Warumi 2
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Huwezi Kuwahukumu Wengine
2 Je, unadhani unaweza kuwahukumu watu wengine? Unakosea. Wewe pia una hatia ya dhambi. Unawahukumu kwa kuwa wanatenda mabaya, lakini wewe unatenda yale wanayotenda. Hivyo unapowahukumu, unajihukumu wewe mwenyewe. 2 Lakini tunajua kwamba Mungu yuko sahihi kwa kuwahukumu wote wanaotenda mambo ya jinsi hiyo! 3 Lakini kwa kuwa unatenda mambo sawa na wale unaowahukumu, hakika unaelewa kuwa Mungu atakuadhibu nawe pia. Unawezaje kufikiri kuwa utaiepuka hukumu yake? 4 Mungu amekuwa mwema kwako. Na amekuwa mvumilivu sana, akisubiri ubadilike. Lakini haufikirii jambo lolote kuhusu wema wake mkuu. Pengine huelewi kwamba Mungu ni mwema kwako ili ubadili moyo na maisha yako.
5 Lakini wewe ni mkaidi sana! Unakataa kubadilika. Hivyo unaikuza hukumu yako wewe mwenyewe zaidi na zaidi. Utahukumiwa siku ile ambapo Mungu ataonesha hasira yake. Siku ambayo kila mtu ataona Mungu anavyowahukumu watu kwa haki.[a] 6 Kama anavyosema, “Atamlipa au kumwadhibu kila mtu kutokana na matendo yale.”(A) 7 Watu wengine hawachoki kutenda mema. Wanaishi kwa ajili ya utukufu na heshima kutoka kwa Mungu na kwa ajili ya maisha yasiyoweza kuharibiwa. Mungu atawapa watu hao uzima wa milele. 8 Lakini wengine hutenda mambo yanayowafurahisha wao wenyewe. Hivyo hukataa yaliyo haki na huchagua kutenda mabaya. Watateseka kwa hukumu ya Mungu yenye hasira. 9 Matatizo na mateso yatampata kila mmoja anayetenda uovu; kuanzia Wayahudi kwanza kisha wale wasio Wayahudi. 10 Lakini atampa utukufu, heshima na amani kila atendaye mema; wale wote wanaotenda mema; kuanzia Wayahudi kwanza kisha wale wasio Wayahudi. 11 Ndiyo, Mungu humhukumu kila mtu pasipo upendeleo, bila kujali yeye ni nani.
12 Watu walio na sheria na wote ambao hawajawahi kuisikia sheria, wote wako sawa wanapotenda dhambi. Watu wasio na sheria na ni watenda dhambi wataangamizwa. Vivyo hivyo, wale walio na sheria na ni watenda dhambi watahukumiwa kuwa na hatia kwa kutumia sheria. 13 Kuisikia sheria hakuwafanyi watu wawe wenye haki kwa Mungu. Wanakuwa wenye haki mbele zake, pale wanapotekeleza kile kinachoagizwa na sheria.
14 Fikirini kuhusu wasio Wahayudi ambao hawakukua wakiwa na sheria. Wanapotenda kama sheria inavyoamuru,[b] wanakuwa kielelezo cha sheria, ijapokuwa hawana sheria iliyoandikwa. 15 Wanaonesha kuwa wanafahamu kilicho sahihi na kibaya, kama sheria inavyoamuru na dhamiri zao zinakubali. Lakini wakati mwingine mawazo yao huwaambia kuwa wamekosea au wamefanya sahihi. 16 Hivi ndivyo itakavyokuwa siku ambayo Mungu atazihukumu siri za watu kupitia Yesu Kristo, sawasawa na Habari Njema ninayoihubiri.
Wayahudi na Sheria
17 Wewe unajiita Myahudi, na unajiona upo salama kwa kuwa tu una sheria. Kwa majivuno unadai kuwa wewe ni mmoja wa wateule wa Mungu. 18 Unajua yale ambayo Mungu anataka ufanye. Na unajua yaliyo muhimu, kwa sababu umejifunza sheria. 19 Unadhani kuwa wewe ni kiongozi wa watu wasioweza kuiona njia sahihi, na nuru kwa wale walio gizani. 20 Unafikiri unaweza kuwaonesha wajinga kilicho sahihi. Na unadhani kuwa wewe ni mwalimu wa wanaoanza kujifunza. Unayo sheria, na hivyo unadhani unajua kila kitu na una kweli yote. 21 Unawafundisha wengine, sasa kwa nini usijifundishe wewe wenyewe? Unawaambia usiibe, lakini wewe mwenyewe unaiba. 22 Unasema wasizini, lakini wewe mwenyewe una hatia ya dhambi hiyo. Unachukia sanamu, lakini unaziiba sanamu katika mahekalu yao. 23 Unajivuna sana kwamba una sheria ya Mungu, lakini unamletea Mungu aibu kwa kuivunja sheria yake. 24 Kama Maandiko yanavyosema, “Watu wa mataifa mengine wanamtukana Mungu kwa sababu yako.”[c]
25 Ikiwa mnaifuata sheria, basi kutahiriwa kwenu kuna maana. Lakini mkiivunja sheria, mnakuwa kama watu ambao hawakutahiriwa. 26 Wale wasiokuwa Wayahudi hawatahiriwi. Lakini wakiifuata sheria inavyosema, wanakuwa kama watu waliotahiriwa. 27 Mnayo sheria na tohara, lakini mnaivunja sheria. Hivyo wale wasiotahiriwa katika miili yao, lakini bado wanaitii sheria, wataonesha kuwa mna hatia.
