Muwe Na Umoja, Furaha Na Amani

Kwa hiyo ndugu zangu wapendwa, ninaotamani mno kuwaona; ninyi ambao ni furaha yangu na taji yangu, hivi ndivyo mnavyop aswa kusimama imara katika Bwana. Nawasihi Euodia na Sintike wapatane katika Bwana. Na wewe ndugu yangu uliye mwaminifu katika Bwana, nakuomba uwasaidie hawa akina mama, kwa maana wame fanya kazi ya kueneza Injili kwa bidii wakiwa nami pamoja na Kle menti na watumishi wenzangu wengine, ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.

Furahini katika Bwana siku zote, tena nasema furahini! Upole wenu ufahamike kwa watu wote. Bwana anakaribia kuja. Msifadhaike juu ya jambo lo lote; lakini katika kila jambo mjulisheni Mungu haja zenu, kwa kusali na kuomba pamoja na kushu kuru Na amani ya Mungu, ambayo inapita ufahamu wote, italinda mioyo yenu na nia zenu kwa Kristo Yesu.

Hatimaye ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo na sifa, yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote ya kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo uzuri wo wote, pakiwepo na cho chote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo. Mambo yote mliyojifunza au kupokea au kusikia kutoka kwangu, au kuyaona kwangu, yatekelezeni. Na Mungu wa amani ata kuwa pamoja nanyi. 10 Nina furaha kubwa katika Bwana kwa maana hatimaye mmeanza tena kunikumbuka. Kusema kweli mmekuwa mkinikum buka lakini mlikuwa hamjapata nafasi ya kuonyesha upendo wenu. 11 Sisemi hivyo kwa sababu nahitaji kitu, la. Kwa maana nimeji funza kuridhika katika hali yo yote niliyo nayo. 12 Nimepata kupungukiwa, pia nimepata kuwa na wingi wa vitu. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa shibe na wakati wa njaa; wakati wa kuwa na wingi wa vitu na wakati wa kupungukiwa. 13 Naweza kufanya mambo yote katika yeye anipaye nguvu.

14 Hata hivyo, mlifanya vizuri kunisaidia kwa kushirikiana nami katika taabu zangu. 15 Ninyi ndugu zangu Wafilipi mnajua kwamba nilipoanza kuhubiri Injili, nilipokuwa natoka Makedonia, hakuna kanisa lililoshirikiana nami katika kutoa na kupokea isi pokuwa ninyi. 16 Hata nilipokuwa Thesalonike, mliniletea msaada zaidi ya mara moja. 17 Msifikiri kwamba napenda sana kupokea zawadi, sivyo. Ninachotaka kuona ni matunda ambayo kama yak iongezeka ni faida kwenu. 18 Nimekwishapokea malipo yangu yote na ziada. Sasa ninavyo vitu tele kwa sababu Epafrodita amekwisha niletea zawadi zenu. Hakika zawadi hizi ni matoleo yenye harufu nzuri ya manukato inayokubaliwa na kumpendeza Mungu. 19 Na Mungu wangu atawapeni ninyi kila kitu mnachohitaji kwa kadiri ya uta jiri wake mtukufu katika Kristo Yesu. 20 Mungu wetu na Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amina. 21 Natuma salamu zangu kwa kila mtu wa Mungu katika Kristo Yesu. Ndugu ninaokaa nao pia wanawasalimu. 22 Vile vile watu wote wa Mungu wa hapa na hasa wale wa nyumba ya Kaisari, nao pia wanawasalimu.