Wafilipi 3
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Kristo ni wa Muhimu Zaidi
3 Kwa hiyo sasa, kaka na dada zangu, furahini kwa kuwa ninyi ni wa Bwana. Sisiti kuwaandikia mambo haya haya, kwa sababu yatawasaidia ninyi kuwa imara na salama.
2 Mjihadhari na mbwa, mjihadhari na wafanyakazi waovu, mjihadhari na watu wanaotaka kumkata kila mtu ambaye hajatahiriwa.[a] 3 Lakini sisi ndiyo wenye tohara[b] ya kweli, tunaomwabudu Mungu kupitia Roho wake. Hatutumaini katika namna tulivyo kwa kuzaliwa au kwa yale tuliyoyakamilisha. Tunajivuna kuwa sisi ni milki ya Kristo Yesu. 4 Hata kama ninaweza kujitumainisha mimi mwenyewe, bado sifanyi hivyo. Ikiwa kuna watu wanadhani wana sababu za kutumaini sifa za kibinadamu, wanapaswa kujua kuwa nina sababu zaidi za kufanya hivyo. 5 Nilitahiriwa siku ya nane baada ya kuzaliwa. Mimi ni Myahudi wa kabila la Benjamini. Mimi ni Mwebrania halisi, hata wazazi wangu pia. Nikawa Farisayo na nilitii torati kwa uangalifu sana. 6 Nilikuwa na hamu sana ya kumridhisha Mungu[c] hata nikalitesa kanisa. Kwa usahihi niliitii sheria ya Musa.
7 Wakati fulani mambo haya yote yalikuwa muhimu kwangu. Lakini kwa sababu ya Kristo, sasa ninayachukulia mambo haya yote kuwa yasiyo na thamani. 8 Na si haya tu, lakini sasa ninaelewa kuwa kila kitu ni hasara tu ukilinganisha na thamani kuu zaidi ya kumjua Kristo Yesu, ambaye sasa ni Bwana wangu. Kwa ajili yake nilipoteza kila kitu. Na ninayachukulia yote kama kinyesi, ili nimpate Kristo. 9 Ninataka niwe wake. Katika Kristo ninayo haki mbele za Mungu, lakini kuwa na haki mbele za Mungu hakuji kwa kuitii sheria, Bali inakuja toka kwa Mungu kupitia imani kwa[d] Kristo. Mungu anatumia imani yangu kwa Kristo kunihesabia haki. 10 Ninachotaka ni kumjua Kristo na nguvu iliyomfufua kutoka kwa wafu. Ninataka kushiriki katika mateso yake na kuwa kama yeye hata katika kifo chake. 11 Kisha mimi mwenyewe naweza kuwa na matumaini kwamba nitafufuliwa kutoka kwa wafu.
Kuyafikia Malengo
12 Sisemi kuwa nimekwisha kupata ujuzi huo au kuifikia shabaha ya mwisho. Lakini bado ninajitahidi kuifikia shabaha kwa kuwa ndivyo ambavyo Kristo Yesu anataka nifanye. Ndiyo sababu alinifanya kuwa wake. 13 Kaka na dada zangu, ninajua ya kuwa bado nina safari ndefu. Lakini kuna kitu kimoja ninachofanya, nacho ni kusahau yaliyopita na kujitahidi kwa kadri ninavyoweza kuyafikia malengo yaliyo mbele yangu. 14 Ninaendelea kupiga mbio kuelekea mwisho wa mashindano ili niweze kushinda tuzo ambayo Mungu ameniitia kutoka mbinguni kwa njia ya Kristo Yesu.
15 Sisi sote tuliokua kiroho tunapaswa kufikiri namna hii. Na ikiwa kuna jambo lolote ambalo hamkubaliani nalo, Mungu atalifunua kwenu. 16 Lakini tunapaswa kuendelea kuifuata kweli tuliyonayo tayari.
