Warumi 3
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
3 Je, Wayahudi wana upendeleo wowote kuliko wengine? Je, tohara yao inawasaidia lolote jema? 2 Ndiyo, Wayahudi wana upendeleo mwingi. Lililo muhimu zaidi ni kuwa: Mungu aliwaamini akawapa kazi ya kuzitangaza ahadi zake kwa watu wote. 3 Ni kweli kuwa baadhi ya Wayahudi hawakuwa waaminifu kufanya yale Mungu aliyotaka. Lakini je, hilo laweza kumzuia Mungu kutenda kwa uaminifu yale aliyoahidi? 4 Hapana! Hata ikiwa wengine wote watashindwa kutimiza ahadi zao, daima, Mungu atatekeleza aliyosema. Kama Maandiko yanavyosema kuhusu Mungu,
“Utathibitika kuwa mwenye haki kwa maneno yako,
na utashinda utakaposhitakiwa na watu.”(A)
5 Lakini hivi ndivyo wengine hufikiri: Tunapotenda mabaya, inaonesha wazi kuwa Mungu ni wa haki. Je, tunaweza kusema kwamba Mungu hatutendei haki anapotuadhibu? 6 Hapana. Ikiwa Mungu si wa haki atawezaje kuuhukumu ulimwengu?
7 Ninaposema uongo, inamletea Mungu utukufu, kwa sababu uongo wangu hurahisisha ionekane kuwa yeye ni wa kweli. Hivyo kwa nini nihukumiwe kama mtenda dhambi? 8 Na kwa nini tusiseme, “Tufanye maovu ili jambo jema litokee humo.” Baadhi ya watu wanadai kuwa hivyo ndivyo tunavyofundisha! Wahukumiwe kwa kusema hivyo.
9 Je, sisi Wayahudi ni bora kuliko wengine? Hapana, nimekwishaonyesha kuwa watu wote, wawe Wayahudi au wasio Wayahudi, wako chini ya nguvu ya dhambi.
Watu Wote Wana Hatia
10 Kama Maandiko yanavyosema,
“Hakuna atendaye haki,
hakuna hata mmoja.
11 Hakuna hata mmoja anayeelewa,
hakuna anayetaka kumfuata Mungu.
12 Wote wamegeuka na kumwacha,
na hawana manufaa kwa yeyote.
Hakuna atendaye mema,
hakuna hata mmoja.”(B)
13 “Maneno yao ni ya hatari kama kaburi lililo wazi.
Wanatumia ndimi zao kwa kusema uongo.”(C)
“Maneno yao ni kama sumu ya nyoka.”(D)
14 “Midomo yao imejaa maneno ya laana na hasira.”(E)
15 “Nyakati zote wako tayari kuua mtu.
16 Kila wanakokwenda wanasababisha matatizo na uharibifu.
17 Hawajui jinsi ya kuishi kwa amani.”(F)
18 “Hawamheshimu wala kumcha Mungu.”(G)
19 Tunajua ya kwamba, kile ambacho sheria inasema ni kwa ajili ya wale waliopewa sheria. Hii inamaanisha kuwa watu wote, Wayahudi na wasio Wayahudi, hawana udhuru kwa matendo yao. Hivyo ulimwengu wote unasimama mbele za Mungu na lazima ujibu kwake. 20 Kwa sababu kufuata sheria hakumfanyi mtu akahesabiwa haki mbele za Mungu.[a] Sheria inatuonyesha dhambi zetu tu.
