Kutokuamini Kwa Waisraeli

10 Ndugu zangu, shauku ya moyo wangu na maombi yangu kwa Mungu ni kwamba Waisraeli waokolewe. Ninashuhudia wazi kwamba wao wanajuhudi kubwa ya kumtumikia Mungu, lakini juhudi yao haitokani na kuelewa. Wameshindwa kuelewa haki itokayo kwa Mu ngu, na badala yake wakajaribu kujiwekea ya kwao; kwa hiyo hawa kutii haki ya Mungu. Kwa maana Kristo amekamilisha sheria ili kila mtu mwenye imani ahesabiwe haki.

Wokovu Ni Kwa Wote

Musa anaandika kwamba mtu anayejaribu kutenda haki kwa msingi wa sheria ataishi kwa sheria. Lakini haki itokanayo na imani husema hivi, “Usiseme nafsini mwako, ‘Ni nani atapaa mbi nguni?”’ yaani kumleta Kristo duniani, au “‘Ni nani atashuka kuzimuni?”’yaani kumleta Kristo kutoka kwa wafu. Bali inasema hivi, “Neno la Mungu liko karibu nawe; liko mdomoni mwako na moyoni mwako,” yaani, neno la imani tunayohubiri. Kama ukikiri kwa kinywa chako kuwa Yesu ni Bwana na ukiamini moyoni mwako kuwa Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka. 10 Kwa maana mtu ana poamini moyoni mwake huhesabiwa haki, na anapokiri kwa kinywa chake, huokolewa. 11 Kama yasemavyo Maandiko, “Hakuna amwami niye ambaye ataaibika.” 12 Kwa maana hakuna tofauti kati ya wote naye huwabariki wote wamwitao. 13 Kwa maana, “Kila mtu atakayeliita Jina la Bwana, ataokoka.”

Read full chapter

18 Wale viongozi wa Wayahudi hawakuamini ya kuwa yule mtu aliwahi kuwa kipofu, mpaka walipoamuru wazazi wake waletwe; 19 wakawauliza, “Je, huyu ni mtoto wenu ambaye alizaliwa kipofu? Ikiwa ndiye, imekuwaje sasa anaweza kuona?” 20 Wazazi wake wakajibu, “Tunajua ya kuwa huyu ni mtoto wetu ambaye ali zaliwa kipofu. 21 Lakini hatujui jinsi alivyoponywa akaweza kuona, wala hatujui ni nani aliyemwezesha kuona. Mwulizeni, yeye ni mtu mzima na anaweza kujieleza mwenyewe.” 22 Walisema hivi kwa tahadhari kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wamekubal iana kuwa mtu ye yote atakayetamka kuwa Yesu ndiye Kristo atafu kuzwa kutoka katika ushirika wa sinagogi. 23 Ndio maana wakasema “Mwulizeni, yeye ni mtu mzima.”

24 Kwa hiyo kwa mara ya pili wakamwita yule aliyekuwa kipofu wakamwambia, “Tuambie kweli mbele ya Mungu. Sisi tunafahamu kuwa mtu huyu ni mwenye dhambi.” 25 Akawajibu, “Kama yeye ni mwenye dhambi au sio, mimi sijui. Lakini nina hakika na jambo moja: nil ikuwa kipofu na sasa naona.”

26 Wakamwuliza, “Alikufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?” 27 Akawajibu, “Nimekwisha waambia aliyonifanyia lakini hamtaki kusikia. Mbona mnataka niwaeleze tena? Au na ninyi mna taka kuwa wafuasi wake?” 28 Ndipo wakamtukana na kusema, “Wewe ni mfuasi wake. Sisi ni wafuasi wa Musa. 29 Tunajua kwamba Mungu alisema na Musa. Lakini huyu mtu hatujui anakotoka.” 30 Akawa jibu, “Hii kweli ni ajabu! Hamjui anakotoka naye ameniponya upofu wangu! 31 Tunajua ya kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini huwasikiliza wote wanaomwabudu na kumtii. 32 Haijawahi kutokea tangu ulimwengu kuumbwa kwamba mtu amemponya kipofu wa kuzaliwa. 33 Kama huyu mtu hakutoka kwa Mungu, asingeweza kufa nya lo lote.” 34 Wao wakamjibu, Wewe ulizaliwa katika dhambi! Utawezaje kutufundisha?” Wakamfukuzia nje.

Vipofu Wa Kiroho

35 Yesu alipopata habari kuwa yule mtu aliyemfumbua macho amefukuzwa kutoka katika sinagogi, alimtafuta akamwuliza, “Je, unamwamini Mwana wa Adamu?” 36 Yule mtu akamjibu, “Tafadhali nifahamishe yeye ni nani ili nipate kumwamini.” 37 Yesu akam jibu “Umekwisha mwona naye ni mimi ninayezungumza nawe.” 38 Yule mtu akamjibu huku akipiga magoti, “Bwana, naamini.”

39 Yesu akasema, “Nimekuja ulimwenguni kutoa hukumu; ili wale walio vipofu wapate kuona; na wale wanaodhani wanaona, waonekane kuwa vipofu.”

40 Baadhi ya Mafarisayo waliomsikia akisema hivi wakauliza, “Je, unataka kusema kuwa sisi pia ni vipofu?” 41 Yesu akawa jibu, “Kama mngekuwa vipofu kweli, hamngekuwa na hatia. Lakini kwa kuwa mnasema, ‘Tunaona,’ basi bado mna hatia.”

Read full chapter