17 Kaka na dada zangu, unganeni pamoja na mfuate mfano wangu. Mtazame na mjifunze pia kutoka kwa wale wanaoishi katika namna tuliyoionesha kwenu. 18 Wapo wengi ambao mwenendo wao unaonesha kuwa ni adui za msalaba wa Kristo. Nimekwishawaambia kuhusu hao mara nyingi. Na inanifanya nitokwe machozi ninapowaambia kuhusu watu hao sasa. 19 Wanauendea uharibifu kwa namna wanavyoishi. Wanaabudu tamaa za mili yao kana kwamba hizo ndizo Mungu. Wanatenda mambo ya aibu na wanajivuna kwa kutenda mambo hayo. Wanayawazia mambo ya kidunia tu. 20 Lakini sisi tunatawaliwa na serikali iliyoko mbinguni. Tunamsubiri Mwokozi wetu, Bwana wetu Yesu Kristo atakayekuja kutoka mbinguni. 21 Ataibadilisha miili yetu minyenyekevu na kuifanya iwe kama mwili wake yeye mwenyewe, mwili wenye utukufu. Kristo atafanya hivi kwa nguvu yake inayomwezesha kutawala juu ya vyote.
Footnotes
- 3:2 wanaotaka … hajatahiriwa Neno la msingi hapa ni kama “tohara” (tazama Tahiri, kutahiriwa, tohara katika Orodha ya Maneno), Lakini hapa inamaanisha “kukata kiungo cha mwili” au “kukatakata vipande”.
- 3:3 tohara Neno hili limetumika hapa kumaanisha hali ya kiroho. Tazama Tahiri, kutahiriwa, tohara katika Orodha ya Maneno.
- 3:6 hamu sana ya kumridhisha Mungu Kabla Paulo hajawa mwamini katika Yesu kama Mfalme Aliyeteuliwa na Mungu, alidhani kuwa alikuwa na wajibu kama Farisayo mwema wa kuwapinga Wayahudi waliokuwa wafuasi wa Kristo.
- 3:9 imani kwa Au, “uaminifu wa”.
Wafilipi 3
Neno: Bibilia Takatifu
Njia Ya Kweli Ya Wokovu
3 Hatimaye ndugu zangu, furahini katika Bwana. Mimi sichoki kuwaandikieni mambo yale yale niliyokwisha waandikia kwa maana najua kwamba yatakuwa ni kinga kwenu. 2 Jihadharini na watenda maovu, hao mbwa, na wale wanaokaza mafundisho ya kutahiriwa. 3 Sisi tumepokea tohara ya kweli, kwa maana tunamwabudu Mungu katika Roho. Sisi tunaona fahari kwa ajili ya maisha yetu ndani ya Kristo Yesu. Hatuweki matumaini yetu katika mambo ya mwili, 4 ijapokuwa mimi mwenyewe ninazo sababu za kuweka matumaini katika mambo hayo. Kama mtu mwingine ye yote anadhani kuwa anazo sababu za kuweka matumaini yake katika mambo ya mwili, basi mimi ninazo sababu zaidi. 5 Nilitahiriwa siku ya nane, mimi ni Mwis raeli wa kabila la Benjamini; Mwebrania halisi. Kuhusu mambo ya kushika sheria, mimi nilikuwa Mfarisayo; 6 na kwa upande wa juhudi, mimi nilikuwa na bidii katika kutesa kanisa; na kuhusu haki ipatikanayo kwa kutii sheria, mimi nilikuwa sina hatia.
