罗马书 3
Chinese Contemporary Bible (Simplified)
3 那么,犹太人有什么长处呢?割礼有什么价值呢? 2 其实益处非常多!首先,上帝的圣言托付给了犹太人。 3 虽然有些人不相信,但那有什么关系呢?难道上帝的信实可靠会因他们的不信而化为无有吗? 4 当然不会!纵然人人都撒谎,上帝仍然真实可靠。正如圣经上说:
“你的判语证明你是公义的;
你虽被人控告,却终必得胜。”
5 我姑且用人的观点说:“如果我们的不义可以反衬出上帝的公义,我们该做何论?上帝向我们发怒是祂不公正吗?” 6 当然不是!若是这样,上帝怎么能审判这世界呢? 7 你们又说:“如果我们的虚谎凸显出上帝的真实,增加祂的荣耀,为什么祂还要把我们当作罪人审判呢?” 8 为什么你们不干脆说:“我们作恶吧,好成就善事”?有人毁谤我们,说我们传这种道理。这些人受审判是罪有应得!
没有义人
9 那么,我们犹太人比别人优越吗?绝对不是!我们已经说过,无论是犹太人还是希腊人,所有的人都身陷罪中。 10 正如圣经上说:
“没有义人,一个也没有,
11 没有人明白,没有人寻求上帝。
12 人人偏离正路,变得毫无价值。
没有人行善,一个也没有。
13 他们的喉咙是敞开的坟墓,
舌头上尽是诡诈,
嘴唇有蛇的毒液,
14 满口咒诅,言语恶毒;
15 杀人流血,脚步飞快;
16 所到之处,大肆毁灭;
17 平安之路,他们未曾知道;
18 他们眼中毫无对上帝的畏惧。”
19 我们知道律法所讲的都是针对律法之下的人,好叫所有的人都无话可说,使全世界都伏在上帝的审判之下。 20 因为无人能够靠遵行律法而被上帝视为义人,律法的本意是要使人知罪。
因信称义
21 但如今,上帝的义在律法以外显明出来,有律法和众先知做见证。 22 人只要信耶稣基督,就可以被上帝称为义人,没有一个人例外。 23 因为世人都犯了罪,亏欠上帝的荣耀, 24 但蒙上帝的恩典,靠着基督耶稣的救赎,世人被无条件地称为义人。 25 上帝使基督耶稣成为赎罪祭,以便人借着相信耶稣的宝血可以得到赦免。这是为了显明上帝的义,因为祂用忍耐的心宽容人过去的罪, 26 好在现今显明祂的义,使人知道祂是公义的,祂也称信耶稣的为义人。
27 既然如此,我们哪里能夸口呢?当然没有可夸的。靠什么方法让人不能夸口呢?靠遵行律法吗?不是!是靠信主的方法。 28 因为我们坚信人被称为义人是借着信,不是靠遵行律法。 29 难道上帝只是犹太人的上帝吗?祂不也是外族人的上帝吗?祂当然也是外族人的上帝。 30 因为上帝只有一位,祂本着信称受割礼的人为义人,也本着信称未受割礼的人为义人。 31 这么说来,我们是借着信心废掉上帝的律法吗?当然不是!我们反倒是巩固律法。
Warumi 3
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
3 Je, Wayahudi wana upendeleo wowote kuliko wengine? Je, tohara yao inawasaidia lolote jema? 2 Ndiyo, Wayahudi wana upendeleo mwingi. Lililo muhimu zaidi ni kuwa: Mungu aliwaamini akawapa kazi ya kuzitangaza ahadi zake kwa watu wote. 3 Ni kweli kuwa baadhi ya Wayahudi hawakuwa waaminifu kufanya yale Mungu aliyotaka. Lakini je, hilo laweza kumzuia Mungu kutenda kwa uaminifu yale aliyoahidi? 4 Hapana! Hata ikiwa wengine wote watashindwa kutimiza ahadi zao, daima, Mungu atatekeleza aliyosema. Kama Maandiko yanavyosema kuhusu Mungu,
“Utathibitika kuwa mwenye haki kwa maneno yako,
na utashinda utakaposhitakiwa na watu.”(A)
5 Lakini hivi ndivyo wengine hufikiri: Tunapotenda mabaya, inaonesha wazi kuwa Mungu ni wa haki. Je, tunaweza kusema kwamba Mungu hatutendei haki anapotuadhibu? 6 Hapana. Ikiwa Mungu si wa haki atawezaje kuuhukumu ulimwengu?
7 Ninaposema uongo, inamletea Mungu utukufu, kwa sababu uongo wangu hurahisisha ionekane kuwa yeye ni wa kweli. Hivyo kwa nini nihukumiwe kama mtenda dhambi? 8 Na kwa nini tusiseme, “Tufanye maovu ili jambo jema litokee humo.” Baadhi ya watu wanadai kuwa hivyo ndivyo tunavyofundisha! Wahukumiwe kwa kusema hivyo.