28 Wewe si Myahudi halisi ikiwa utakuwa Myahudi tu kwa nje. Tohara halisi si ile ya nje ya mwili tu. 29 Myahudi halisi ni yule aliye Myahudi kwa ndani. Tohara halisi inafanywa moyoni. Ni kitu kinachofanywa na Roho, na hakifanyiki ili kufuata sheria iliyoandikwa. Na yeyote aliyetahiriwa moyoni kwa Roho hupata sifa kutoka kwa Mungu, siyo kutoka kwa watu.
Warumi 2
Neno: Bibilia Takatifu
Hukumu Ya Mungu
2 Kwa hiyo huna udhuru wo wote, hata ukiwa nani, unapowahu kumu wengine. Kwa maana unapowahukumu wengine unajihukumu mwe nyewe, kwa kuwa wewe uliye hakimu unafanya mambo hayo hayo. 2 Tunajua kwamba hukumu ya Mungu huwafikia kwa halali wote wanaotenda mambo haya. 3 Je, wewe uliye binadamu tu, unapowahuku mu watu wanaofanya mambo hayo na huku wewe mwenyewe pia unafanya hayo hayo, unadhani utaepuka hukumu ya Mungu? 4 Au labda unad harau wingi wa huruma, uvumilivu na subira ya Mungu, ukasahau kwamba wema wake una shabaha ya kukufanya utubu?
5 Lakini kwa sababu ya ugumu na ukaidi wa moyo wako usioku bali kutubu, unajiwekea ghadhabu kwa siku ile ambapo ghadhabu ya Mungu na hukumu yake ya haki itadhihirishwa. 6 Siku hiyo, Mungu atamlipa kila mtu kulingana na matendo yake. 7 Wale ambao hutenda wema wakati wote na kutafuta utukufu, heshima na maisha yasiyo haribika, Mungu atawapa uzima wa milele. 8 Lakini wote watafu tao kujinufaisha, wanaokataa kweli na kufuatauovu, watapokea ghadhabu na hasira ya Mungu. 9 Kwa maana kila binadamu atendaye uovu atapata mateso na shida, kuanzia kwa Myahudi na kisha kwa mtu wa mataifa mengine. 10 Lakini Mungu atawapa utukufu, heshima na amani wote watendao mema; Wayahudi kwanza na kisha watu wa mataifa mengine. 11 Kwa maana Mungu hana upendeleo.
12 Watu wote waliotenda dhambi pasipokuwa na sheria ya Musa wataangamia pasipo sheria; na wale wote waliotenda dhambi chini ya sheria ya Musa watahukumiwa kwa sheria iyo hiyo. 13 Kwa maana wanaohesabiwa haki mbele ya Mungu si wale wanaosikia bali ni wal ewanaotii maagizo ya sheria. 14 Watu wa mataifa mengine ambao hawana sheria ya Musa, wanapoamua kutenda yale ambayo yameagizwa na sheria kwa kuongozwa na dhamiri zao, wao wenyewe wanakuwa wamejiwekea sheria, ingawa hawana sheria ya Musa. 15 Kwa jinsi hii matendo yao yanaonyesha kwamba yale yaliyoagizwa katika she ria ya Musa yameandikwa ndani ya mioyo yao. Dhamiri zao pia hush uhudia hivyo; kwa maana mawazo yao mara nyingine huwashtaki na mara nyingine huwatetea. 16 Kwa hiyo, kama Habari Njema ninay ohubiri inavyosema, hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile ambayo Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo, atayahukumu mawazo ya siri ya wanadamu.
