Add parallel Print Page Options

Salamu kutoka kwa mtume Paulo. Sikutumwa na kundi lolote la watu au mtu yeyote hapa duniani niwe mtume. Sikupewa mamlaka yangu na mwanadamu yeyote. Nilipewa mamlaka haya moja kwa moja kutoka kwa Kristo Yesu[a] na Mungu Baba, aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu. Salamu pia kutoka kwa wote walio familia ya Mungu, walio pamoja nami.

Kwa makanisa yaliyoko Galatia:[b]

Read full chapter

Footnotes

  1. 1:1 Kristo Yesu Au “Mfalme Yesu”. Neno “Kristo” ni tafsiri ya Kiyunani ya neno la Kiebrania “Masihi”, ambao ni wadhifa wa kifalme. Tazama Mk 15:32: Lk 23:2. Tazama pia Kristo na Masihi katika Orodha ya Maneno.
  2. 1:2 Galatia Yamkini ni eneo ambako Paulo alianzisha makanisa katika safari yake ya kwanza ya kitume. Soma Mdo 13 na 14. Au katika safari yake ya pili ya kitume katika Mdo 16:6.