband dies, then the woman is free from the law of marriage. So if she marries another man after her husband dies, she is not guilty of adultery.
4 In the same way, my brothers, your old selves died, and you became free from the law through the body of Christ. Now you belong to someone else. You belong to the One who was raised from death. We belong to Christ so that we can be used in service to God. 5 In the past, we were ruled by our sinful selves. The law made us want to do sinful things. And those sinful things we wanted to do controlled our bodies, so that the things we did were only bringing us death. 6 In the past, the law held us like prisoners. But our old selves died, and we were made free from the law. So now we serve God in a new way, not in the old way with written rules. Now we serve God in the new way, with the Spirit.
Our Fight Against Sin
7 You might think that I am saying that sin and the law are the same thing. That is not true. But the law was the only way I could learn what sin meant. I would never have known what it means to want something wrong if the law had not said, “You must not want to take your neighbor’s things.”[a] 8 And sin found a way to use that command and cause me to want every kind of wrong thing. So sin came to me because of that command. But without the law, sin has no power. 9 I was alive without the law before I knew the law. But when the law’s command came to me, then sin began to live. 10 And I died because of sin. The command was meant to bring life, but for me that command brought death. 11 Sin found a way to fool me by using the command. Sin used the command to make me die.
12 So the law is holy, and the command is holy and right and good. 13 Does this mean that something that is good brought death to me? No! Sin used something that is good to bring death to me. This happened so that I could see what sin is really like. The command was used to show that sin is something very evil.
The War Within Man
14 We know that the law is spiritual. But I am not spiritual. Sin rules me as if I were its slave. 15 I do not understand the things I do. I do not do the good things I want to do. And I do the bad things I hate to do. 16 And if I do not want to do the bad things I do, then that means that I agree that the law is good. 17 But I am not really the one who is doing these bad things. It is sin living in me that does these things. 18 Yes, I know that nothing good lives in me—I mean nothing good lives in the part of me that is earthly and sinful. I want to do the things that are good. But I do not do them. 19 I do not do the good things that I want to do. I do the bad things that I do not want to do. 20 So if I do things I do not want to do, then I am not the one doing those things. It is sin living in me that does those bad things.
21 So I have learned this rule: When I want to do good, evil is there with me. 22 In my mind, I am happy with God’s law. 23 But I see another law working in my body. That law makes war against the law that my mind accepts. That other law working in my body is the law of sin, and that law makes me its prisoner. 24 What a miserable man I am! Who will save me from this body that brings me death? 25 God will. I thank him for saving me through Jesus Christ our Lord!
So in my mind I am a slave to God’s law. But in my sinful self I am a slave to the law of sin.
Footnotes
- 7:7 “You . . . things.” Quotation from Exodus 20:13, 15–17.
© 2017 Bible League International
The Holy Bible, International Children’s Bible® Copyright© 1986, 1988, 1999, 2015 by Thomas Nelson. Used by permission.