Wayahudi Na Sheria Ya Musa
17 Na wewe je? Wewe unayejiita Myahudi: unaitegemea sheria ya Musa na kujisifia uhusiano wako na Mungu; 18 unajua mapenzi ya Mungu na unatambua lililo bora kutokana na hiyo sheria. 19 Kama unatambua kuwa wewe ni kiongozi wa vipofu na mwanga kwa wale walioko gizani; 20 mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa watoto wachanga, kwa kuwa una hakika kwamba ndani ya hiyo sheria mna maarifa na kweli yote: 21 wewe unayewafundisha wengine, mbona hujifunzi mwenyewe? Wewe unayehubiri kwamba watu wasiibe, wewe huibi? 22 Wewe unayewaambia watu wasizini, wewe huzini? Wewe uchukiaye miungu ya sanamu, huibi katika mahekalu? 23 Wewe unayejisifia sheria, humwaibishi Mungu kwa kuvunja sheria? 24 Kwa maana Maandiko yanasema, “Kwa ajili yenu ninyi Wayahudi, jina la Mungu linatukanwa miongoni mwa mataifa ya watu wasiom jua Mungu.”
25 Kutahiriwa kuna thamani tu iwapo unatii sheria, lakini kama unavunja sheria, umekuwa kama hukutahiriwa. 26 Kwa hiyo kama watu ambao hawakutahiriwa wanatimiza maagizo ya she ria, je, Mungu hatawahesabu kuwa kama waliotahiriwa? 27 Ndipo wale ambao kimwili hawakutahiriwa lakini wanatii sheria watawa hukumu ninyi mlio na Maandiko ya sheria nakutahiriwa lakini mna vunja sheria. 28 Kwamaana Myahudi wa kweli si yule anayeonekana kwa dalili za nje, wala tohara ya kweli si kitu cha kimwili. 29 Myahudi wa kweli ni yule aliye Myahudi kwa ndani, na tohara ya kweli ni jambo la moyoni, jambo la kiroho, wala si la sheria iliyoandikwa. Mtu wa jinsi hii anapata sifa kutoka kwa Mungu, wala si kutoka kwa wanadamu.
Romans 2
New International Version
God’s Righteous Judgment
2 You, therefore, have no excuse,(A) you who pass judgment on someone else, for at whatever point you judge another, you are condemning yourself, because you who pass judgment do the same things.(B) 2 Now we know that God’s judgment against those who do such things is based on truth. 3 So when you, a mere human being, pass judgment on them and yet do the same things, do you think you will escape God’s judgment? 4 Or do you show contempt for the riches(C) of his kindness,(D) forbearance(E) and patience,(F) not realizing that God’s kindness is intended to lead you to repentance?(G)
5 But because of your stubbornness and your unrepentant heart, you are storing up wrath against yourself for the day of God’s wrath(H), when his righteous judgment(I) will be revealed. 6 God “will repay each person according to what they have done.”[a](J) 7 To those who by persistence in doing good seek glory, honor(K) and immortality,(L) he will give eternal life.(M) 8 But for those who are self-seeking and who reject the truth and follow evil,(N) there will be wrath and anger.(O) 9 There will be trouble and distress for every human being who does evil:(P) first for the Jew, then for the Gentile;(Q) 10 but glory, honor and peace for everyone who does good: first for the Jew, then for the Gentile.(R) 11 For God does not show favoritism.(S)
12 All who sin apart from the law will also perish apart from the law, and all who sin under the law(T) will be judged by the law. 13 For it is not those who hear the law who are righteous in God’s sight, but it is those who obey(U) the law who will be declared righteous. 14 (Indeed, when Gentiles, who do not have the law, do by nature things required by the law,(V) they are a law for themselves, even though they do not have the law. 15 They show that the requirements of the law are written on their hearts, their consciences also bearing witness, and their thoughts sometimes accusing them and at other times even defending them.) 16 This will take place on the day when God judges people’s secrets(W) through Jesus Christ,(X) as my gospel(Y) declares.
The Jews and the Law
17 Now you, if you call yourself a Jew; if you rely on the law and boast in God;(Z) 18 if you know his will and approve of what is superior because you are instructed by the law; 19 if you are convinced that you are a guide for the blind, a light for those who are in the dark, 20 an instructor of the foolish, a teacher of little children, because you have in the law the embodiment of knowledge and truth— 21 you, then, who teach others, do you not teach yourself? You who preach against stealing, do you steal?(AA) 22 You who say that people should not commit adultery, do you commit adultery? You who abhor idols, do you rob temples?(AB) 23 You who boast in the law,(AC) do you dishonor God by breaking the law? 24 As it is written: “God’s name is blasphemed among the Gentiles because of you.”[b](AD)
25 Circumcision has value if you observe the law,(AE) but if you break the law, you have become as though you had not been circumcised.(AF) 26 So then, if those who are not circumcised keep the law’s requirements,(AG) will they not be regarded as though they were circumcised?(AH) 27 The one who is not circumcised physically and yet obeys the law will condemn you(AI) who, even though you have the[c] written code and circumcision, are a lawbreaker.