7 Lakini mambo hayo niliyoyaona mwanzo kuwa ni faida kwangu, sasa nayaona kuwa ni hasara kwa ajili ya Kristo. 8 Zaidi ya hayo, nahesabu mambo yote kuwa hasara tupu yakilinganishwa na faida kubwa ninayopata kwa kumjua Kristo Yesu aliye Bwana wangu. Kwa ajili yake nilikubali kupoteza kila kitu na kuona mambo hayo yote kuwa ni takataka ili nipate faida ya kuwa na Kristo; 9 na nikiwa kwake nisionekane kama mtu mwenye haki yake mwenyewe, inayotokana na kushika sheria, bali niwe na ile haki inayotokana na kumwamini Kristo, ambaye yeye ni haki itokayo kwa Mungu inayopatikana kwa imani. 10 Nataka nimjue Kristo na nguvu ya ufufuo wake na nishi riki mateso yake, niwe kama yeye katika kifo chake; 11 na hivyo, kama ikiwezekana, niufikie ufufuo kutoka kwa wafu.
12 Sisemi kwamba nimekwisha kupokea haya yote, au kwamba nimekwisha kuwa mkamilifu, la hasha; bali nazidi kukaza mwendo ili nipate kile ambacho, kwa ajili yake, Kristo amenifanya niwe wake. 13 Ndugu zangu, bado sijihesabu kuwa nimekwisha pata ile zawadi. Lakini jambo moja ninalofanya ni kusahau mambo yote yali yopita, na kukaza mwendo kufikia yaliyo mbele yangu. 14 Nakaza na nifikie ushindi, ili nipate zawadi ambayo Mungu ameniitia mbinguni, nikiwa ndani ya Kristo Yesu.
15 Sisi tuliokomaa kiroho tuwe na msimamo kama huu. Lakini kama kuna mawazo tofauti kuhusu jambo lo lote, Mungu atawafunu lia. 16 Ila tushike sana yale tuliyokwisha kupokea.
17 Ndugu zangu, nawasihi mfuate mfano wangu, na muwatazame wale wanaofuata mfano tuliowapa. 18 Kwa maana, kama nilivyok wisha waambia kabla, na sasa nasema tena kwa machozi, wako watu wengi miongoni mwenu ambao maisha yao yanaonyesha kuwa wao ni adui wa msalaba wa Kristo. 19 Mwisho wa watu hao ni kuangamia, na Mungu wao ni tumbo; kwa sababu wao huyaonea fahari mambo ya aibu na mawazo yao yametawaliwa na mambo ya dunia. 20 Lakini uraia wetu uko mbinguni. Nasi tunangoja kwa hamu Mwokozi kutoka huko, yaani Bwana wetu Yesu Kristo, 21 ambaye, kwa uwezo unaomwezesha kutawala kila kitu, atabadilisha miili yetu midhaifu ili iwe na utukufu kama alionao yeye.
Филипяни 3
Библия, нов превод от оригиналните езици (с неканоничните книги)
Предпазване от лъжеучители
3 (A)И така, братя мои, радвайте се в името на Господа. За мене не е досадно да ви пиша едно и също, а вас ще ви предпазва.
2 Пазете се от злостни деятели, пазете се от тези кучета, пазете се от лъжеобрязването, 3 (B)защото истинското обрязване сме ние, които духовно служим на Бога и се хвалим с Иисус Христос, и не се уповаваме на човешки предимства, 4 (C)(D)макар че аз мога да се уповавам и на човешки предимства. Ако някой друг мисли да се уповава на тях, то още повече аз, 5 (E)(F)който съм обрязан в осмия ден и съм от Израилев род, от Вениаминовото племе, евреин от евреите, по отношение на Закона – фарисей, 6 (G)по усърдие – гонител на църквата, според изискваната от Закона праведност – непорочен. 7 Но това, което беше за мене придобивка, заради Христос го сметнах за загуба. 8 Наистина смятам, че всичко е загуба в сравнение с предимството да се познава Иисус Христос, моят Господ, заради Когото се отрекох от всичко. Всичко за мене е смет, за да придобия Христос 9 и да пребъдвам в Него. Аз търся не своето оправдаване, произхождащо от Закона, а придобиваното чрез вяра в Христос – оправдаването от Бога чрез вярата, 10 (H)за да позная Него и силата на възкресението Му, да споделя страданията Му и да умра подобно на Него, 11 та дано достигна възкресението от мъртвите.