9 Je, sisi Wayahudi ni bora kuliko wengine? Hapana, nimekwishaonyesha kuwa watu wote, wawe Wayahudi au wasio Wayahudi, wako chini ya nguvu ya dhambi.
Watu Wote Wana Hatia
10 Kama Maandiko yanavyosema,
“Hakuna atendaye haki,
hakuna hata mmoja.
11 Hakuna hata mmoja anayeelewa,
hakuna anayetaka kumfuata Mungu.
12 Wote wamegeuka na kumwacha,
na hawana manufaa kwa yeyote.
Hakuna atendaye mema,
hakuna hata mmoja.”(B)
13 “Maneno yao ni ya hatari kama kaburi lililo wazi.
Wanatumia ndimi zao kwa kusema uongo.”(C)
“Maneno yao ni kama sumu ya nyoka.”(D)
14 “Midomo yao imejaa maneno ya laana na hasira.”(E)
15 “Nyakati zote wako tayari kuua mtu.
16 Kila wanakokwenda wanasababisha matatizo na uharibifu.
17 Hawajui jinsi ya kuishi kwa amani.”(F)
18 “Hawamheshimu wala kumcha Mungu.”(G)
19 Tunajua ya kwamba, kile ambacho sheria inasema ni kwa ajili ya wale waliopewa sheria. Hii inamaanisha kuwa watu wote, Wayahudi na wasio Wayahudi, hawana udhuru kwa matendo yao. Hivyo ulimwengu wote unasimama mbele za Mungu na lazima ujibu kwake. 20 Kwa sababu kufuata sheria hakumfanyi mtu akahesabiwa haki mbele za Mungu.[a] Sheria inatuonyesha dhambi zetu tu.
Mungu Anavyowafanya Watu Kuwa Wenye Haki
21 Lakini sasa Mungu ametuonesha jinsi alivyo mwema na mwaminifu. Alivyofanya haihusiani na sheria ingawa sheria na manabii walisema kuwa haya yangetokea. 22 Uaminifu wa wema wa Mungu umedhihirishwa kwetu kupitia imani katika[b] Yesu Kristo. Hufanya hivi kwa wote wanaomwamini Kristo. Kwa sababu kwa Mungu watu wote ni sawa. 23 Ndiyo, watu wote wametenda dhambi na wameshindwa kufikia kiwango cha utukufu wa Mungu kilichokusudiwa kwao. 24 Mungu ameamuru sisi sote tufunguliwe kutoka dhambini. Zawadi hii ya neema yake imekuja kwetu kupitia kile ambacho Kristo Yesu alikifanya ili tuwe huru. 25-26 Mungu alimtoa Yesu kama njia ya kusamehe dhambi za watu kupitia imani katika yeye. Mungu anasamehe watu kwa sababu sadaka ya damu ya Yesu iliwaweka huru na dhambi zao. Mungu alimtoa Yesu kuonesha kuwa hutenda haki na bila upendeleo. Alikuwa sahihi huko nyuma alipovumilia na hakuwaadhibu watu kwa sababu ya dhambi zao. Na katika wakati wetu bado anatenda haki. Mungu alifanya hili ili awahukumu watu pasipo kuwa na upendeleo na kumwesabia haki mtu yeyote aliye na imani katika Yesu.
27 Hivyo, sisi Wayahudi tuna nini cha kujivunia? Hatuna kitu. Mungu amefunga mlango kuzuia nje kiburi cha Kiyahudi. Sheria gani husema hivyo? Sheria inayohimiza matendo? Hapana, ni sheria inayosisitiza imani. 28 Ninamaanisha kuwa watu hufanyika wenye haki na kukubaliwa na Mungu kwa njia ya imani,[c] siyo kwa sababu ya yale wanayotenda ili kuifuata sheria. Hili ndilo tunaloamini. 29 Je, mnadhani kuwa Mungu ni Mungu wa Wayahudi tu? Je, yeye si Mungu wa watu wengine pia? Ndiyo, yeye ni Mungu wa wasio Wayahudi pia. 30 Kuna Mungu mmoja tu. Atawahesabia haki Wayahudi[d] kwa imani yao, na atawahesabia haki wasio Wayahudi[e] kwa imani yao. 31 Je, mnadhani kuwa tunaondoa sheria na kuweka imani hii? Hapana! Kwa kuifuata njia ya imani tunafanya kilichokusudiwa na sheria.
Chinese Contemporary Bible Copyright © 1979, 2005, 2007, 2011 by Biblica® Used by permission. All rights reserved worldwide.
© 2017 Bible League International