28 A person is not a Jew who is one only outwardly,(AJ) nor is circumcision merely outward and physical.(AK) 29 No, a person is a Jew who is one inwardly; and circumcision is circumcision of the heart,(AL) by the Spirit,(AM) not by the written code.(AN) Such a person’s praise is not from other people, but from God.(AO)
Footnotes
- Romans 2:6 Psalm 62:12; Prov. 24:12
- Romans 2:24 Isaiah 52:5 (see Septuagint); Ezek. 36:20,22
- Romans 2:27 Or who, by means of a
Romans 2
New King James Version
God’s Righteous Judgment
2 Therefore you are (A)inexcusable, O man, whoever you are who judge, (B)for in whatever you judge another you condemn yourself; for you who judge practice the same things. 2 But we know that the judgment of God is according to truth against those who practice such things. 3 And do you think this, O man, you who judge those practicing such things, and doing the same, that you will escape the judgment of God? 4 Or do you despise (C)the riches of His goodness, (D)forbearance, and (E)longsuffering, (F)not knowing that the goodness of God leads you to repentance? 5 But in accordance with your hardness and your [a]impenitent heart (G)you are [b]treasuring up for yourself wrath in the day of wrath and revelation of the righteous judgment of God, 6 who (H)“will render to each one according to his deeds”: 7 eternal life to those who by patient continuance in doing good seek for glory, honor, and immortality; 8 but to those who are self-seeking and (I)do not obey the truth, but obey unrighteousness—indignation and wrath, 9 tribulation and anguish, on every soul of man who does evil, of the Jew (J)first and also of the [c]Greek; 10 (K)but glory, honor, and peace to everyone who works what is good, to the Jew first and also to the Greek. 11 For (L)there is no partiality with God.
12 For as many as have sinned without law will also perish without law, and as many as have sinned in the law will be judged by the law 13 (for (M)not the hearers of the law are just in the sight of God, but the doers of the law will be justified; 14 for when Gentiles, who do not have the law, by nature do the things in the law, these, although not having the law, are a law to themselves, 15 who show the (N)work of the law written in their hearts, their (O)conscience also bearing witness, and between themselves their thoughts accusing or else excusing them) 16 (P)in the day when God will judge the secrets of men (Q)by Jesus Christ, (R)according to my gospel.
The Jews Guilty as the Gentiles
17 [d]Indeed (S)you are called a Jew, and (T)rest[e] on the law, (U)and make your boast in God, 18 and (V)know His will, and (W)approve the things that are excellent, being instructed out of the law, 19 and (X)are confident that you yourself are a guide to the blind, a light to those who are in darkness, 20 an instructor of the foolish, a teacher of babes, (Y)having the form of knowledge and truth in the law. 21 (Z)You, therefore, who teach another, do you not teach yourself? You who preach that a man should not steal, do you steal? 22 You who say, “Do not commit adultery,” do you commit adultery? You who abhor idols, (AA)do you rob temples? 23 You who (AB)make your boast in the law, do you dishonor God through breaking the law? 24 For (AC)“the name of God is (AD)blasphemed among the Gentiles because of you,” as it is written.
Circumcision of No Avail
25 (AE)For circumcision is indeed profitable if you keep the law; but if you are a breaker of the law, your circumcision has become uncircumcision. 26 Therefore, (AF)if an uncircumcised man keeps the righteous requirements of the law, will not his uncircumcision be counted as circumcision? 27 And will not the physically uncircumcised, if he fulfills the law, (AG)judge you who, even with your [f]written code and circumcision, are a transgressor of the law? 28 For (AH)he is not a Jew who is one outwardly, nor is circumcision that which is outward in the flesh; 29 but he is a Jew (AI)who is one inwardly; and (AJ)circumcision is that of the heart, (AK)in the Spirit, not in the letter; (AL)whose [g]praise is not from men but from God.
Footnotes
- Romans 2:5 unrepentant
- Romans 2:5 storing
- Romans 2:9 Gentile
- Romans 2:17 NU But if
- Romans 2:17 rely
- Romans 2:27 Lit. letter
- Romans 2:29 A play on words—Jew is literally praise.
© 2017 Bible League International
Copyright © 1989 by Biblica
Holy Bible, New International Version®, NIV® Copyright ©1973, 1978, 1984, 2011 by Biblica, Inc.® Used by permission. All rights reserved worldwide.
NIV Reverse Interlinear Bible: English to Hebrew and English to Greek. Copyright © 2019 by Zondervan.
Scripture taken from the New King James Version®. Copyright © 1982 by Thomas Nelson. Used by permission. All rights reserved.