Mungu Anavyowafanya Watu Kuwa Wenye Haki
21 Lakini sasa Mungu ametuonesha jinsi alivyo mwema na mwaminifu. Alivyofanya haihusiani na sheria ingawa sheria na manabii walisema kuwa haya yangetokea. 22 Uaminifu wa wema wa Mungu umedhihirishwa kwetu kupitia imani katika[b] Yesu Kristo. Hufanya hivi kwa wote wanaomwamini Kristo. Kwa sababu kwa Mungu watu wote ni sawa. 23 Ndiyo, watu wote wametenda dhambi na wameshindwa kufikia kiwango cha utukufu wa Mungu kilichokusudiwa kwao. 24 Mungu ameamuru sisi sote tufunguliwe kutoka dhambini. Zawadi hii ya neema yake imekuja kwetu kupitia kile ambacho Kristo Yesu alikifanya ili tuwe huru. 25-26 Mungu alimtoa Yesu kama njia ya kusamehe dhambi za watu kupitia imani katika yeye. Mungu anasamehe watu kwa sababu sadaka ya damu ya Yesu iliwaweka huru na dhambi zao. Mungu alimtoa Yesu kuonesha kuwa hutenda haki na bila upendeleo. Alikuwa sahihi huko nyuma alipovumilia na hakuwaadhibu watu kwa sababu ya dhambi zao. Na katika wakati wetu bado anatenda haki. Mungu alifanya hili ili awahukumu watu pasipo kuwa na upendeleo na kumwesabia haki mtu yeyote aliye na imani katika Yesu.
27 Hivyo, sisi Wayahudi tuna nini cha kujivunia? Hatuna kitu. Mungu amefunga mlango kuzuia nje kiburi cha Kiyahudi. Sheria gani husema hivyo? Sheria inayohimiza matendo? Hapana, ni sheria inayosisitiza imani. 28 Ninamaanisha kuwa watu hufanyika wenye haki na kukubaliwa na Mungu kwa njia ya imani,[c] siyo kwa sababu ya yale wanayotenda ili kuifuata sheria. Hili ndilo tunaloamini. 29 Je, mnadhani kuwa Mungu ni Mungu wa Wayahudi tu? Je, yeye si Mungu wa watu wengine pia? Ndiyo, yeye ni Mungu wa wasio Wayahudi pia. 30 Kuna Mungu mmoja tu. Atawahesabia haki Wayahudi[d] kwa imani yao, na atawahesabia haki wasio Wayahudi[e] kwa imani yao. 31 Je, mnadhani kuwa tunaondoa sheria na kuweka imani hii? Hapana! Kwa kuifuata njia ya imani tunafanya kilichokusudiwa na sheria.
Romans 3
English Standard Version
God's Righteousness Upheld
3 Then what advantage has the Jew? Or what is the value of circumcision? 2 Much in every way. To begin with, (A)the Jews were entrusted with (B)the oracles of God. 3 (C)What if some were unfaithful? (D)Does their faithlessness nullify the faithfulness of God? 4 By no means! (E)Let God be true though (F)every one were a liar, as it is written,
5 But if our unrighteousness serves to show the righteousness of God, what shall we say? That God is unrighteous to inflict (I)wrath on us? ((J)I speak in a human way.) 6 By no means! For then how could (K)God judge the world? 7 But if through my lie God's truth abounds to his glory, (L)why am I still being condemned as a sinner? 8 And why not (M)do evil that good may come?—as some people slanderously charge us with saying. Their condemnation is just.
No One Is Righteous
9 What then? Are we Jews[a] any better off?[b] No, not at all. For we have already charged that all, both (N)Jews and (O)Greeks, are (P)under sin, 10 as it is written:
(Q)“None is righteous, no, not one;
11 no one understands;
no one seeks for God.
12 All have turned aside; together they have become worthless;
no one does good,
not even one.”
13 (R)“Their throat is (S)an open grave;
they use their tongues to deceive.”
(T)“The venom of asps is under their lips.”
14 (U)“Their mouth is full of curses and bitterness.”
15 (V)“Their feet are swift to shed blood;
16 in their paths are ruin and misery,
17 and (W)the way of peace they have not known.”
18 (X)“There is no fear of God before their eyes.”
19 Now we know that whatever (Y)the law says it speaks to those who are under the law, (Z)so that every mouth may be stopped, and (AA)the whole world may be held accountable to God. 20 For (AB)by works of the law no human being[c] will be justified in his sight, since (AC)through the law comes knowledge of sin.