Насърчение за съвършенство
12 Не мисля, че вече съм достигнал нещо или че съм станал съвършен, но се стремя, дано постигна това, заради което Иисус Христос ме завладя. 13 Братя, аз не мисля за себе си, че съм постигнал това; но едно само правя: забравил това, което остана назад, и отправил се към това, което е напред, 14 аз се стремя към целта – към наградата на небесното призоваване от Бога чрез Иисус Христос. 15 И тъй, нека ние, които се стремим към съвършенство, да мислим така; ако ли вие другояче мислите, Бог ще ви разкрие онова, което е правилно. 16 Но по това, до което достигнахме, нека бъдем единомислени и да следваме същото правило[a].
17 (I)Братя, бъдете ми подражатели и насочете поглед към онези, които постъпват по нашия пример. 18 (J)Понеже мнозина, за които често съм ви говорил, а сега дори със сълзи говоря, постъпват като врагове на Христовия кръст. 19 Техният край е гибел, тяхното божество – коремът, а славата – в срама им; мислите им са насочени към земното. 20 А ние сме жители на небесата, откъдето очакваме и Спасителя, нашия Господ Иисус Христос, 21 (K)Който ще преобрази унизеното ни тяло тъй, че то да стане подобно на Неговото славно тяло, със силата, чрез която Той всичко може да покори на Себе Си.
Footnotes
- 3:16 В някои ръкописи липсва: „и да следваме същото правило“.
Philippians 3
King James Version
3 Finally, my brethren, rejoice in the Lord. To write the same things to you, to me indeed is not grievous, but for you it is safe.
2 Beware of dogs, beware of evil workers, beware of the concision.
3 For we are the circumcision, which worship God in the spirit, and rejoice in Christ Jesus, and have no confidence in the flesh.
4 Though I might also have confidence in the flesh. If any other man thinketh that he hath whereof he might trust in the flesh, I more:
5 Circumcised the eighth day, of the stock of Israel, of the tribe of Benjamin, an Hebrew of the Hebrews; as touching the law, a Pharisee;
6 Concerning zeal, persecuting the church; touching the righteousness which is in the law, blameless.
7 But what things were gain to me, those I counted loss for Christ.
8 Yea doubtless, and I count all things but loss for the excellency of the knowledge of Christ Jesus my Lord: for whom I have suffered the loss of all things, and do count them but dung, that I may win Christ,
9 And be found in him, not having mine own righteousness, which is of the law, but that which is through the faith of Christ, the righteousness which is of God by faith:
10 That I may know him, and the power of his resurrection, and the fellowship of his sufferings, being made conformable unto his death;
11 If by any means I might attain unto the resurrection of the dead.
12 Not as though I had already attained, either were already perfect: but I follow after, if that I may apprehend that for which also I am apprehended of Christ Jesus.
13 Brethren, I count not myself to have apprehended: but this one thing I do, forgetting those things which are behind, and reaching forth unto those things which are before,
14 I press toward the mark for the prize of the high calling of God in Christ Jesus.
15 Let us therefore, as many as be perfect, be thus minded: and if in any thing ye be otherwise minded, God shall reveal even this unto you.
16 Nevertheless, whereto we have already attained, let us walk by the same rule, let us mind the same thing.
17 Brethren, be followers together of me, and mark them which walk so as ye have us for an ensample.
18 (For many walk, of whom I have told you often, and now tell you even weeping, that they are the enemies of the cross of Christ:
19 Whose end is destruction, whose God is their belly, and whose glory is in their shame, who mind earthly things.)
20 For our conversation is in heaven; from whence also we look for the Saviour, the Lord Jesus Christ:
21 Who shall change our vile body, that it may be fashioned like unto his glorious body, according to the working whereby he is able even to subdue all things unto himself.
© 2017 Bible League International
Copyright © 1989 by Biblica
Copyright by © Българско библейско дружество 2013. Използвани с разрешение.