Warumi 6
Neno: Bibilia Takatifu
Uhai Katika Kristo
6 Tusemeje basi? Tuendelee kutenda dhambi ili neema izidi kuongezeka? 2 Hata kidogo! Itawezekanaje sisi tuliokufa kwa mambo ya dhambi, tuendelee tena kuishi humo? 3 Au hamfahamu kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika kifo chake? 4 Kwa hiyo tulikufa na kuzikwa naye kwa njia ya ubatizo ili kama vile Kristo alivyofufuliwa kutoka kwa wafu kwa nguvu na utukufu wa Baba, sisi pia tupate kuishi maisha mapya.
5 Kwa maana ikiwa tumeunganika naye katika kifo chake, basi tutaunganika naye katika kufufuka kwake. 6 Tunafahamu kwamba mwili wetu wa asili ulisulubiwa msalabani pamoja na Kristo ili mwili wetu wa dhambi uharibiwe kabisa na tusiwe tena watumwa wa dhambi. 7 Kwa maana mtu anapokufa anakuwa huru na mambo ya dhambi. 8 Lakini ikiwa tumekufa na Kristo, tunaamini kwamba pia tutaishi pamoja naye. 9 Kama tujuavyo, Kristo alikwisha kufufu liwa kutoka kwa wafu kwa hiyo hafi tena; kifo hakina mamlaka juu yake tena. 10 Alikufa kwa ajili ya dhambi mara moja tu, lakini maisha anayoishi anamwishia Mungu.
11 Kwa hiyo ninyi pia hamna budi kujihesabu kuwa wafu kwa mambo ya dhambi bali hai kwa Mungu mkiwa ndani ya Kristo Yesu.
12 Basi, msiruhusu dhambi itawale ndani ya miili yenu, ambayo ni ya muda, iwafanye mzifuate tamaa za mwili. 13 Msiku bali kutoa sehemu yo yote ya miili yenu itumike kama vyombo vya uovu kutenda dhambi. Bali jitoeni kwa Mungu kama watu waliotolewa kutoka katika kifo wakaingizwa uzimani. Pia toeni sehemu zote za miili yenu zitumike kama vyombo vya haki. 14 Kwa maana dhambi haitakuwa na mamlaka juu yenu kwa sababu hamtawaliwi na sheria bali mnatawaliwa na neema. Watumwa Wa Haki
15 Tufanyeje basi? Tuendelee kutenda dhambi kwa kuwa hatutawa liwi na sheria bali tuko chini ya neema? La , sivyo! 16 Hamfahamu kuwa kama mkijitoa kumtumikia mtu na kumtii kama watumwa basi mnakuwa watumwa wa huyo mnayemtii? Mnaweza kuwa watumwa wa dhambi ambayo matokeo yake ni mauti au mnaweza kuwa watumwa wa utii ambao huleta haki. 17 Lakini Mungu ashukuriwe kwa kuwa ninyi ambao mlikuwa watumwa wa dhambi mmetii kwa moyo wote mafundi sho mliyopewa. 18 Mmewekwa huru, mbali na dhambi na mmekuwa watumwa wa haki. 19 Ninatumia mifano ya kibinadamu kwa sababu ya upungufu wenu wa hali ya asili. Kama mlivyokuwa mkiitoa miili yenu kwa ajili ya mambo ya uchafu na uovu uliokuwa ukiongezeka zaidi na zaidi, sasa itoeni miili yenu itumike kwa ajili ya haki na utakatifu.
20 Mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa hamtawaliwi na haki. 21 Lakini mlipata faida gani kwa mambo hayo ambayo sasa mnayaonea aibu? Mwisho wa mambo hayo ni kifo. 22 Lakini sasa kwa kuwa mmewekwa huru kutokana na dhambi na mmekuwa watumwa wa Mungu, faida mnayopata ni utakaso, na hatimaye, uzima wa milele. 23 Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.
罗马书 6
Chinese Contemporary Bible (Simplified)
与基督同死同活
6 那么,我们该怎么说呢?我们可以继续犯罪,使恩典显得更丰富吗? 2 绝不可以!我们既然向罪死了,岂可继续活在罪中? 3 难道你们不知道,我们受洗归属基督耶稣是和祂一同死吗? 4 我们借着洗礼和祂一同死了,埋葬了,这样我们的一举一动可以有新生命的样式,正如基督借着父的荣耀从死里复活一样。
5 如果我们和基督一同死了,也必和祂一同复活。 6 我们知道,我们的旧人已经和祂一同钉在十字架上,使辖制我们身体的罪失去力量,使我们不再做罪的奴隶。 7 因为人一旦死了,便脱离了罪。
8 如果我们与基督同死,相信也必与祂同活。 9 因为我们知道,基督既然从死里复活了,就不会再死,死亡也不能再控制祂。 10 祂死,是向罪死,只死一次;祂活,却是向上帝永远活着。 11 这样,你们应当看自己是向罪死了,但向上帝则看自己是活在基督耶稣里。
12 所以,不要让罪辖制你们必死的身体,使你们顺从身体的私欲; 13 也不要将你们的身体献给罪作不义的工具,而是要像一个从死里复活的人将自己奉献给上帝,把身体献给上帝作义的工具。 14 罪不能再主宰你们,因为你们已经不在律法之下,而是在恩典之中。
做义的奴仆
15 那么,我们在恩典之中,不在律法之下,就可以任意犯罪吗?绝不可以! 16 你们难道不明白吗?你们献身给谁、服从谁,就是谁的奴隶。做罪的奴隶,结局是死亡;做上帝的奴仆,就被称为义人。 17 感谢上帝!你们从前虽然做过罪的奴隶,现在却衷心服从了所传给你们的教导, 18 从罪中得到释放,成为义的奴仆。
19 因为你们有人性的软弱,我就从人的立场向你们解释。以前你们将身体献给肮脏不法的事,任其奴役,助长不法。现在你们要将身体奉献给义,为义效劳,成为圣洁的人。 20 你们做罪的奴隶时,不受义的约束, 21 做了现在想起来也觉得羞耻的事,得到了什么益处呢?那些事只能导致死亡! 22 但现在你们已从罪中得到释放,做了上帝的奴仆,这样会使你们圣洁,最终得到永生。 23 因为罪的代价就是死亡,而上帝借着主基督耶稣赐下的礼物则是永生。
Copyright © 1989 by Biblica
Chinese Contemporary Bible Copyright © 1979, 2005, 2007, 2011 by Biblica® Used by permission. All rights reserved worldwide.