The Righteousness of God Through Faith
21 But now (AD)the righteousness of God (AE)has been manifested apart from the law, although (AF)the Law and the Prophets bear witness to it— 22 the righteousness of God (AG)through faith in Jesus Christ for all who believe. (AH)For there is no distinction: 23 for (AI)all have sinned and fall short of the glory of God, 24 (AJ)and are justified (AK)by his grace as a gift, (AL)through the redemption that is in Christ Jesus, 25 whom God (AM)put forward as (AN)a propitiation (AO)by his blood, to be received by faith. This was to show God's righteousness, because in (AP)his divine forbearance he had passed over (AQ)former sins. 26 It was to show his righteousness at the present time, so that he might be just and the justifier of the one who has faith in Jesus.
27 (AR)Then what becomes of our boasting? It is excluded. By what kind of law? By a law of works? No, but by the law of faith. 28 For we hold that one is justified by faith (AS)apart from works of the law. 29 Or (AT)is God the God of Jews only? Is he not the God of Gentiles also? Yes, of Gentiles also, 30 since (AU)God is one—who will justify the circumcised by faith and (AV)the uncircumcised through faith. 31 Do we then overthrow the law by this faith? By no means! On the contrary, we uphold the law.
Footnotes
- Romans 3:9 Greek Are we
- Romans 3:9 Or at any disadvantage?
- Romans 3:20 Greek flesh
Romans 3
King James Version
3 What advantage then hath the Jew? or what profit is there of circumcision?
2 Much every way: chiefly, because that unto them were committed the oracles of God.
3 For what if some did not believe? shall their unbelief make the faith of God without effect?
4 God forbid: yea, let God be true, but every man a liar; as it is written, That thou mightest be justified in thy sayings, and mightest overcome when thou art judged.
5 But if our unrighteousness commend the righteousness of God, what shall we say? Is God unrighteous who taketh vengeance? (I speak as a man)
6 God forbid: for then how shall God judge the world?
7 For if the truth of God hath more abounded through my lie unto his glory; why yet am I also judged as a sinner?
8 And not rather, (as we be slanderously reported, and as some affirm that we say,) Let us do evil, that good may come? whose damnation is just.
9 What then? are we better than they? No, in no wise: for we have before proved both Jews and Gentiles, that they are all under sin;
10 As it is written, There is none righteous, no, not one:
11 There is none that understandeth, there is none that seeketh after God.
12 They are all gone out of the way, they are together become unprofitable; there is none that doeth good, no, not one.
13 Their throat is an open sepulchre; with their tongues they have used deceit; the poison of asps is under their lips:
14 Whose mouth is full of cursing and bitterness:
15 Their feet are swift to shed blood:
16 Destruction and misery are in their ways:
17 And the way of peace have they not known:
18 There is no fear of God before their eyes.
19 Now we know that what things soever the law saith, it saith to them who are under the law: that every mouth may be stopped, and all the world may become guilty before God.
20 Therefore by the deeds of the law there shall no flesh be justified in his sight: for by the law is the knowledge of sin.
21 But now the righteousness of God without the law is manifested, being witnessed by the law and the prophets;
22 Even the righteousness of God which is by faith of Jesus Christ unto all and upon all them that believe: for there is no difference:
23 For all have sinned, and come short of the glory of God;
24 Being justified freely by his grace through the redemption that is in Christ Jesus:
25 Whom God hath set forth to be a propitiation through faith in his blood, to declare his righteousness for the remission of sins that are past, through the forbearance of God;
26 To declare, I say, at this time his righteousness: that he might be just, and the justifier of him which believeth in Jesus.
27 Where is boasting then? It is excluded. By what law? of works? Nay: but by the law of faith.
28 Therefore we conclude that a man is justified by faith without the deeds of the law.
29 Is he the God of the Jews only? is he not also of the Gentiles? Yes, of the Gentiles also:
30 Seeing it is one God, which shall justify the circumcision by faith, and uncircumcision through faith.
31 Do we then make void the law through faith? God forbid: yea, we establish the law.
Romanos 3
Almeida Revista e Corrigida 2009
O privilégio dos judeus. A justiça de Deus
3 Qual é, logo, a vantagem do judeu? Ou qual a utilidade da circuncisão? 2 Muita, em toda maneira, porque, primeiramente, as palavras de Deus lhe foram confiadas. 3 Pois quê? Se alguns foram incrédulos, a sua incredulidade aniquilará a fidelidade de Deus? 4 De maneira nenhuma! Sempre seja Deus verdadeiro, e todo homem mentiroso, como está escrito: Para que sejas justificado em tuas palavras e venças quando fores julgado.
5 E, se a nossa injustiça for causa da justiça de Deus, que diremos? Porventura, será Deus injusto, trazendo ira sobre nós? (Falo como homem.) 6 De maneira nenhuma! Doutro modo, como julgará Deus o mundo? 7 Mas, se pela minha mentira abundou mais a verdade de Deus para glória sua, por que sou eu ainda julgado também como pecador? 8 E por que não dizemos (como somos blasfemados, e como alguns dizem que dizemos): Façamos males, para que venham bens? A condenação desses é justa.
Todos os homens estão debaixo do pecado
9 Pois quê? Somos nós mais excelentes? De maneira nenhuma! Pois já dantes demonstramos que, tanto judeus como gregos, todos estão debaixo do pecado, 10 como está escrito: Não há um justo, nem um sequer. 11 Não há ninguém que entenda; não há ninguém que busque a Deus. 12 Todos se extraviaram e juntamente se fizeram inúteis. Não há quem faça o bem, não há nem um só. 13 A sua garganta é um sepulcro aberto; com a língua tratam enganosamente; peçonha de áspides está debaixo de seus lábios; 14 cuja boca está cheia de maldição e amargura. 15 Os seus pés são ligeiros para derramar sangue. 16 Em seus caminhos há destruição e miséria; 17 e não conheceram o caminho da paz. 18 Não há temor de Deus diante de seus olhos.
19 Ora, nós sabemos que tudo o que a lei diz aos que estão debaixo da lei o diz, para que toda boca esteja fechada e todo o mundo seja condenável diante de Deus. 20 Por isso, nenhuma carne será justificada diante dele pelas obras da lei, porque pela lei vem o conhecimento do pecado.
A justificação pela fé em Jesus Cristo
21 Mas, agora, se manifestou, sem a lei, a justiça de Deus, tendo o testemunho da Lei e dos Profetas, 22 isto é, a justiça de Deus pela fé em Jesus Cristo para todos e sobre todos os que creem; porque não há diferença. 23 Porque todos pecaram e destituídos estão da glória de Deus, 24 sendo justificados gratuitamente pela sua graça, pela redenção que há em Cristo Jesus, 25 ao qual Deus propôs para propiciação pela fé no seu sangue, para demonstrar a sua justiça pela remissão dos pecados dantes cometidos, sob a paciência de Deus; 26 para demonstração da sua justiça neste tempo presente, para que ele seja justo e justificador daquele que tem fé em Jesus.
27 Onde está, logo, a jactância? É excluída. Por qual lei? Das obras? Não! Mas pela lei da fé. 28 Concluímos, pois, que o homem é justificado pela fé, sem as obras da lei. 29 É, porventura, Deus somente dos judeus? E não o é também dos gentios? Também dos gentios, certamente. 30 Se Deus é um só, que justifica, pela fé, a circuncisão e, por meio da fé, a incircuncisão, 31 anulamos, pois, a lei pela fé? De maneira nenhuma! Antes, estabelecemos a lei.
© 2017 Bible League International
The ESV® Bible (The Holy Bible, English Standard Version®), © 2001 by Crossway, a publishing ministry of Good News Publishers. ESV Text Edition: 2025.
Copyright 2009 Sociedade Bíblica do Brasil. Todos os direitos reservados / All rights reserved.
